Wananchi TV

Wananchi TV Karibu katika ukurasa wetu kupata habari za matukio ya ๐ค๐ข๐ญ๐š๐ข๐Ÿ๐š ๐ง๐š ๐ค๐ข๐ฆ๐š๐ญ๐š๐ข๐Ÿ๐š ๐ค๐ฎ๐ก๐ฎ๐ฌ๐ฎ ๐’๐ข๐š๐ฌ๐š | ๐๐ฎ๐ซ๐ฎ๐๐š๐ง๐ข | ๐Œ๐ข๐œ๐ก๐ž๐ณ๐จ na vipindi maalum.

Wizara ya mambo ya ndani Nchini Tanzania kwa mwaka 2026/27, imeliomba Bunge la Tanzania kuidhinisha bajeti ya Jumla ya s...
25/05/2026

Wizara ya mambo ya ndani Nchini Tanzania kwa mwaka 2026/27, imeliomba Bunge la Tanzania kuidhinisha bajeti ya Jumla ya shilingi trilioni mbili, Bilioni mia nne arobaini na tatu, Milioni mia mbili kumi na tano, laki tisa na ishirini na saba elfu (2,443,215,927,000) kwaajili ya matumizi ya Wizara hiyo.

Akiwasilisha makadirio ya mapato na matumizi ya Wizara hiyo, Waziri wa Mambo ya ndani Mhe. Patrobas Katambi, leo Mei 25, 2026, ameliambia Bunge la Tanzania kuwa Wizara yake pia imepanga kukusanya jumla ya shilingi Bilioni mia nne tisini na tisa na milioni tisini (499,090,000,000) kutoka kwenye vyanzo mbalimbali, akisema Wizara hiyo itaendelea kuimarisha matumizi ya mifumo ya kielektroniki na ununuzi wa vitendea kazi vya kisasa ili kuweza kufikia lengo walilojiwekea.

Kulingana na ufafanuzi wa Waziri Katambi, shilingi trilionj moja, bilioni mia tisa hamsini na tatu, milioni mia tatu sitini na sita, laki nne na themanini na sita elfu (1,953,366,486,000) sawa na asilimia 80 ya bajeti yote ya wizara ni kwaajili ya matumizi ya kawaida.

Aidha Shilingi Bilioni mia nne themanini na tisa, Milioni mia nane arobaini na tisa, laki nne na arobaini na moja elfu (489,849,441,000) sawa na asilimia 20 ni kwaajili ya miradi ya maendeleo.

Serikali kupitia Wakala wa Nishati Vijijni (REA), unaendelea kutekeleza miradi mbalimbali pamoja na kuwasimamia kwa kari...
25/05/2026

Serikali kupitia Wakala wa Nishati Vijijni (REA), unaendelea kutekeleza miradi mbalimbali pamoja na kuwasimamia kwa karibu wakandarasi wote waliopewa na watakaopewa zabuni ya kutekeleza miradi ili kuhakikisha kuwa miradi hiyo inakamilika kwa wakati na kwa ubora uliopangwa ili iweze kuwanufaisha wananchi.

Hayo yamebainishwa leo Mei 25, 2026 na Wajumbe wa Bodi ya Nishati Vijijini (REB), wakati wa hafla ya kukagua miradi, kutembelea na kuwasha umeme kitongoji cha Nkanda kilichopo wilaya ya Ludewa mkoani Njombe mradi uliokuwa unatekelezwa na Suma Jkt Electric Company Ltd.

Mha. Ahmed Chinemba amesema kuwa, mradi wa kupeleka umeme katika vitongoji vya mwambao wilayani Ludewa unatekelezwa na mkandarasi M/S SUMAJKT ELECTRIC COMPANY LTD kwa gharama ya zaidi ya shilingi bilioni 3.2 ili wananchi wa mwambao wapate huduma ya umeme.

โ€œMradi huu umelenga kuongeza shughuli za kiuchumi kwa wananchi wa kitongoji cha nkanda ukiwa na chachu ya kutoa fursa za kibiashara kwa kuongeza thamani ya mazao ya uvuvi, kurahisiha upatikanaji wa huduma za kijamii na uwekezaji wa viwanda vidogo vidogo k**a mashine za kusaga, mashine za kuchana mbao pamoja na mashine za kuchomelea,โ€ Amesema Mha. Chinemba.

Kwa upande wake, Naibu Mkurugenzi Mtendaji wa Suma JKT Brigedia Jenerali Shija Lupi, ameishukuru REA kwa kuwapatia kazi hiyo ya kufikisha umeme katika maeneo ya mwambao kikiwemo kitongoji hicho cha Nkanda ambapo kazi imekamilika kwa ubora.

Akizungumza kwa niaba ya Mkurugenzi Mkuu, Mha. Deogratius Nagu amesema katika kitongoji cha Nkanda takribani shilingi milioni 450 zimetolewa na Serikali kupitia REA ili kufikisha huduma ya umeme katika kitongoji hicho.

Aidha, amewataka wananchi wa Nkanda kuchangamkia fursa ya uwepo wa umeme kwa kuhakikisha wanafanya wiring katika nyumba zao na kuunganisha umeme kwa wingi ili wanufaike na umeme huo katika kitongoji chao.

