Kusini Yetu Online Tv

Kusini Yetu Online Tv Ukarasa maalum wa habari utakaokuweza kupata taarifa zote zinazotokea ndani na nje ya Tanzania.

08/06/2026

Wapuliziaji wa mikorosho katika Wilaya ya Mkuranga, Mkoa wa Pwani, wamepatiwa mafunzo na Bodi ya Korosho Tanzania (CBT) na TARI, ili kuongeza ufanisi katika matumizi ya viuatilifu na udhibiti wa wadudu na magonjwa ya korosho.

Washiriki wamesema mafunzo hayo yatawawezesha kufanya kazi kwa weledi zaidi, huku Afisa Kilimo wa Chuo cha MATI Mtwara, M***a Rodania, akieleza kuwa elimu hiyo itasaidia wapuliziaji kutambua changamoto mashambani na kuwashauri wakulima kwa usahihi, jambo litakaloongeza uzalishaji na ubora wa korosho.

TIMU YA MAFUNZO YA MATUMIZI SAHIHI YA VIUATILIFU YAWAFIKIA MAAFISA UGANI NEWALA VIJIJINIZoezi la utoaji mafunzo kuhusu m...
07/06/2026

TIMU YA MAFUNZO YA MATUMIZI SAHIHI YA VIUATILIFU YAWAFIKIA MAAFISA UGANI NEWALA VIJIJINI

Zoezi la utoaji mafunzo kuhusu matumizi sahihi na salama ya viuatilifu vya zao la korosho limeendelea katika Halmashauri ya Wilaya ya Newala Vijijini, mkoani Mtwara, likiwahusisha maafisa ugani kutoka maeneo mbalimbali ya wilaya hiyo.

Mafunzo hayo yanatolewa na wataalamu kutoka Mamlaka ya Afya ya Mimea na Viuatilifu Tanzania (TPHPA), kwa kushirikiana na Taasisi ya Utafiti wa Kilimo Tanzania (TARI) pamoja na Bodi ya Korosho Tanzania (CBT), ikiwa ni sehemu ya maandalizi ya msimu wa kilimo wa korosho wa mwaka 2026/27.

Akizungumza baada ya mafunzo hayo, Mtafiti kutoka TARI, Stanslaus Lilai, alisema mafunzo hayo yanalenga kuwawezesha maafisa ugani kutambua kwa usahihi dalili za magonjwa yanayoshambulia mikorosho pamoja na matumizi sahihi ya viuatilifu katika kuyadhibiti.

Alitaja baadhi ya magonjwa hayo kuwa ni Ubwili Unga na Braiti, ambayo yanaweza kusababisha upotevu mkubwa wa mazao endapo hayatadhibitiwa kwa wakati na kwa njia stahiki.

Kwa upande wake, Afisa Kilimo wa Bodi ya Korosho Tanzania, Shinje Ngalula, alisema Serikali inaendelea kutoa pembejeo za kilimo kwa mfumo wa ruzuku sambamba na elimu kwa wakulima na maafisa ugani, kwa lengo la kuongeza tija na kufikia malengo ya kuzalisha zaidi ya tani 700,000 za korosho katika msimu wa mwaka 2026/27.

Nao maafisa ugani walioshiriki mafunzo hayo walisema elimu waliyoipata itawasaidia kuwahudumia wakulima kwa ufanisi zaidi, hasa katika kukabiliana na changamoto zinazojitokeza kabla na wakati wa msimu wa uzalishaji.

Hata hivyo, wamebainisha kuwa baadhi ya wakulima bado wanakabiliwa na changamoto za kifedha kutokana na kutotenga bajeti ya kutosha ya maandalizi ya msimu mpya mara baada ya mavuno, jambo linalowafanya kushindwa kumudu baadhi ya gharama za uzalishaji licha ya uwepo wa pembejeo zinazotolewa kwa ruzuku.

Kwa mujibu wa maafisa hao, hali hiyo imekuwa ikiwakwamisha baadhi ya wakulima kuanza mapema shughuli za kilimo na kuwekeza kwa kiwango kinachohitajika ili kuongeza uzalishaji na ubora wa zao la korosho.

06/06/2026

Wataalamu kutoka Bodi ya Korosho Tanzania, Mamlaka ya Afya ya Mimea na Viuatilifu Tanzania na Taasisi ya Utafiti wa Kilimo Tanzania wametoa mafunzo kwa maafisa ugani na wapuliziaji wa mikorosho wilayani Tandahimba kuhusu matumizi sahihi na salama ya viuatilifu kuelekea msimu wa korosho wa 2026/27.

