Business And Employment Motives

Business And Employment Motives Contact information, map and directions, contact form, opening hours, services, ratings, photos, videos and announcements from Business And Employment Motives, Advertising/Marketing, Gongo la Mboto, Dar es Salaam.

02/08/2020

UJUMBE WA LEO: HIZI NDIO MBINU KUU ZINAZOWEZA KUKUSAIDIA KUUPATA UTAJIRI

1. Epuka kampani na watu wasio na malengo wala mawazo mapya kimaendeleo.

Ili kufanikiwa katika maisha inabidi ukae na watu makini wenye PLAN na idea za kimaendeleo ili uweze kuongeza mbinu na maarifa katika kuongeza kipato, usipende kukaa na watu wenye story za michezo, mizaha,utani, muziki, umbea, siasa, mapenzi na porojo nyingine maana huto gain kitu.

2. Okoa muda
Usipende kuwa mtu wa kupoteza muda kwenye mambo yasiyosaidia kuongeza kipato chako, usipende kupumzika kupita kiasi fanya kazi k**a mtumwa ili uje uishi k**a mfalme. Hakikisha kila inapopita siku unapiga hesabu umefanya lipi la maana na limekuingizia kiasi gani katika maendeleo yako.
3. Kuwa na mipango ya uhakika.
K**a una nia kweli ya kutoka kweli kwenye umaskini ulionao, hakikisha pia una mipango ya uhakika ya kukutoa pale ulipo. K**a unataka kufanya kitu fulani, tafuta njia itakayokutoa na hasa tafuta mtu mwingine aliyewahi kufanikisha jambo hilo unalotaka kulifanya.

Weka mipango ya uhakika na inayowezekana kwako kuifikia. Jifunze haya yote kwa wale waliofanikiwa zaidi yako. Unapokuwa na mipango ya uhakika inakuwa ni rahisi sana kwako kuifatilia na kiutekeleza. Acha kupanga mipango yako bila ya kuifatilia, ipange mipango yako kisha uifatile. Ikiwa huwezi kufatilia mipango yako nani ataifatilia?

4. Jifunze kutokukata tamaa mapema.
Hii ni njia muhimu sana kwako ya kukufanya wewe kuwa tajiri na kukutoa kwenye umaskini ulionao. Ukiwa na uwezo wa kupambana na vikwazo, ndicho kitu kitakachokufanya ufanikiwe zaidi, na si kukata tamaa na kuacha. Kila safari ya mafanikio ina changamoto zake na vikwazo vyake, hivyo inabidi kukabiliana navyo.

Utaweza kufika kule unakotaka , ikiwa utakuwa uko tayari kupambana na vikwazo vitakavyotokea njiani. Vikwazo vyote ni nafasi ya kufanikiwa k**a utajifunza kitu kwenye hivyo vikwazo au matatizo yanayokuzunguka.

5. Jifunze kufanyia kazi ndoto zako kila siku.
Hii iko wazi kabisa ikiwa utaendelea kufikiria tu, unalofikiria litaendelea milele kubaki kwenye fikra zako na si zaidi. Ni lazima ufanye mambo kwa vitendo ili uweze kujikwamua na umaskini. Unatakiwa kuanzia mahali fulani hasa pale ulipo.
Mpaka utakapoanza ndipo utakapopata matokeo yatakayokusaidia kuweka misingi bora na mwelekeo wako. Ndege ni lazima ianze kwa kuruka inapofika hewani huanza kujiweka sawa ili upate mwelekeo mzuri wa kule inakokwenda.

Ni lazima uanze na mahala fulani popote, si lazima iwe mahala maalumu k**a unavyofikiri, wewe anza tu kufanyia kazi ndoto zako mambo mengine yatajipanga mbele ya safari. Acha kusita sita fanyia kazi ndoto zako ili ufanikishe kile unacholenga.

6. Jifunze kuwa na bajeti maalumu katika maisha yako.
Unapokuwa na bajeti hii itakusaidia wewe kuwa na taarifa nyingi za matumizi na mapato ya pesa zako binafsi na za biashara zako. Ikiwa kila siku unaishi maisha ya kutoweka kumbukumbu hiyo itakusababishia kutojua wakati unapopoteza fedha bila ya sababu hadi hali yako itakapokuwa mbaya zaidi.

