03/04/2026
*Nilitaka Kumkataa Kinyozi MPYA Kisa Nimezoea Kunyolewa Na Niliyemzoea Kutoka Na Mtindo Aliokuwa Ananinyoa...*
..Mkuu Ukininyoa Vibaya Sikupi Hela
Jamaa Akacheka Sana-kisha Akaniambia Kaa Kwenye Kiti Mdogo Wangu...
..Nikunyoe Nikikunyoa Vibaya Basi
*"Usinipe Hela"*
..In Short Hapa Ambapo Huwa Nanyoa Wanalipisha Tshs 2,000 Tu
Hii ni Wiki Moja Iliyopita
Sikia...
Kuna Somo Nahitaji Tupate kwa Pamoja-kabla Sijakusimulia Hii Story Ya Mimi Na Kinyozi Mpya
Iko Hivii...
Wateja Huwa Hawapendi kujaribishiwa Hata Mara Moja...
..Yaani:
Mteja Aje Kwako Alafu Ajue Huna Uwezo Wa Kumpa Suluhisho Sahihi
Trust Me...
Atakukimbia Tu 🤣
Ngoja Nikuulize Hili Swali Hapa Chini...
..Umeenda Hospitalini Kutibiwa(kufanyiwa Upasuaji)
Alafu...
Unakutana na Madaktari Hawa Wawili...
*Daktari A:* Anasema Mimi Ndio Nimetoka Chuo Muhimbili Jana Tu Nimegraduate Sina Experience Ya Kupasua Watu Nimezoea Tu Kupasua Maiti 🤣💔
*Daktari B:* Mimi Nina Uzoefu wa Miaka 7 Nimefanya Upasuaji kwa Wagonjwa zaidi Ya 200 Na Wote Wamepona Hizi Hapa Shuhuda Zao(Anakuonyesha Portfolio yake)
Kuwa Mkweli Tu Utamchagua Nani Daktari A Au Daktari B?...
Umesema Daktari B Eenh?...
Well:
Hivyo Ndivyo Hata Wateja Huwa Wanachagua...
..Sehemu Pa Kununua Bidhaa Au Huduma Fulani
Let's Back To The Story...
Ilikuwa mida Ya 18:25 Jioni
..Nilikuwa nipo Mitaa Ya Magomeni
Nikaingia Saluni Moja Hivii Ya Kawaida Tu...
..Of Course Huwa Napenda Sana Kwenda Yale Maeneo
Kwasababu...
Yule Anayenyoa Mule Ndani ni Mshikaji Wangu Sana-Pia Ananyoa Vizuri Saaana 😋
Basi Bhana...
Baada ya Kuingia ndani ya Saluni nikakuta Jamaa Anamnyoa mteja Mwingine...
..Ile nimekaa Kwenye Sofa Nakula Kiyoyozi pamoja Na Muziki Wa Celine Dion *"My Heart Will Go On"*
Akaja...
Jamaa Kasokota Rasta...
..Akaniambia Kaa Kwenye Kiti Nikunyoe
Nikamuuliza Ili Kupata Uhakika Unasemaje?...
Kaa Kwenye Kiti Nikunyoe...
Nikamwambia Namsubiria Huyo Mwingine Amalize Ndio Nimezoea Kunyolewa Na Yeye...
..Akaniuliza Hauna Haraka?...
Nikajibu Nina Haraka 🤣
Hapo Tayari Amanipa Sababu Ya Kunyoa Haraka(Kuokoa Muda)
Nikaona Isiwe Kesi Au Vp...
Nikakaa Kwenye Kiti...
..Kabla Hajaanza Madoido Yoyote
Nikamchimba Mkwara 😆
Ukininyoa Vibaya Sikupi Hela yako
..Akasema Fresh
Baada ya Hapo...Hata Kabla Sijawambia Chochote Akaniambia Unanyoa Ngazi Tatu Eeenh?...
Nikajibu Ndio
Nikajiuliza Kimoyo-moyo Huyu Jamaa Kajuaje Aisee 🤣💔
..Kumbe Ana Uzoefu wa Zaidi Ya Miaka 5 Kwenye Field ya Kunyoa
Niwe Mkweli Tu...Nikawa Mpole Mazima
Akaniambia Nipe Dkk 25 Mkuu...
Majibu Utayaona...
Aisee Nilishangazwa Na Ujuzi Aliokuwa nao Huyu Mwamba...
..Alininyoa Vizuri Sana
Na:
Niwe Mkweli Tu Nikampa Hela Kiroho Safi Kabisa...
Je Ni Kwanini Nimekupa Hii Story?...
Well...
Iko Hivii:
Wateja Huwa Wananunua Kwa Watu Ambao Tayari Wana Matokeo Ya Wateja Wengine(Hakikisha Unajenga Portfolio Yako)
Huo ndio utakuwa Mwanzo wa Kuwahudumia Wateja Wengi Zaidi...
Mteja Huwa Hana Shida Kutoa Hela Yake Sehemu ambayo Anajua Anapata Matokeo...
..Na Kinyume Chake Ni Sahihi
Anyways...
I Hope Umepata Value Familia 🫡
Am Your Guy
Vido
As Our Sacred Slogan Says:
*"You Can Either Find A Way Or Make A Way"*