03/05/2022
Anaitwa .
Jana J2 alihubiri kwenye hema ya Nabii Mkuu Mheshimiwa GeorDavie iliyoko Kisongo Arusha....Na alihubiri kwa dakika kadhaa kumtangulia Nabii huyo ambaye inawezekana walipangana mapema ya kuhubiri.
Kwenye Mahubiri yake alisema "hakuna sababu ya kuhubiri ukitaja mitume na manabii k**a Petro au Yuda ambao hatujawaona kwa macho wala hatujui sura zao."
Alisema yeye ameamua kuhubiri kuhusu Nabii Mkuu GeoDavie na atamtangaza kwa nguvu zake zote na yuko tayari kufa akitangaza jina la GeorDavie Nabii Mkuu na siyo Yesu.
Alidai aliwahienda South Africa alialikwa k**a mwimbaji.....sasa ili aheahimiwe akadanganya yeye ni Nabii mkuu sana kutoka Tanzania, na alipopewa madhabahu kuhubiri akaletewa kiwete akamwombea k**a watumishi wengine wanavyoomba (akimaanisha kwa jina la Yesu) lakini kilema hakupona, mwisho akakumbuka Ngurumo ya Upako na Mungu wa GeorDavie.
Akaanza kuonba kwa jina la ngurumo mungu wa GeorDavie, yule kiwete kupitia mungu wa GeorDavie akapona. Akasema nilipokuja hapa Kuna watu walitegemea nihubiri acha uzinzi, akasema hapana nimekuja kumhubiri Nabii mkuu maana ndiye aliyechagua kumhubiri......Ndiye ampaye kula na kulipa Kodi ya nyumba na atamtangaza Kila mahali maana kumtangaza yeye ni kupata promotion.
Halafu Nabii akawa nyuma na anatikisa kichwa....anagurahia sifa anazozipata kutoka kwa kiumbe k**a yeye. Akamzawadia milioni 2 na kumpa mil 1 Kila mwezi kwa miezi 10.
Inasikitisha sana😭😭😭😭
Kwa upande wangu nikimsikia mtu anashuhudia na kunisifu vile, nitazima maiki na kularua mavazi yangu nibaki uchi ili watu wanione ni mtu k**a wao na sina sehemu Yoyote kugusa utukufu wa Bwana hata robo.
Najiuliza tu neno moja, Huyu Nabii mkuu au bashando hajajua Bado sauti ya Neno hili na uzito wake? “Mimi ni Bwana; ndilo jina langu; na utukufu wangu sitampa mwingine, wala sitawapa sanamu sifa zangu.” Is 42:8
Matebdo 14
Makutano walipoona miujiza aliyoifanya Paulo wakapaza sauti zao, Miungu wametushukia kwa mifano ya wanadamu. Kuhani wa Zeu ambaye hekalu lake lilikuwa mbele ya mji, akaleta ng'ombe na taji za maua hata malangoni, akitaka kutoa dhabihu pamoja na makutano kumpa Paulo na Barnabas. Barnaba na Paulo, waliposikia wakararua nguo zao, wakaenda mbio wakaingia katika makutano, wakipiga kelele, wakisema, Akina bwana, mbona mnafanya haya (mnataka kutukosanisha na Mungu?) Sisi nasi tu wanadamu hali moja na ninyi; twawahubiri habari njema, ili mgeuke na kuyaacha mambo haya ya ubatili na kumwelekea Mungu aliye hai, aliyeumba mbingu na nchi na bahari na vitu vyote vilivyomo.....sasa mbona mnatusujudia na kutusifu sisi?
Mitume wa kabisa la kwanza walikuwa ni wanyenyekevu sana......baada ya Petro na yohana kumnyanyua kiwete watu wakaanza kuwatazama wao......“Hata Petro alipoyaona haya akawajibu wale watu, Enyi Waisraeli, mbona mnastaajabia haya, au mbona mnatukazia macho sisi, kana kwamba tumemfanya huyu aende kwa nguvu zetu sisi, au kwa utauwa wetu sisi?” Mat 3:12
Walikuwa wanajua kumpa Bwana utukufu afanyaye yote hayo......Hata Roho mtakatifu Yesu alisema hatanena kwa shauri lake mwenyewe Bali yote atayatoa kwangu na atanishuhudia Mimi......INAKUWAJE NINYI MNAMSHUHUDIA MTU NA KUMWINUA YEYE😠
By
Kuhani Mwakalambo