Jijengee utaratibu wa kujiwekea bajeti hii itakufanya hautatumia pesa hovyo na hizo pesa utakazozotunza zitakusaidia sana katika kuwekeza pale zitakapokuwa nyingi na hatimaye zitakutoa kwenye umaskini.

7. Jijengee tabia ya kijiendeleza zaidi.
Ni watu wachache sana ambao huwa na tabia ya kujiendeleza kwa kujisomea mara baada ya kumaliza masomo. K**a unataka kuondokana na umaskini hakikisha unasoma mambo mengi na mapya ili kukabiliana na changamoto zaidi za dunia ya sasa.

Bahati mbaya sana mfumo wetu wa elimu tulionao sasa hautusaidii sana kuhusiana na hali halisi ya maisha yetu, hivyo usifikirie kwamba kwa vile umefika chuoni, basi una kila nyenzo ya kukufanya ufanikiwe. Unatakiwa kuendelea kujifunza, watu wenye mafanikio ni watu wakujifunza sana katika maisha yao yote.

Kumbuka ukitaka kufika hadi kwenye kilele cha mafanikio unaweza endapo tu utaamua mwenyewe, hizo ndizo njia muhimu unazoweza kuzitumia kukutoa kwenye umaskini ulionao......

8. Chunguza na kuzifanyia kazi fursa zinazopatikana mahali na wakati husika.

Siku zote fursa zinazojitokeza katika eneo huihitaji uchunguzi wa kina ili kuzibaini, jitahidi kufanya utafiti ujue ni fursa gani katika eneo ulilopo au popote na unaeza ukaitumia vipi kujiendeleza kisha ifanyie kazi. Usiwe mtu wa kuzubaa na kushangaa shangaa, you must be flexible
9. Epuka mapenzi na utani katika kazi

Ni ngumu mno kufanikiwa k**a umeendekeza mambo ya masihara na utani mwingi pamoja na ngono, utapoteza muda wako na rasilimali ikiwemo fedha hatimaye utajiri utabaki kuwa ndoto tu katika maisha yako. Hamna kupe wabaya wanaorudisha watu nyuma kimaendeleo k**a michepuko na wachuna mabuzi yaani wao kila ukigeuka wanakupiga mizinga bajeti yako inakua mara mia.

10. Jitahidi kusoma vitabu na historia ya watu waliofanikiwa kimaendeleo ujue walifanya vipi uongeze maarifa, omba ushauri kwa waliofanikiwa pale inapobidi usijifanye unajua kila kitu, mawazo ya wengine yaweza kukuongezea idea mpya katika kukabili changamoto zingine zitakazo jitokeza katika harakati zako kimaisha na kimaendeleo unazopitia kila siku.
Usipoteze muda wako kuangalia series na season za kikorea, Usipoteze muda wako kujadili maisha ya watu, epuka kupoteza muda kufuatilia umbea na udaku fuatilia fursa na mijadala ya kijasiriamali.

11. Mtangulize Mwenyezi Mungu katika kazi zako Na Mipango yako

Pasipo uwepo wa Mungu katika mipango na kazi zako shetani aeza pata nafasi na kufanikisha mipango yake miovu dhidi yako na kukusababishia anguko, kufilisika, maradhi au kifo na hivyo kukwamisha maendeleo yako. Zipo hila chafu katika kazi mfano chuma ulete katika biashara ambapo washirikina hutumia nguvu za giza kukwamisha watu hivyo ni muhimu kuomba ulinzi wa Mungu siku zote katika harakati zako kimaisha na kimaendeleo.

C&P

You must work on yourself continuously, never be satisfied with yourself. Always know that as you invest the time and ef...
22/01/2020

You must work on yourself continuously, never be satisfied with yourself.
Always know that as you invest the time and effort on you that’s the greatest ability that human beings have above animals.
A dog can’t be anything but a dog, a tree can’t be anything but a tree.
Human being, you’ve got unlimited potential, you can put effort into you.
And by concentrating on you and developing you, you can transform your life no matter where you are right now.

