Wananchi TV

Wananchi TV Karibu katika ukurasa wetu kupata habari za matukio ya ๐ค๐ข๐ญ๐š๐ข๐Ÿ๐š ๐ง๐š ๐ค๐ข๐ฆ๐š๐ญ๐š๐ข๐Ÿ๐š ๐ค๐ฎ๐ก๐ฎ๐ฌ๐ฎ ๐’๐ข๐š๐ฌ๐š | ๐๐ฎ๐ซ๐ฎ๐๐š๐ง๐ข | ๐Œ๐ข๐œ๐ก๐ž๐ณ๐จ na vipindi maalum.

26/08/2026

Hospitali ya Taifa Muhimbili- Mloganzila imeanza rasmi kambi maalum ya upasuajฤฑ wa nyonga, magoti na mabega inayofanyika mpaka Agosti 29, 2026 kwa kutumia teknolojia ya kisasa ya upasuaji wa matundu madogo.

Zaidi huyu hapa Daktari Bingwa wa mifupa ambaye pia ni mbobezi wa matatizo ya Noynga na Magoti, Dokta Rabi Ndeserua akielezea namna kambi hiyo itakavyokuwa ikitoa huduma.

Miili ya askari wawili wa Jeshi la Polisi Wilaya ya Kibaha Mkoa wa Pwani waliofariki Agosti 25, 2026 baada ya kugongwa n...
26/08/2026

Miili ya askari wawili wa Jeshi la Polisi Wilaya ya Kibaha Mkoa wa Pwani waliofariki Agosti 25, 2026 baada ya kugongwa na gari eneo la kivuko cha watembea kwa miguu (zebra) eneo la Maili Moja imeagwa leo na kusafirishwa kwenda Mikoani kwao kwa mazishi.

Tukio la kuaga miili ya askari hao wa Jeshi la Polisi Kostebo Izdory George Michael na askari wa k**e Rehema Juma Magawa limefanyika katika hospitali ya Rufaa ya Mkoa huo ya Tumbi, tukio limeongozwa na Kamanda wa Polisi Mkoa wa Pwani Kamishna Msaidizi wa Polisi Salim Morcase, ambapo askari wa vyeo mbalimbali na waombolezaji wengine wameshiriki katika kuaga.

Mwili wa Marehemu Rehema umesafirishwa kwenda Korogwe Mkoani Tanga kwa mazishi na Mwili wa Izdory umepelekwa Mkoa wa Rukwa Wilaya ya Sumbawanga
Vijijini kwa mazishi.

26/08/2026

Slow Juicer Blender โ€“ Ofa ya Tsh 150,000 tu (Delivery Bure)

PATA JUICE HALISI NA FRESH 100% BILA KUONGEZA MAJI! ๐Ÿ๐ŸŠ๐Ÿฅ•
Jipatie Slow Juicer Blender ya kisasa kabisa itakayokurahisishia maisha jikoni:
1. Uwezo Mkubwa: Watts 500.
2. Ujazo wa Kutosha: 1000ml.
3. Cold Press / Slow Squeez.
4. Rahisi Kusafisha na Kutumia.

BEI YA OFA: Tsh 150,000/= Tu!
DELIVERY BURE POPOTE ULIPO

๐Ÿ“ Duka Letu: Kariakoo, Mtaa wa Magila, Dar es Salaam.

Bofya hapa chini kuagiza sasa kabla ofa haijaisha. KARIBU

26/08/2026

Msanii Dogo Paten akitoa Burudani katika Tamsha la Kitaifa la Utamaduni linalofanyika katika Uwanja wa Jamhuri Mkoani Morogoro leo.

Umekoshwa na nini hapa kwa Paten?

Askari wa Jeshi la Polisi, wawili wamefariki dunia baada ya gari kuwagonga watembea kwa miguu katika eneo la Maili Moja,...
26/08/2026

Askari wa Jeshi la Polisi, wawili wamefariki dunia baada ya gari kuwagonga watembea kwa miguu katika eneo la Maili Moja, Wilaya ya Kibaha, Mkoa wa Pwani.

Kwa mujibu wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Pwani, ajali hiyo ilitokea Agosti 25, 2026, majira ya saa 1:40 usiku katika barabara kuu ya Dar es Salaamโ€“Morogoro, eneo la kivuko cha waenda kwa miguu.