25/05/2026
25/05/2026

Jeshi la Polisi kupitia Mkuu wa Kikosi cha Usalama Barabarani (RTO) Mkoa wa Arusha, Kamishna Msaidizi wa Polisi (ACP) Zauda Mohamed, limeingilia kati kunusuru hali hiyo.
ACP Zauda ametoa wito kwa wamiliki na madereva wote wa vyombo hivyo vya moto mkoani humo kusitisha mgomo huo na badala yake watumie njia ya mazungumzo.

Kufuatia shinikizo hilo, Pia uongozi wa LATRA mkoani Arusha umeonyesha utayari wa kusikiliza kero hizo na kuzitafutia ufumbuzi.

25/05/2026

Chanzo cha Mgomo Madereva na wamiliki wa daladala wamefunguka kero zao na wakishinikiza kupatiwa ufumbuzi wa kero yao ya kutozwa faini na Mamlaka ya Udhibiti Usafiri wa Ardhini (LATRA) bila kupewa taarifa rasmi.

Usafiri wa umma jijini Arusha umesimama mapema leo kufuatia mgomo mkubwa uliofanywa na wamiliki pamoja na madereva wa daladala, hatua iliyoleta adha kubwa kwa wananchi na wanafunzi waliokuwa wakiwahi kwenye majukumu yao.

25/05/2026

Waziri wa Mambo ya ndani Nchini Tanzania Mhe. Patrobas Katambi, ameliambia Bunge la Tanzania kuwa katika kipindi cha Julai 2025 hadi Aprili 2026, makosa makubwa ya jinai 39,027 yalitolewa taarifa katika Vituo mbalimbali vya Polisi ikilinganishwa na makosa 40,022 yaliyotolewa taarifa katika kipindi k**a hicho kwa mwaka 2024/25.

"Kupungua kwa makosa hayo kumetokana na kuongezeka kwa uelewa na ushirikiano wa Jamji katika kubaini na kuzuia uhalifu." Amesema Waziri Katambi wakati akiwasilisha makadirio ya mapato na matumizi ya Wizara ya mambo ya ndani kwa mwaka 2026/27 leo Mei 25, 2026 Bungeni, Dodoma.

Kuelekea mwaka 2026/27, Waziri Katambi amesema Wizara yake kupitia Jeshi la Polisi litaendelea kudhibiti uhalifu Nchini, ikiwemo matumizi mabaya ya mitandao ya kijamii na udukuzi wa taarifa za kimtandao kwa kukamilisha uanzishwaji wa Ofisi za Kanda za upelelezi wa makosa ya uhalifu wa Kimtandao katika Jiji la Dodoma na Zanzibar.

Ameeleza pia kuhuys mpango wa kuimarisha kikosi Maalumu cha kudhibiti taarifa potofu na uchochezi mtandaoni pamoja na kutoa elimu kwa umma kuhusu athari za kusambaza taarifa za uongo.

Klabu ya Mamelodi Sundowns ya Afrika Kusini imetwaa ubingwa wa Klabu Bingwa Afrika CAFCL baada ya kuifunga AS FAR Rabat ...
24/05/2026

Klabu ya Mamelodi Sundowns ya Afrika Kusini imetwaa ubingwa wa Klabu Bingwa Afrika CAFCL baada ya kuifunga AS FAR Rabat kwa jumla ya mabao 2-1.

Katika mchezo wa Fainali ya pili uliopigwa Morocco timu hizo zimemaliza kwa sare ya bao 1-1.

Vilabu vya Tanzania vinakwama wapi kupata mafanikio k**a haya?

Nahodha wa Manchester United, Bruno Fernandes ameandika historia mpya ndani ya Ligi Kuu ya Uingereza baada ya kuvunja re...
24/05/2026

Nahodha wa Manchester United, Bruno Fernandes ameandika historia mpya ndani ya Ligi Kuu ya Uingereza baada ya kuvunja rekodi iliyokuwa ikishikiliwa Kevin De Bruyne na Thierry Henry,.

Rekodi hiyo ni kutoa pasi nyingi zaidi za mabao katika msimu mmoja wa Ligi hiyo, kiungo huyo wa Ureno amefikisha jumla ya pasi za mabao 21 msimu huu wa 2025/26 idadi ambayo haijawahi
kufikiwa katika historia ya EPL.

Mchezo umekwisha Simba anaondoka na aama tatu KMC Complex
24/05/2026

Mchezo umekwisha Simba anaondoka na aama tatu KMC Complex

Kipindi cha kwanza kinamalizika katika Dimba la KMC Simba dhidi ya Dodoma Jiji hakuna mbabe.Kipindi cha pili mnyama afan...
24/05/2026

Kipindi cha kwanza kinamalizika katika Dimba la KMC Simba dhidi ya Dodoma Jiji hakuna mbabe.

Kipindi cha pili mnyama afanye nini ili kupata goli? Au unaishauri nini Dodoma Jiji ili wapate ushindi?

Wanachama wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) waliojitokeza katika Uwanja wa Mtekelezo, Dodoma katika Uzinduz...
24/05/2026

Wanachama wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) waliojitokeza katika Uwanja wa Mtekelezo, Dodoma katika Uzinduzi wa Operesheni ya Katiba Mpya Free Lissu.

Address

Sinza
16102

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Wananchi TV posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Wananchi TV:

Share