20/09/2019

GET ADDICTED!!

Wataalam wa mambo wanakwambia kuwa Addiction yoyote kwenye kitu positive huwa inamfanya mtu awe na Impact kubwa sana kwenye Ulimwengu. Hata ulimwengu wenyewe ume-prove hili kuwa kila mtu aliyefanikiwa kwa kiwango kikubwa cha hali ya juu basi mtu huyo anafahamika kwa kitu kimoja tu ambacho alikuwa addicted nacho ambacho ndicho kimefanya afanikiwe kwa kiwango hicho.

Bill Gates alikuwa addicted kwenye Computer Programming iliyosababisha atengeneze Oparating System kwenye Computer ambayo ndiyo imemfanya awe Bilionea wa dunia. Aliko Dangote tangu akiwa mtoto alikuwa addicted kwenye biashara ambayo ndiyo imemfikisha kuwa tajiri namba moja Afrika. Elon Musk ni addict wa Electronics kitu kilichopelekea afanye mambo makubwa kwenye teknolojia ya vifaa vya anga. Addiction ya Steve Jobs na Steve Wozniak kwenye Electronics ndiyo imeleta mapinduzi makubwa kwenye teknolojia ya computer na smartphone. Get addicted kwenye eneo lako!!

Addiction ni kitu muhimu sana kwa mtu yeyote mwenye ndoto kubwa. Hutakiwi kuwa addicted na mapenzi. Hutakiwi kuwa addicted na hobbies zako. Hutakiwi kuwa addicted na starehe. Hutakiwi kuwa addicted na mpira."The Only thing you must get addicted to is YOUR DREAM". Ongea yako ifanane na ndoto yako. Tembea yako ifanane na ndoto yako. Life style lako lifanane na ndoto yako. Yaani ifike hatua watu wakitaka definition ya kitu ambacho ni ndoto yako basi wawe wanakuoneshea tu wewe.

Siku moja nilikuwa nasikikiza interview ya Michael Jackson akaulizwa "Michael Do you love music??" Jibu alilotoa lilibadilisha kabisa mtazamo wangu kuhusu ndoto yangu, Alijibu akasema "I don't just love music, I AM THE MUSIC" Akimaanisha kuwa "Siyo tu kwamba napenda muziki bali Mimi mwenyewe ni Muziki". Akaendelea kujibu kwa kusema "Nikilala, nalala nasikiliza muziki, ndoto naota za muziki tu, Bora nisile chakula lakini nisikilize muziki na niimbe muziki, Mavazi yangu ni ya kumuziki, Nakula huku nasikiliza muziki au huku naimba. Huwezi kumtenganisha Michael Jackson na muziki na huwezi kuutenganisha muziki na Michael Jackson". Akahitimisha kwa kurudia kusema "I AM THE MUSIC".

Ili kufika level ya kuwa addicted kwenye kitu chochote ni lazima uwe umefanya hicho kitu mara nyingi iwezekanavyo na uendelee kukifanya. Ukifika level ya positive addiction kwenye jambo lolote maana yake ni kuwa uwezo wako kwenye hilo eneo ni mkubwa kiasi cha kuweza kufanya lolote kwenye hilo eneo. KWENYE ENEO LA NDOTO YAKO HAKIKISHA UNAKUWA ADDICTED. K**a unaimba basi get addicted kwenye muziki. Kwenye Professional yako get addicted ili ujitofautishe na wengine. Kwenye kipaji chako get addicted. Kwenye Biashara get addicted. Kila mtu kwenye eneo la ndoto yake ahakikishe anafika level ya Addiction ili ajiweke kwenye kundi la washindi wa level ya Ulimwengu mzima!!

Live Your Dream!!

