Rabbi Tv Tanzania

Rabbi Tv Tanzania Karibu Katika Ukurasa Wa Rabbi Tv
kwa Habari,Michezo, na matukio
kila siku. Channel No 121 Startime

China yaufunga mji wakati visa vya Covid vikiongezeka kote ulimwenguniChina leo imeufunga mji wa wakaazi milioni 13 kati...
23/12/2021

China yaufunga mji wakati visa vya Covid vikiongezeka kote ulimwenguni
China leo imeufunga mji wa wakaazi milioni 13 katika jaribio la kutuliza mripuko mdogo wa Covid-19, wakati mataifa mengine kote ulimwenguni yakipambana na ongezeko kubwa la maambukizi yanayosababishwa na kirusi kipya cha Omicron.

Mji wa Xi'an kaskazini mwa China umefungwa baada ya kutokea visa vya mamia kadhaa ya maambukizi.

Hata hivyo tafiti za awali kutoka Afrika Kusini na Uingereza zimetoa matumaini, kwa kuonyesha kuwa maambukizi ya Omicron yanaonekana kusababisha idadi ndogo ya wagonjwa wanaolazwa hospitali ikilinganishwa na kirusi cha Delta.
Ulaya imeathirika pakubwa na wimbi linaloongezeka, kwa kurekodi asilimia 60 ya visa vyote ulimwenguni kwa wiki moja iliyopita.

Mchezaji wa timu ya Muscat FC Mukhaled Al-Raqadi amefariki dunia wakati akifanya mazoezi ( warm up) kabla ya mechi ya Mu...
23/12/2021

Mchezaji wa timu ya Muscat FC Mukhaled Al-Raqadi amefariki dunia wakati akifanya mazoezi ( warm up) kabla ya mechi ya Muscat FC dhidi ya Al Suwaiq FC katika ligi ya Oman jana.

Al Raqadi aliyekuwa mlinzi mahiri akiwa na umri wa miaka 29 alipata shinikizo la moyo na kuanguka. Nyota huyo alikimbizwa hospital na gari la wagonjwa lakini kwa bahati mbaya alipoteza maisha.

𝐌𝐀𝐊𝐔𝐍𝐃𝐈 𝐍𝐀 𝐑𝐀𝐓𝐈𝐁𝐀 𝐘𝐀 𝐌𝐀𝐒𝐇𝐈𝐍𝐃𝐀𝐍𝐎 𝐘𝐀 𝐌𝐀𝐏𝐈𝐍𝐃𝐔𝐙𝐈 𝐘𝐀𝐍𝐀𝐘𝐎𝐓𝐀𝐑𝐀𝐉𝐈𝐖𝐀 𝐊𝐔𝐀𝐍𝐙𝐀 𝐉𝐀𝐍𝐔𝐀𝐑𝐈 2, 2022Timu kutoka Tanzania Bara:1. Simba SC2...
23/12/2021

𝐌𝐀𝐊𝐔𝐍𝐃𝐈 𝐍𝐀 𝐑𝐀𝐓𝐈𝐁𝐀 𝐘𝐀 𝐌𝐀𝐒𝐇𝐈𝐍𝐃𝐀𝐍𝐎 𝐘𝐀 𝐌𝐀𝐏𝐈𝐍𝐃𝐔𝐙𝐈 𝐘𝐀𝐍𝐀𝐘𝐎𝐓𝐀𝐑𝐀𝐉𝐈𝐖𝐀 𝐊𝐔𝐀𝐍𝐙𝐀 𝐉𝐀𝐍𝐔𝐀𝐑𝐈 2, 2022

Timu kutoka Tanzania Bara:
1. Simba SC
2. Yanga SC
3. Azam FC
4. Namungo FC

Watanzania watatu wakamatwa Uganda wakidaiwa kuuaPolisi wilayani Kassanda nchini Uganda wanachunguza mauaji ya Emmanuel ...
23/12/2021

Watanzania watatu wakamatwa Uganda wakidaiwa kuua

Polisi wilayani Kassanda nchini Uganda wanachunguza mauaji ya Emmanuel Deus, mtunza fedha wa Kampuni ya GEM James Gold Processing yanayodaiwa kutekelezwa na Watanzania watatu.

Kwa mujibu wa Gazeti la Daily Monitor la Uganda, Deus aliripotiwa kupigwa hadi kufa na kundi la raia sita wa Tanzania Jumamosi iliyopita katika Halmashauri ya Mji wa Bukuya, Wilaya ya Kassanda.