Jumla ya wapuliziaji 128 pamoja na maafisa ugani kutoka Bodi ya Korosho, TANECU na halmashauri walishiriki mafunzo hayo yaliyolenga kuongeza uelewa na kuboresha uzalishaji wa korosho.

Mtaalamu wa TPHPA, James Simon amesema mafunzo hayo yataongeza ufanisi katika matumizi ya viuatilifu na kuchangia ongezeko la uzalishaji. Naye Afisa Kilimo wa Bodi ya Korosho Tanzania, Shinje Ngalula amesema Serikali inaendelea kusambaza pembejeo kwa lengo la kuongeza uzalishaji wa korosho.

Washiriki wa mafunzo hayo wameahidi kutumia maarifa waliyopata kuwahudumia wakulima kwa ufanisi zaidi ili kuongeza tija katika zao la korosho.

06/06/2026

Maafisa Ugani wa Wilaya ya Mkuranga mkoani Pwani wamepatiwa mafunzo na TARI na Bodi ya Korosho Tanzania kwa lengo la kuwajengea uwezo kuhusu mbinu za kisasa za kudhibiti wadudu na magonjwa ya korosho.

Akizungumza kwa niaba ya Bodi hiyo, Kaisi Jamaldini amesema mafunzo hayo yanalenga kuwawezesha maafisa ugani kuwapa wakulima ushauri sahihi kuhusu matumizi ya viuatilifu na utunzaji wa mikorosho ili kuongeza uzalishaji na ubora wa zao hilo.

Washiriki wa mafunzo hayo wamesema yamewaongezea maarifa yatakayowasaidia kuwahudumia wakulima kwa ufanisi zaidi na kuchangia kufikiwa kwa lengo la taifa la kuongeza uzalishaji wa korosho.

06/06/2026

Mahak**a ya Hakimu Mkazi Mkoa wa Lindi imewahukumu watu wawili vifungo vya muda mrefu gerezani katika kesi mbili tofauti, baada ya kutiwa hatiani kwa makosa ya ubakaji wa mtoto na kupatikana na nyara za serikali kinyume cha sheria.

Katika kesi namba 17366 ya mwaka 2024, mtuhumiwa Hamis Rashid Mkon'gonda (55), mkazi wa Matopeni mkoani Lindi, amehukumiwa kifungo cha maisha gerezani pamoja na kulipa fidia ya shilingi milioni moja baada ya kutiwa hatiani kwa kosa la kumbaka mtoto mwenye umri wa miaka minne.

Akisoma hukumu hiyo, Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mahak**a ya Hakimu Mkazi Lindi, Consolata Singano, alisema mahak**a ilijiridhisha pasipo shaka yoyote kuwa upande wa Jamhuri uliuthibitisha ushahidi dhidi ya mshtakiwa.

Alisema upande wa mashtaka, uliokuwa ukiongozwa na Mwendesha Mashtaka wa Serikali Mofati Seth, uliwasilisha mashahidi saba pamoja na vielelezo vitatu vilivyoisaidia mahak**a kufikia uamuzi huo.

Katika kesi nyingine namba 12451 ya mwaka 2026, mtuhumiwa Michael Atanas Antoni amehukumiwa kifungo cha miaka 20 gerezani baada ya kupatikana na hatia ya kumiliki nyara za serikali kinyume cha sheria.

Mahak**a ilibaini kuwa mtuhumiwa alipatikana na vipande vitatu vya nyama ya mnyama aina ya ngiri bila kuwa na kibali halali kutoka mamlaka husika.

Hukumu hiyo ilitolewa na Hakimu Mkazi Khalfan Omari Khalfan, huku upande wa Jamhuri ukiwakilishwa na Mwendesha Mashtaka wa Serikali Jordan Kyambo.

Mahak**a imesema adhabu zilizotolewa zinakusudia kutenda haki na kutoa funzo kwa watu wanaojihusisha na vitendo vya uhalifu vinavyokiuka sheria za nchi.