20/08/2017

Akiwa na miaka 5 Alifiwa na Baba yake,

Akiwa na miaka 16 aliamua kuacha shule,

Akiwa na miaka 17 tayari alikua kapoteza ajira 4,

Akiwa na miaka 18 aliamua kuoa,

Akiwa na miaka kati ya 18-22, alikua msimazi wa njia za reli lakini alishindwa akafukuzwa,

Baadae alijiunga na Jeshi lakini akafukuzwa pia,

Akatuma maombi shule ya sheria ila hakupata nafasi,

Akawa muuzaji wa Bima lakini alishindwa pia,

Akiwa na miaka 19, alifanikiwa kuwa Baba,

Akiwa na miaka 20, Mke aliamua kuondoka na mtoto,

Hatimaye akapata ajira k**a mpishi na mwosha vyombo wa mgahawa mdogo,

Alishindwa hata katika jaribio la kumpata mwanae, na kuamua kumshawishi mkewe kurejea nyumbani,

Akiwa na miaka 65 alistaafu ajira yake ya kupika na kuosha vyombo katika mgahawa,

Baada ya kustaafu alipata mafao yake kutoka serikalini dola 105 $, k**a Tsh 231,000/=.

Alidhani serikali imemuona k**a hajiwezi kabisa,

Akafanya jaribio la kujiua, akiamini hakuna thamani ya kuishi tena, na kwamba ameshashindwa sana. Hakufanikiwa hata ktk jaribio lake hilo,

Akaamua kukaa chini ya mti na kuandika matarajio yake, Ila aliona ayaandike yale aliyoyakamilisha tayari,

Akagundua kuna mambo mengi hakuyafanya bado. Akagundua lipo jambo moja ambalo anaweza kulifanya vizuri zaidi kuliko mtu yeyote yule anayemfahamu,

Na Ilikua ni namna gani ya Kupika,

Akaamua kuchukua dola 87 $ k**a Tsh 191,400/= kutoka kwenye Hundi yake ya pensheni na kununua kuku. Akawakaanga kwa kuwachanganya na viungo anuai akapata mchanganyiko wa aina yake (unaovutia),

Akaamua kupita mlango kwa mlango kuwauza kwa majirani zake huko Kentucky. Mchanganyiko ule ukapendwa sana na akaamua kuanzisha mgahawa wake uitwao Kentucky Fried Chicken (KFC) uliokua ukitengeneza mchanganyiko wa kuku alioubuni.

Hatimaye biashara yake ikakua na akafungua migahawa mingi ya KFC nchini Marekani. Mchanganyiko ule ukazidi kupendwa na kutanua wigo wa biashara yake.

Huyu si mwingine ni Colonel Harland Sanders mwanzilishi wa migahawa ya KFC duniani. Licha ya kustaafu akiwa "fukara wa kutupwa" katika umri wa miaka 65, lakini hadi wakati anafariki (1980) akiwa na umri wa miaka 90 alikua katika orodha ya mabilionea wakubwa nchini Marekani.

Kwa sasa migahawa ya KFC imeenea kote duniani katika nchi 123, Tanzania ikiwemo, na ni mgahawa wa pili mkubwa ulioenea zaidi duniani baada ya migahawa ya McDonald's.

Mwaka 2013 migahawa ya KFC ulifanya mauzo ya dola Bilioni 23 sawa na Tsh Trilioni 50. Maana yake ni kwamba mauzo ya KFC kwa mwaka mmoja ni sawa na bajeti ya Tanzania kwa miaka miwili.

Kumbuka muasisi alikua FUKARA hadi uzee wake (miaka 65) na akadhani ameshindwa maisha. Akajaribu kujiua. Lakini baada ya kutafakari akaona bado ana nafasi ya kujaribu tena. Akajaribu japo katika umri wa uzee, na hatimaye Mungu akamfanikisha. Akawa BILIONEA MKUBWA sana nchini Marekani.

Je wewe umekata tamaa ya maisha? Ulitamani kusoma lakini ukashindwa kwa kukosa ada? Umesoma lakini umekosa ajira? Miaka inapita na unaona wenzio wanaajiriwa wewe uko tu nyumbani? Je Umejaribu biashara lakini kila wakati unapata tu hasara? Unahisi kukata tamaa? Unahisi Mungu amekuacha?

