12/06/2026
FIFA WORLD CUP 2026 REFA WA SOMALIA AKATALIWA KUINGIA MAREKANI
Dunia ya mpira inatikiswa na tukio jipya kabla ya ufunguzi wa Kombe la Dunia 2026. Refa maarufu wa Somalia, Omar Artan aliyetajwa Refa Bora wa Afrika 2025 na CAF alikataliwa kuingia Marekani huko Miami International Airport, alipowasili akitokea Istanbul.
Aliambiwa "asikubalike" kwa madai ya "vetting concerns," kisha akarudishwa Mogadishu.
Sababu kubwa nyuma ya hili ni kwamba Somalia ni miongoni mwa nchi zilizopo kwenye orodha ya "travel ban" iliyowekwa na utawala wa Rais Trump sera inayozuia raia wa baadhi ya nchi za Kiafrika na Kiislamu kuingia Marekani, hata k**a wana kazi rasmi ya kimataifa k**a hii ya FIFA.
Waziri wa Usalama wa Ndani wa Marekani, Markwayne Mullin, alitetea uamuzi huo akidai kuna "uhusiano" fulani unaomfanya Artan asikubalike, bila kutoa maelezo zaidi: "Sitaeleza kwa nini mtu huyu alikataliwa, lakini kuna sababu."
Tukio hili limemfanya Rais wa zamani wa FIFA, Joseph Blatter, kulipuka kwa hasira. Kwa mujibu wake, kuna kanuni mbili za msingi ambazo nchi yoyote inayopewa heshima ya kuandaa Kombe la Dunia haiwezi kuzikiuka: usalama na kuhakikisha viza kwa maafisa wote wa FIFA.
"Hakuna mtu rasmi zaidi ya refa," alisema Blatter, akiongeza kuwa kumkatalia refa kuingia ni tatizo kubwa zaidi ya tukio la mtu mmoja ni kukataa mamlaka ya mchezo wenyewe.
Cha kushangaza, FIFA kupitia Rais wake Gianni Infantino ilisema tu kuwa hali hiyo ni "unfortunate" (ya kusikitisha), bila hatua zozote madhubuti. Wakati huo huo, UEFA imemheshimu Artan kwa kumteua kuongoza Fainali ya UEFA Super Cup kati ya PSG na Aston Villa ikionyesha wazi kwamba ubora wake unatambulika kila mahali, isipokuwa Marekani.
Swali kubwa linabaki: Je, nchi inayoshindwa kuruhusu refa rasmi wa FIFA kuingia kwa sababu ya sera za uhamiaji badala ya sababu za kimpira inastahili kabisa heshima ya kuandaa Kombe la Dunia? Na je, mfumo huu wa "vetting" hauonyeshi ubaguzi wa kisiasa ukijificha nyuma ya mpira wa miguu?
Wewe unaonaje hili ni suala la usalama tu, au ni dalili ya jambo kubwa zaidi linaloathiri uhuru na haki katika mpira wa dunia? 👇