Mkurugenzi wa Habari wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Tanzania, Emmanuel Buhohela aliyesema bado hawajapata taarifa hiyo na kuahidi kuifuatilia.

Kwa mujibu wa polisi, Deus alikutana na kundi la Watanzania wanaojishughulisha na biashara ya dhahabu, wakinywa pombe huko Bukuya na waliingia katika ugomvi uliosababisha watuhumiwa hao kumpiga hadi kupoteza fahamu.

Salamu za Pole kutoka kwa  kufuatia kifo cha mama yake  kilichotokea usiku wa kuamkia leo"Nakupa pole nyingi ndugu yangu...
23/12/2021

Salamu za Pole kutoka kwa kufuatia kifo cha mama yake kilichotokea usiku wa kuamkia leo

"Nakupa pole nyingi ndugu yangu,Champ msiba mzito wa Bi Mkubwa.
Sisi wote ni wake na kwake tutarejea. Nakuombea ustahamilivu.
Najua unaijua dini na maelekezo yake uzuri,la muhimu ni dua kaka. Pole sana bro".

Aliekua kiungo wa klabu ya Simba sc kwa sasa anakipiga miamba ya soka Africa kwenye klabu ya Al Ahly ya nchini misri Lui...
23/12/2021

Aliekua kiungo wa klabu ya Simba sc kwa sasa anakipiga miamba ya soka Africa kwenye klabu ya Al Ahly ya nchini misri Luis Jose Miquissone usiku wa kuamkia Leo amefanikiwa kuvaa medali ya Super cup ya Africa baada klabu yake kuibuka na ushindi dhidi ya Raja Casablanca ya Morocco

Mama mzazi wa Bondia, Hassan Mwakinyo  Bi Fatuma Hassan Siri amefariki Dunia leo Sinza Jijini Dar es Salaam baada ya kuu...
23/12/2021

Mama mzazi wa Bondia, Hassan Mwakinyo Bi Fatuma Hassan Siri amefariki Dunia leo Sinza Jijini Dar es Salaam baada ya kuumwa na kulazwa Muhimbili kwa siku sita kutokana na kuwa na uvimbe tumboni.

kupitia kwenye ukurasa wake wa Twitter ameandika haya

"K**a kuna siku nimekosa raha ya kila kitu ulimwenguni ni kukukosa wewe Mlezi wangu,Mama mzazi nilie yatoa maisha yangu kwa utayari wa kufanya kila kitu kwa ajili yako nikulee mzee wangu lakini kwa mungu haikuwa ridhiki eeh yaaarab nijalie ustahamilivu msiba wa mama yangu kipenzi"

VIFO 739 VYA KORONA TANZANIAWaziri wa Afya Maendeleo ya Jamii, Jinsia Wazee na Watoto, Dr. Dorothy Gwajima amesema mpaka...
23/12/2021

VIFO 739 VYA KORONA TANZANIA

Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii, Jinsia Wazee na Watoto, Dr. Dorothy Gwajima amesema mpaka sasa nchini Tanzania ni Watu 739 wamefariki tangu ugonjwa wa covid-19 uingie nchini huku idadi ya Wagonjwa waliopatwa na ugonjwa huo hadi sasa ikifikia 28218.

Dr. Gwajima ameyasema hayo mkoani Arusha akizindua kampeni harakishi na shirikishi kwa Jamii awamu ya pili ya mapambano dhidi ya covid-19 na kuhudhuriwa na Viongozi wa Serikali, Dini na Wananchi wa Arusha na Mikoa ya jirani.

Dr. Gwajima amewasisitiza Watanzania kujitokeza kwenda kuchanjwa na kuongeza kuwa katika Wagonjwa 10 waliolazwa Hospitali kutokana na covid- 19, Wagonjwa 8 kati yao hawajapata chanjo na kwamba Wagonjwa wawili waliochanja wakipata ugonjwa hupata nafuu mapema ikilinganishwa na ambao hawajachanja.

  Amemnunulia Dancer wake   Zawadi Ya Gari Aina Ya Crown Hii Ni Baada Ya kufanya Nae kazi kwa muda mrefu na Juhudi Alizo...
23/12/2021

Amemnunulia Dancer wake Zawadi Ya Gari Aina Ya Crown Hii Ni Baada Ya kufanya Nae kazi kwa muda mrefu na Juhudi Alizo zionyesha Dancer uyo kwenye utendaji wake wa kazi

Address

Mabibo Georage
Dar Es Salaam

Telephone

+255756467012

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Rabbi Tv Tanzania posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Rabbi Tv Tanzania:

Share