RATIBA  YA MINADA YA UFUTA KWA CHAMA KIKUU CHA USHIRIKA TANECU
05/06/2026

RATIBA YA MINADA YA UFUTA KWA CHAMA KIKUU CHA USHIRIKA TANECU

Mkuu wa Mkoa wa Mtwara, Kanali Donald Msengi, amewataka wananchi kuongeza juhudi katika uhifadhi wa mazingira kwa kushir...
05/06/2026

Mkuu wa Mkoa wa Mtwara, Kanali Donald Msengi, amewataka wananchi kuongeza juhudi katika uhifadhi wa mazingira kwa kushiriki kikamilifu shughuli mbalimbali za usafi wa mazingira, ikiwemo ujenzi na matumizi ya vyoo bora, upandaji na utunzaji wa miti, ili kuhakikisha mazingira yanakuwa safi, salama na yenye afya kwa jamii.

Kanali Msengi ametoa rai hiyo leo Juni 5, 2026, wakati wa maadhimisho ya Siku ya Mazingira Duniani, akisisitiza kuwa utunzaji wa mazingira ni wajibu wa kila mwananchi na msingi muhimu wa maendeleo endelevu ya jamii na taifa kwa ujumla.

Amesema mazingira safi huchangia kuzuia magonjwa ya mlipuko, kulinda vyanzo vya maji, kuhifadhi bioanuwai na kupunguza athari za mabadiliko ya tabianchi ambazo zimeendelea kuathiri sekta mbalimbali za kiuchumi, ikiwemo kilimo, uvuvi na mifugo.

Aidha, amewahimiza wananchi kuepuka vitendo vinavyoharibu mazingira k**a vile ukataji holela wa miti, uchomaji moto ovyo, utupaji wa taka katika maeneo yasiyoruhusiwa na matumizi yasiyo sahihi ya rasilimali za asili. Amesisitiza kuwa ushirikiano kati ya serikali, taasisi mbalimbali na wananchi ni muhimu katika kuhakikisha mazingira yanahifadhiwa kwa manufaa ya kizazi cha sasa na vijavyo.

Maadhimisho ya mwaka huu yamekuwa fursa ya kuhamasisha jamii kuchukua hatua za vitendo katika kulinda mazingira na kuendeleza kampeni za usafi na upandaji miti katika maeneo mbalimbali ya Mkoa wa Mtwara.

Mkuu wa Mkoa wa Mtwara, Kanali Donald Msengi, ameiagiza kampuni ya Zhong Wang kuharakisha malipo ya fidia kwa wananchi w...
04/06/2026

Mkuu wa Mkoa wa Mtwara, Kanali Donald Msengi, ameiagiza kampuni ya Zhong Wang kuharakisha malipo ya fidia kwa wananchi wa Wilaya ya Masasi waliopisha maeneo yao kwa ajili ya shughuli za uwekezaji wa uchimbaji wa madini.

Kanali Msengi ametoa agizo hilo Juni 3, 2026 alipofanya ziara katika kampuni hiyo inayojihusisha na uchimbaji wa madini ya dhahabu wilayani humo.


04/06/2026

Serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Rais Samia Suluhu Hassan imeendelea kuimarisha sekta ya uvuvi kupitia utekelezaji wa miradi ya maendeleo, ikiwemo ujenzi wa Bandari ya Uvuvi ya Kilwa Masoko mkoani Lindi unaogharimu Sh280 bilioni.

Akizungumza katika kikao cha wadau wa uvuvi Wilaya ya Kilwa, Mkuu wa Mkoa wa Lindi, Zainab Telack, amesema serikali imeendelea kuweka mazingira wezeshi kwa ukuaji wa sekta za uvuvi na mifugo ili kuongeza tija na mchango wake katika uchumi.

Telack amewataka wadau wa uvuvi kulinda rasilimali za bahari ili kuhakikisha uwekezaji huo mkubwa unaleta manufaa endelevu kwa wananchi.

Naye Katibu Tawala Msaidizi wa Mkoa wa Lindi anayeshughulikia Uchumi na Uzalishaji, Mwijuma Mkungu, amesema uwekezaji wa serikali umechangia kuongezeka kwa uzalishaji wa samaki na kipato cha wananchi.

Baadhi ya wavuvi wameiomba serikali kuimarisha doria katika maeneo ya uvuvi ili kudhibiti uvuvi haramu na kulinda rasilimali za bahari.

*PICHA:* Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan katika Matukio tofauti ya Picha alipopoke...
03/06/2026

*PICHA:* Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan katika Matukio tofauti ya Picha alipopokelewa na Mwenyeji wake Rais wa Shirikisho la Urusi Mhe. Vladimir Putin alipowasili Ikulu ya Jijini Moscow Leo Juni 03,2026.


Address

1050, Mtwara
Mikindani

Telephone

+255682907172

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Kusini Yetu Online Tv posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Kusini Yetu Online Tv:

Share