Usikate tamaa. Mungu hajakuacha. Jipange tena na uanze upya. Haujakawia bado.... Kitu kikubwa ni "Mtazamo" ( Attitude).

Usikate tamaa .... Haijalishi mambo ni magumu kiasi gani. Una kila kitu cha kukufanya Ufanikiwe, Amua kubadili mtazamo ili kubadili Stori ya maisha yako. Inawezekana, anza sasa.!

©Greataziz

See You At The Top

USIANGALIE PESA, ANGALIA KILICHO NYUMA YA PESA ZA MAYWEATHERSiku zote ukitaka kufanikiwa, usiangalie vitu kwa negative w...
29/07/2017

USIANGALIE PESA, ANGALIA KILICHO NYUMA YA PESA ZA MAYWEATHER

Siku zote ukitaka kufanikiwa, usiangalie vitu kwa negative way, yaani ukiona mtu kapiga picha na hela, usiseme anajidai, akipiga picha na gari kali, usiseme anakuringishia bali unachotakiwa ni kujiuliza yeye kapataje na mimi nashindwaje?

Huyu jamaa namkubali sana, huwa anasema kwamba anapenda kuonyesha pesa kwa anataka sisi tusiokuwa nazo tuumie na twende kuzitafuta, ila tatizo linalokuja kwa sisi masikini, tunaanza kuangalia jambo kwa negative way.

Anapambana, anakesha gym akichukua mazoezi, wakati mwingine anajinyima akitafuta, kwa nini asiyafurahie maisha? Tunachotakiwa ni kupambana k**a yeye kwa kuamini kwamba kuna siku na sisi tutafanikiwa.
Anaingia ulingoni, anastaafu, akitangaziwa dau anarudi tena, anapambana. Hebu jiulize, una roho ya kupambana? Unaweza kukesha usiku mzima ukifanya kitu ambacho unaamini kitakuingizia pesa?

Watanzania wengi hatuna roho ya upambanaji, tunaridhika, tukiwa na milioni kumi benki tunaona tumemaliza kila kitu. Ndugu zangu, hata ukiwa na trilioni 100, bado utatakiwa kupambana pesa ziongezeke.

15/06/2017

★"TUPATE SHULE KIDOGO"★

Kati ya sifa kubwa unayotakiwa kuwa nayo ili uweze kufanikiwa kimaisha ni uwezo wako wa kughairisha (suspend) mambo yanayokupa raha kwa muda mfupi ili kujenga mambo yatakayokupa furaha kwa muda mrefu.

Mwanzoni mwa 1960 Professor Walter Michael wa chuo kikuu cha Stanford alifanya jaribio fulani la tabia ambalo limekua marufu sana miongoni mwa wanazuoni wa sayansi ya jamii na saikolojia. Jaribia hilo linajulikana k**a “Marshmallow Experiment”.

Katika utafiti huu aliwajaribu watoto wadogo k**a 100 wenye umri wa miaka minne na mitano. Aliwaweka katika chumba na akawawekea kila mmoja kipande cha mkate mtamu wenye chocolate.

Kisha akawaambia "K**a nikirudi nikakuta haujala huu mkate nitakupatia kimkate cha pili, ila k**a nikirudi nikakuta umeshakula sitakupatia kitu."

Kisha akawaacha kwa dakika kumi na tano (15) wakiwa peke yao chumbani halafu akarejea. Aliporudi alikuta matokeo k**a ifuatavyo:

1. Zaidi ya watoto 60 walibugia ile mikate baada tu ya yule Profesa kutoka. Yani alipofunga mlango tu wao wakala mara moja ile mikate licha ya ahadi waliyopewa.

2. Watoto 30 walijitahidi kujizuia kwa kujizungusha zungusha lakini mwishoni walikula.

3. Watoto wachache sana (chini ya 10) ndio walioweza kujizuia na kutokula ile mikate kwa dakika zote 15. Watoto hawa waliacha kula wakiwa na matarajio ya kupata mikate ya ziada k**a walivyoahidiwa.

