02/09/2026
Kijana mtanashati wa Marekani mwenye umri wa miaka 21, Otto Warmbier, mwanafunzi wa Chuo Kikuu cha Virginia, alikuwa kwenye foleni ya kukaguliwa pasipoti ili kupanda ndege kurudi kwao. Safari yake ya siku tano ya utalii nchini Korea Kaskazini ilikuwa imemalizika, na alikuwa na furaha ya kurudi nyumbani kujiandaa na muhula mpya wa masomo.
Ghafla, mikono miwili yenye nguvu ilimshika bega kwa nyuma.
Maafisa wawili wa usalama wa Korea Kaskazini waliokuwa wamevaa sare za kijani kibichi na kofia kubwa walisimama pembeni yake kushoto na kulia. Bila kusema neno lolote, walimvuta pembeni. Marafiki zake waliokuwa naye kwenye foleni walishtuka huku Otto anawaangalia kwa hofu na kusema kwa sauti ya chini: "Nadhani nina shida kidogo... nitawapigia simu."
Haikuwa shida ndogo. Hiyo ndiyo ilikuwa mara ya mwisho kwa dunia kumsikia Otto Warmbier akiongea akiwa na akili timamu.
Siku mbili kabla ya kuk**atwa kwake, usiku wa Mwaka Mpya, Otto na kundi lake la watalii walilala kwenye Hoteli ya Yanggakdo jengo refu la ghorofa 47 lililopo kwenye kisiwa katikati ya Mto Taedong jijini Pyongyang.
Hoteli hiyo ilikuwa na ghorofa ya tano ya siri, eneo ambalo halikuwa na batani kwenye lift (elevator) na lilijaa mabango ya propaganda ya serikali. Usiku huo, Otto alijipenyeza kwenye ghorofa hiyo yenye giza na kutoa bango moja la propaganda lililokuwa limeandikwa: "Tujihami vikali kwa imani ya Kim Jong-il!"
Serikali ya Korea Kaskazini iliona kitendo hicho si tu k**a wizi, bali k**a uhalifu mkubwa wa kumpinga Kiongozi Mkuu na Dola.
Wiki sita baadae, mbele ya kamera za vyombo vya habari vya kimataifa jijini Pyongyang, Otto alionyeshwa kwenye runinga. Alikuwa anatetemeka mwili mzima, anatokwa na machozi ya hofu, huku anasoma maelezo aliyolazimishwa na serikali:
"Nilifanya kosa kubwa zaidi maishani mwangu... Nataka kurudi nyumbani kwenye familia yangu! Tafadhali niokoeni!"
Mnamo Machi 16, 2016, Mahak**a Kuu ya Korea Kaskazini ilimuhukumu Otto Warmbier miaka 15 ya kazi ngumu gerezani (hard labor). Hukumu hiyo ilichukua dakika 5 tu kusomwa.
Baada ya hukumu hiyo, Otto alipotea kabisa. Hakuna mwanadiplomasia, daktari, wala Mmarekani yeyote aliyeruhusiwa kumuona au kuongea nae kwa zaidi ya mwaka mmoja.
Ndani ya wiki chache tu baada ya hukumu hiyo, kitu fulani cha kutisha kilitokea akiwa mikononi mwa vyombo vya usalama vya Korea Kaskazini.
Ingawa serikali ya Korea Kaskazini ilidai kuwa Otto alipata ugonjwa wa (botulism) na kisha kupewa kidonge cha kulala kilichomfanya azimie, madaktari wa Marekani na uchungu*i wa kitabibu baadae ulipinga vikali maelezo hayo.
Ukweli ni kwamba, Otto alipatwa na kiharusi kikubwa cha ubongo (Anoxic Brain Damage) kilichosababishwa na ukosefu wa hewa ya oksijeni kwenye ubongo kwa muda mrefu. Hali hii hutokea pale mtu anaponyongwa, kukabwa koo, kuteswa kwa kutumbukizwa kichwa kwenye maji (waterboarding), au kupigwa vibaya sana kichwani na kusababisha mfumo wa moyo na upumuaji kusimama.
Mwili na umri wake mdogo haukuweza kuvumilia ukatili wa magereza ya Korea Kaskazini. Ubongo wake ulipoteza seli zote muhimu, na akakaa kwenye koma ya kudumu.
Mwezi Juni 2017, baada ya shinikizo kubwa la kidiplomasia kutoka kwa serikali ya Marekani chini ya Rais Donald Trump, Korea Kaskazini hatimae ilikubali kumwachia Otto kwa "sababu za kiutu."
Usiku wa tarehe 13 Juni 2017, ndege ya jeshi ya Marekani ilitua kwenye uwanja wa ndege wa Cincinnati, Ohio. Wazazi wa Otto, Fred na Cindy Warmbier, walikuwa wanasubiri kwa hamu na matumaini kumkumbatia mtoto wao.
Milango ya ndege ilipofunguka, hali iliyojitokeza ilikuwa ya kusikitisha mno: Otto hakutoka anatembea. Alitolewa yuko kwenye kitanda cha wagonjwa akiwa amefungwa mipira ya kumsaidia kupumua. Macho yake yalikuwa wazi lakini hayakuwa yanaona wala kutambua chochote, ameuma meno na kutoa sauti za maumivu zisizoeleweka. Alipoteza uwezo wa kuona, kusikia, au kusogea, ubongo wake ulikuwa umekufa kabisa (vegetative state).
"Kijana wetu alirudishwa kwetu akiwa amepooza kabisa, asiyeweza kuongea wala kumtambua mtu yeyote. Korea Kaskazini haikumpiga tu kikatili, bali ilimwangamiza kabisa," alieleza baba yake, Fred Warmbier.
Siku sita tu baada ya kurejeshwa nyumbani Marekani, mnamo tarehe 19 Juni 2017, Otto Warmbier alifariki dunia akiwa na umri wa miaka 22, akiwa amezungukwa na familia yake iliyokuwa inamlilia.
Kwa nini Otto Warmbier hakunusurika?
1. Mateso na Ukatili wa jeshi: Uchungu*i wa kitatibu ulionyesha kuwa ubongo wake ulipata uharibifu mkubwa kutokana na ukosefu wa hewa ya oksijeni, matokeo ya mateso makali ya kisaikolojia na kimwili mara tu baada ya hukumu yake.
2. Kunyimwa Matibabu: Mfumo wa Korea Kaskazini ulimficha kwa zaidi ya mwaka mmoja bila kumpa matibabu sahihi ya mfumo wa fahamu, ukisubiri hadi hali yake iwe haina matumaini ndipo umwachie ili asifie gerezani.
3. Kutumiwa K**a Shinikizo la Kisiasa: Korea Kaskazini ilimtumia Otto k**a "kete ya kisiasa" (political pawn) ili kuilazimisha Marekani kufanya mazungumzo, lakini ukatili waliomfanyia ulivuka mipaka ya kibadamu.
Kifo cha Otto Warmbier kilitikisa dunia na kuisukuma Marekani kupiga marufuku raia wake wote kusafiri kwenda Korea Kaskazini k**a watalii, marufuku inayodumu hadi leo..
.................................
Download app hii ili usipitwe na simulizi hizi za kusisimua maana zinapatikana huko zaidi... App hii iko playstore.. Bonyeza link https://dub.sh/Wx9mJtc