08/07/2024
Nawasisitiza wafanyabiashara wote nchini kusajili majina ya biashara au majina ya kampuni kabla ya kuanza Biashara ili kuepuka jina la biashara husika kuchukuliwa na hatimaye kulazimika kubadilisha taarifa upya.
Urasimishaji wa biashara unawawezesha wananchi kushiriki kikamilifu katika ujenzi na ukuaji wa uchumi wa nchi yao na kuwa walipa kodi wazuri na washiriki wenza wa Serikali katika kutoa huduma kwa jamii, hivyo ni vema wafanyabiashara wakajitokeza kusajili biashara zao.
Tawahamasisha watu wasifanye biashara kibubu, unaposajili biashara yako inatambulika kisheria hivyo kuifanya biashara yako haiwezi kuchukuliwa na mtu yeyote.
Mfanyabiashara unaposajili jina la biashara, kampuni na alama za biashara k**a mfanyabiashara unakuwa na alama ambayo inawakilisha biashara yako, hivyo inakuwa rahisi kwa mteja kuitambua.
Watu wengi wanafanya makosa wakati wa uanzishwaji wa biashara, mathalani kuanzisha na kutangaza biashara ambayo haijasajiliwa ni kinyume na taratibu kwa sababu kwa kufanya hivyo unaweza kuwa unavunja sheria kwa kutumia jina la mtu mwingine bila kujua au mtu mwingine anaweza kulisajili jina hilo na kulifanya lake kisheria.
Pia tunakufanyia taratibu zote za usajili wa kampuni kuanzia uandaaji wa nyaraka mpaka kukamilika kwa Usajili wa Kampuni, kukamilisha maswala yote ya TRA pamoja na leseni mbalimbali za biashara.
Hatuishii tu kukufanyia usajili wa jina au kampuni yako, bali bali pia tunakupatia ushauri juu ya uendeshaji wa biashara na makampuni kabla na baada ya usajili na urasimishaji. Tutakuwa nawe katika mchakato mzima wa kuendesha biashara yako mpaka itakapokuwa imara na wewe kupata uzoefu wa kutosha katika biashara yako.
Tuna washauri na watalamu wa uchumi, biashara na uwekezaji wenye ujuzi wa kufanya upembuzi yakinifu na makini katika masuala ya uwekezaji, biashara na ujasiriamali nchini Tanzania.
☎️ +255 717 820 820