Profesa Walter aliwafuatilia watoto hawa kwa muda wa miaka 40 mfululizo na uligundua yafuatayo;

1. Watoto walioshindwa kujizuia walikua na maisha mabovu baadae. Hawakujua umuhimu wa kuweka akiba. Walitumia pesa zote walizopata kwa starehe. Hawakuwa wabunifu na walitegemea zaidi kazi za kuajirdiwa ktk maisha yao yote.

2. Watoto waliojizuia kwa muda mfupi lakini badae wakala hawakua na maisha yenye msimamo. Walipanga mipango ya maendeleo lakini hawakuikamilisha kwa sababu ya hofu ya kushindwa. Baadhi walianzisha biashara lakini zilipoyumba kidogo walirudi kuajiriwa na hawakufanya biashara tena.

3. Watoto ambao walikuwa na uwezo wa kujizuia na hawakula kabisa ile mikate walikuwa na mafanikio makubwa sana kimaisha. Hawakujiingiza katika matumizi ya madawa ya kulevya, walikuwa na nidhamu ya fedha na walikuwa waaminifu ktk ndoa zao na maisha kwa ujumla.

★Hii inaitwa “The power of delayed gratification” yani nguvu ya kuweza kujizuia vinavyokufurahisha kwa muda ili uweze kufaidi vitu vya muda mrefu katika maisha yako.

★MORAL:

★Kupitia theory hii ya Prof.Walter tunajifunza mambo mengi katika maisha. Kwa kawaida mambo yanayotuharibia "direction ya maisha" ni yale yanayotupa raha kwa muda mfupi lakini huwa yana madhara mengi kwa baadae.

★Kwa mfano; kuangalia "movies" kwa masaa inakupa raha ya muda mfupi lakini ungetumia muda huo kujiendeleza katika ujuzi kwa kusoma au kufanya biashara kungekupa matokeo mazuri na ya muda mrefu.

★Kwa kawaida tunapenda kujiachia na kufanya mambo yanayotupa raha ya muda mfupi bila kujali matokeo yake hadi baaada ya miaka mingi sana ndipo tunakuja kujutia. Mwanzoni unaweza kuona k**a hakuna madhara yoyote unayopata kwa sasa.

★Hujawahi kukaa na wazee wakaanza kukupa story zao walivyokula bata zamani? Watakuambia mahali fulani viwanja vilikua bei Rahisi sana lakini cha ajabu hawakukunua. Kwa wale wazee walioishi Dar enzi hizo ukimkuta atakwambia Segerea ilikua pori, ulikua ukienda na senti 50 ukimpa Mjumbe unajipimia eneo mwenyewe. Lakini yeye bado anaishi nyumba ya kupanga. Unajiuliza mbona yeye alishindwa kujipimia.??

★Au anakwambia Mbezi Beach viwanja vilikua vinalingana bei na kreti moja ya bia. Lakini unashangaa yeye hakununua. It means "aliopt" kreti ya bia instead of kiwanja. Maana yake ni kuwa alichagua jambo la kumpa raha muda mfupi lakini akateseka badae muda mrefu.

★Uwezo wako wa kujizuia kutonunua nguo za gharama kwa sasa ili kuwekeza ndio utakaokufanya uwe na maisha mazuri kesho. Uwezo wako wa kujizuia kutonunua simu ya gharama kubwa leo ili usave pesa yako kwa badae ndio kiini cha mafanikio yako.

★Uwezo wako wa kujizuia kutoishi kwenye nyumba ya gharama kubwa ili utunze pesa ununue kiwanja chako ndio utakaokufanya ujenge kwako na uondokane na nyumba za kupanga.

★Kila wakati jitahidi kuwa mtu unayeweza kujizuia kufanya vitu vinavyokupa raha ya muda mfupi ili uweze kujenga msingi wa kupata mafanikio ya muda mrefu maishani mwako.

★Leo jiulize ni vitu gani maishani mwako ambavyo vinakupa furaha ya muda mfupi lakini vinakuharibia malengo yako ya muda mrefu? Ukiweza kuvitambua, mara moja dhamiria na anza kuviepuka ili kujenga msingi imara wa mafanikio yako ya muda mrefu.

