22/12/2024
Jinsi Ya Kuuza Chochote Kwa Kutumia STORY...
Hiki unachoenda kukisoma Ndani ya Sekunde 60 Zijazo kitakugeuza Kuwa:
.
“Selling Machine”
Kivipi?...
Ngoja nielezee Hapa Chini...
Unapouza Chochote Unatakiwa kuelewa Kwamba:
“Watu Huwa Hawanunui Vitu Bila Sababu”
NA:..Kitu Cha Kushangaza ni Kwamba:
Watu Huwa Hawanunui Vitu Vitu Kwa Kutumia AKILI Kabisa.....Huwa wananunua Vitu Kwa Kutumia MOYO
Ngoja nielezee vyema Hapa Chini...
Kwenye Akili Kuna Kitu Kinaitwa “LOGIC”...(Mantiki)
NA:
Kwenye Moyo Kuna Kitu Kinaitwa “HISIA”
Ndio Maana Wataalamu wa Mauzo Duniani Wana msemo wao unaosema Hivi...
“People Buy By EMOTIONS...and they Justify by LOGIC”
Maana yake ni Kwamba:
“Watu Hununua Vitu Kwa Kutumia Hisia Kisha wanahalalisha Maamuzi Yao Kwa Kutumia Mantiki”
Kwahiyo:
Ukitaka Kuuza Zaidi Tumia STORIES....
Usiwafanye Wateja Wafikiri na Kutumia AKILI pindi wanaponunua.....wafanye Wahisi!
Ndio Maana 99% ya Matangazo yanayofanya Vizuri Duniani Yana Kitu Kimoja Kinachoitwa:
“STORY”
NA:
Ujuzi Huo unaitwa:
“Storyselling”
Je Uandikaje Story Yako Pindi Unapotaka Kuuza Chochote Kwa Kutumia Story?
Hii Hapa Chini FORMULA...
Hata Siku Moja usiifanye Story Yako Itabirike Kwa Mteja Jinsi itakavyoisha..Ndio Maana hutakiwi Kuanza Story Yako na Maneno k**a:
-Nilizaliwa Katika Familia ya Kimasikini
Kwanini?
Kwasababu watajua Kabisa baadae Kwenye Story Utakuwa Tajiri
Badala yake:
Anza Story Yako Kwa:
“Drama & Curiosity”
Kwanini?
Ili Kuteka Attention ya Mteja wako asome Mpaka Mwisho
Story zinazofanya Vizuri Sokoni ni zile Zinazoanza Na:
“DRAMA & CURIOSITY”
Mfano:
-Sitasahau Siku niliyosimama Pale k**a Mjinga
-Sitosahau Siku Niliyofumamiwa na Mke wa Mtu
-Mme Wangu alinitishia Kunipa talaka na kuniacha na watoto Wawili...
-Alinipigia Simu 2:15am Huku analia...
-Baada ya Kugundua kuw a Naenda Kufa nilijiandaa kumuua Dakitari
Anza Story Yako na Kitu ambacho Kitateka Attention Ya Mteja wako Ili asome Mwaka Mwisho
Kitu Adimu Zaidi na chenye Thamani Kubwa Zaidi Mtandaoni ni:
.
“Attention ya Wateja wako”
Attention Ndio Iliyobeba Pesa Zako Kwenye Matangazo Yako
Voila!