Pepshop Kenya Online Marketing Business".

Pepshop Kenya Online Marketing Business". Contact information, map and directions, contact form, opening hours, services, ratings, photos, videos and announcements from Pepshop Kenya Online Marketing Business"., 556, Nairobi.

16/02/2025

Here we are

16/02/2025
16/02/2025

Online selling

06/10/2017

Mchungaji mmoja alijibadili na kuwa omba omba katika viunga vya kanisa alilokuwa akitarajia kutangazwa jumapili hiyo k**a ni mchungaji mpya wa kanisa lile akitokea mji mwingine.
Alitembea kuzunguka lile kanisa akiwa amevaa nguo kukuuu zilizochanika chanika huku akipishana na watu waliokuwa wakiingia kanisani. Ni watu watatu tu ndio waliomsalimia.
Wengine wote hawakutaka hata kumuangalia mara mbili, walipitiliza moja kwa moja na kuingia kanisani.
Aliwaomba watu msaada wa chakula au hela ya kula hakuna hata mmoja aliyempa chochote.
Akaenda katika malango ya kanisa na kukaa katika ngazi akaweka chombo chake ili aguswae atoe msaada lakini hakuna hata mmoja alietoa hata senti moja.
Akainuka na kwenda mbele kabisa ya kanisa, akakaa benchi la kwanza kabisa, mzee wa kanisa akamwambia aondoke pale na akakae nyuma kwa vile ile sehemu ni ya watu maarafu (VIP).
Akaenda nyuma ya kanisa na akakaa benchi la mwisho kabisa lilikowa halina watu, maana wote walionekana kulikwepa. Akiwa amekaa akawa anasikiliza matangazo ya wiki kutoka kwa mzee wa kanisa.
Akasikiliza wageni wapya wakitajwa na kukaribishwa katika kanisa ila hakuna hata mmoja aliyemkaribisha kwa kuwa nae alikuwa mgeni mazingira yale.
Akaendelea kuwatizama watu waliokuwa wakimuangalia na kutoa mshangao ambao ulikuwa na tafsiri kwamba hatakiwi mahala pale.
Baadae kiongozi wa kanisa akaenda pale mbele kutangaza jambo la muhimu. Akasema kwamba anayo furaha kumtambulisha mchungaji mpya mbele ya waumini wote.
Waumini wakasimama na kutizama huku na huku wakiwa wanapiga makofi. Yule ombaomba akasimaa kutokea kule nyuma na kuanza kutembea kuelekea mbele ya aisle.
Kufikia hapo watu wakaacha kupiga makofi na kanisa likawa kimya wote wakimtizama yeye...akatembea mpaka madhabahuni na kuchukua kipaza sauti. Akasimama pale kwa dakika kadhaa, akakohoa kidogo na kunukuu mistari kutoka kitabu kitakatifu cha Mathayo 25:34-40 akaanza
"Kisha mfalme atawaambia wale walio mkono wake wa kuume, Njoni, mliobarikiwa na Baba yangu, urithini ufalme mliowekewa tayari tangu kuumbwa ulimwengu; kwa maana nalikuwa na njaa, mkanipa chakula; nalikuwa na kiu, mkaninywesha; nalikuwa mgeni, mkanikaribisha; nalikuwa uchi, mkanivika, nalikuwa mgonjwa, mkaja kunitizama, nalikuwa kifungoni mkanijia...Ndipo wenye haki watakapomjibu wakisema, Bwana ni lini tulikuona una njaa, tukakulisha au una kiu, tukakunywesha? Tena ni lini tulipokuona u mgeni, tukakukaribisha? Au u uchi tukakuvika? Ni lini tena tulipokuona u mgonjwa au kifungoni tukakujia?
Na mfalme atajibu, akiwaambia, AMIN AMIN NAWAAMBIA. KADIRI MLIVYOMTENDEA MMOJAWAPO WA HAO NDUGU ZANGU WALIO WADOGO, MLINITENDEA MIMI"
Baada ya kunukuu hayo, kwa masikitiko na uchungu mwingi moyoni mwake akajitambulisha mbele yao kwamba yeye ndiye mchungaji mpya wa kanisa lile na kuwaeleza ni nini amejifunza kutoka kwao asubuhi ile.
Wengi wakaanza kulia huku wameinamisha vichwa vyao chini.
Akawaambia "Leo naona ni mkusanyiko wa watu, ila sioni kanisa la Mungu. Dunia inayo watu wengi wa namna yenu, tunaleta mazoea hata kwenye ibada sasa, kimsingi Mungu tunaemuabudu hayupo mioyoni mwetu. Wakristo mnatakiwa muwe wanafunzi wa Yesu kristo wa kufuata mafundisho na kutenda mema k**a yeye alivyofanya. Lini mtaamua kuwa wanafunzi wa Yesu!?
Baada ya kusema hayo akaahirisha ibada mpaka jumapili inayofuata baada ya kutimiza neno la Mungu kupitia vitendo.
______________________________
_____________
Basi wewe uliye mkristo, zitafakari njia zako, kwenda kanisani kila Jumapili haitoshi, tuishi katika misingi ya kweli ya ukristo huku tukiwa na moyo wa kuwasaidia wale wote wasiojiweza.
Mwenyezi Mungu atubariki, tuishi vema sawasawa na vile yeye apendavyo.
Kwanini tusiseme 'Amen
Share na wengine

23/05/2017

keep on checking for new products

03/05/2017

Comming soon

Address

556
Nairobi
0051

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Pepshop Kenya Online Marketing Business". posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share