★Kumbuka, k**a hautakuwa tayari kuumia kidogo leo ili upate raha ya muda mrefu, utajikuta unapata raha kidogo leo na unaumia maisha yako yote.

★Akina Bakhresa, Mengi, Dewji walikubali kuteseka kwa muda fulani ili waje wapate raha ya muda mrefu.

★Bakhersa aliwahi kusema kuwa alianza biashara yake k**a "baba lishe" kwa kuuza mgahawa huko Z'bar. Alikubali kuteseka kwa muda mfupi ili atengeneze kesho yake. Leo Bakhresa ni bilionea. Angeamua "kula bata" kipindi hicho bila shaka asingekuwa hapa alipo leo. Pengine angekua bado anasugua sufuria kule Zanzibar akipikia watu.

★Mabilionea wakubwa k**a Mark Zukerberg, au Bill Gates leo wana maisha mazuri kwa sababu walikubali kuteseka kwenye "jana yao".

★Sasa wewe umeanza kazi leo unataka "udrive" wakati huna hata mwaka kazini. Unadhani kesho yako itafanikiwa?

★Unalipwa "milioni moja" lakini umepanga nyumba ya laki 5 kwa mwezi. Unafurahia watu wakija kwako wanasifia geti la gharama kubwa na kukupamba "unakaa nyumba kali". Unalewa sifa na kusahau kwamba hilo geti ni la mwenye nyumba na wewe ni mpangaji tu. Aisee my friend Sahau kitu kinachoitwa mafanikio kwako. Utaishia kukaa nyumba za kupanga hadi uzeeni.

★Kubali uteseke muda mfupi leo ili ufurahi muda mrefu kesho, au amua kufurahi muda mfupi leo na uteseke muda mrefu kesho. Uamuzi ni wako.!

10/03/2017

.
*LIFE BEGINS AT 40.... HOW OLD ARE YOU?*

Life Begins at 40..

Huo ni msemo wanao waingereza wakimaanisha maisha yako ijapokuwa yanaanza toka milele iliyopita na toka umeumbwa au toka umefika duniani na toka umeanza kukua nk nk lakini bana maisha yataanza rasmi siku ukitimiza *miaka 40.*

Hapo k**a bado nauli ya *daladala ni ishu, ada, chakula, kodi ya nyumba, nk* basi ndo utaanza kuelewa maana ya muda uliokuwa unatumia Facebook kulike picha za ajabu na story zisizokupeleka popote.
Nadhani unanielewa sasa hasa wewe ambaye unahisi umri wako bado ni mdogo kwa hiyo bado bado kidogo muda wa kuwa serious na maisha haujafika.

Sikia kijana mwenzangu *TODAY* is your future kwa taarifa yako..

Ulipokuwa mdogo ulisema, nikiwa mkubwa nitakuwa na gari na nyumba nzuri wazazi wangu wataishi hivi na vile. *Je unayo?* Je imetokea? Maybe yes. But maybe no.

K**a haijatokea je bado *hujawa mkubwa?* Basi k**a ni mkubwa ujue kuna *kitu hujafanya.*

*Utasema tena nikifika miaka 40* nataka niwe na hiki na kile watoto wangu wasome international school nk. Subiri uone miaka inavyoenda.

Usishangae kufika *40* bado umeajiriwa kwa mtu na anakugombeza kwa nini mwanao anaumwa kila siku unachelewa kazini.

*Kazi nyingi. No bright future. No enjoyable present. Just existing and not living!*

Hapo ndo unawaza kufuga *ng'ombe* wa maziwa Kibamba kwenye kiwanja chako cha miguu *12 kwa 15!*

Wenzako wa umri wako hapo unasikia wameanzisha *bizness in Australia.*

Wamenunua kiwanja Mbezi Beach kwa *300M!* Wamejenga mjengo wa ukweli.