Taarifa ya Polisi iliyotolewa leo, Agosti 26, 2026, imeeleza kuwa gari aina ya Toyota Noah, lenye namba za usajili T.804 ERM, lilikuwa likitokea Dar es Salaam kuelekea Mlandizi likiendeshwa na Josia Isaya Arute, mwenye umri wa miaka 34, mkazi wa Mlandizi.

Inadaiwa kuwa gari hilo lilipofika katika eneo la zebra, dereva alilipita kundi la magari yaliyokuwa yamesimama ili kutoa nafasi kwa watembea kwa miguu kuvuka barabara, kisha kuwagonga.

Katika ajali hiyo, askari wa Polisi, Izdory George Michael, alifariki dunia, huku askari mwenzake, Rehema Juma Magawa, akijeruhiwa kichwani na kukimbizwa katika Hospitali ya Tumbi kwa ajili ya matibabu.

Hata hivyo, Rehema Juma Magawa alifariki dunia asubuhi ya Agosti 26, 2026, wakati akiendelea na matibabu.

Jeshi la Polisi limesema miili ya marehemu imehifadhiwa katika Hospitali ya Rufaa ya Tumbi, ikisubiri taratibu za kusafirishwa kwenda makwao kwa ajili ya mazishi.

Baada ya ajali hiyo, dereva wa gari hilo alikimbia eneo la tukio. Polisi kwa kushirikiana na wananchi waliendesha msako na baadaye kulikamata gari hilo katika eneo la Kwa Mfipa, Wilaya ya Kibaha, majira ya saa 8:40 usiku, likiwa limefichwa.

Gari hilo limepelekwa katika Kituo cha Polisi Kibaha kwa ajili ya hatua zaidi za kisheria.

Jeshi la Polisi Mkoa wa Pwani limewataka madereva kuzingatia sheria za usalama barabarani pamoja na alama za barabarani, likisisitiza kuwa hatua hizo ni muhimu katika kuzuia ajali zinazoweza kuepukika.

26/08/2026

Burudani ya Ngoma za Asili iliendelea katika Tamasha la Kitaifa la Utamaduni linaloendelea Mkoani Morogoro leo Agosti 26,2026.

26/08/2026

Maneno ya Mwenyekiti wa CHADEMA Tundu Lissu akimpa maelekezo Makamu Mwenyekiti wa Chama hicho John Heche Mahakamani leo.

26/08/2026

Naibu Katibu Mkuu Chadema Zanzibar, Ali Ibrahim akisoma dua muda mchache kabla ya kuanza kwa kesi ya Lissu leo.

Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Tundu Lissu anayekabiliwa na kesi ya uhaini, anatarajiwa kuhitimisha sehemu ya kwanza ya ushahidi wa utetezi wake, yaani ushahidi mkuu, ikiwa ni siku ya tatu katika mfululizo wa utetezi wake.

Leo Jumatano, Agosti 26, 2026, Lissu anatarajiwa kuhitimisha kwa kuangazia ushahidi wa upande wa mashtaka, kwa kuuchambua anachokiita udhaifu wake kuishawishi mahakama kuwa haukuweza kuthibitisha shtaka linalomkabili kwa kiwango kinachotakiwa kisheria, yaani bila kuacha mashaka yoyote.

25/08/2026
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan ameridhia ombi la Makamu wa Rais Balozi Dkt. Emmanuel N...
25/08/2026

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan ameridhia ombi la Makamu wa Rais Balozi Dkt. Emmanuel Nchimbi kujiuzulu nafasi ya Makamu wa Rais wa Tanzania, kupitia barua rasmi iliyosainiwa na Katibu Mkuu Kiongozi Balozi Dkt. Moses Kusiluka imebainisha ombi hilo.

"Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. samia Suluhu Hassan leo tarehe 25 Agosti, 2026, amepokea barua ya ombi la kujiuzulu Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Balozi Dkt. Emmanuel John Nchimbi kuanzia tarehe 04 Septemba, 2026. Mheshimiwa Rais ameridhia ombi hilo.

Taratibu za kikatiba za kumpata Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania mwingine zitachukuliwa".

Address

Sinza
16102

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Wananchi TV posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Wananchi TV:

Shortcuts

Share