Wanamiliki Apartment Johannesburg. Wakienda UK wanaenda kula The Ritz *(Google that).*

Wanasomesha watoto zao the finest schools available wewe wa kwako wakati huo wamekosa nafasi Makongo wameenda Kibamba Secondary School wanapanda daladala sita kwenda na kurudi full *kutukanwa na makondakta.*

Wenzako in their *40s* wanasaidia wasio na uwezo katika jamii wewe ndo kwanza ukipokea simu kutoka kijijini mzazi anahitaji support kidogo *una-mute!*

Wenzako in their *40s* wakisikia kuna ujenzi wa nyumba ya ibada wanachangia *5M* kimyakimya.. Wewe ukitoa *laki moja* basi mpaka mtaa wa saba watajua! Halafu unashangaa wenzako wanazidi kuinuliwa. Unaanza kuwaita *Freemason.* Mwenye nacho ataongezewa au hujui? Na asiye nacho..... *(Malizia)*.

Wakati wenzako walikuwa wanajenga maisha wewe ulikuwa unashinda Facebook kuongelea UKUTA uwepo au usiwepo.. Sijui kuvunja viti uwanja wa taifa. Harmonize anajua kuimba au hajui. Wema Sepetu atafute mtoto au aache tu. *Can you imagine?*

Wenzako mkifika miaka 40 watu wa rika lako wana exposure ya uhakika. Wewe at 40 bado umeajiriwa na mchana unakula kwa mama lishe chakula hata virutubisho hakina. Wenzako at 40 washaacha ajira siku nyingi washatembea dunia na kujifunza maisha kutoka kila mahali. Walishafika kuanzia *Sauzi, Botswana, Mozambique, Kenya, Ethiopia, Ghana, Naija, mpaka Egypt, The UK, Australia, Hawaii, Mexico, Croatia, The Netherlands, Switzerland, US, Panama mpaka Puerto Rico, Brazil na jirani zake, Hong Kong, Australia, Japan, China, (Incredible) India, Thailand, Singapore, New Zealand, Comorros, you name it..!!*

Wewe hata Kampala hujawahi fika. Kila siku *Tegeta Posta* ndo ruti yako miaka 15 mfululizo eti unatafutia watoto maisha! *Unaishi* au *unaisha?*

Acha mawazo mgando. *Eti mi nina mshahara mzuri.* Mshahara mzuri? Kweli?

*Sikia, hiyo ajira ifanye serious sana tu lakini kwa muda tu.*

Jiandae kusimama mwenyewe.

*Kwani hujiamini? Na Mungu naye humwamini?* Changamoto ni sehemu tu ya kufika kileleni. *Don't be afraid*. Don't dwell in that comfort zone!! *Unasubiri kiinua mgongo?*

*Utaenda kukiinvest wapi na kwa nguvu ipi.*

*Na utaenjoy retirement kweli k**a at 60 yrs ndo unafungua duka la vifaa vya ujenzi eti vinalipa.*

Kwa nini hukufungua ukiwa *30yrs* ili uone vinalipa au la. At 60? With due respect. Kisa ulikuwa unafatilia ratiba zote za mechi za mpira na matamasha na mikutano yote ya kisiasa ukasahau muda unaenda. Hao unaowafatilia wako ndani ya kazi zao kwa hiyo muda wao unatumikia shughuli zao wakati wewe utatumia muda wako na pesa yako kwenda kuangalia nk.

*Jenga nidhamu mpya ya kulinda muda wako sasa.*

*Suffer the pain of discipline now. Or else you will suffer the pain of REGRET.*

Halafu ukianza kuregret ndo *pressure zinakuja, stress,* nk mwisho unawacha hata hao watoto in a far worse situation than your own lifetime. Kisa? Ulikuwa unatumia muda wote kuangalia vitu vya kuchekesha chekesha na kuongelea mambo ya siasa sijui wasanii sijui msanii gani ana hela nyingi sijui nani kafulia sijui nani ana mimba.. Seriously? Sijui nani hajapendeza kunyoa bora asuke😡😠😠. Hivi vitu vinaiba muda wako sana.Mimi nimeshtuka mapema sana! Utashangaa umri unaenda bila kupiga hatua. Umri wako ni kila sekunde na kila dakika na kila saa. Ndo umri huo. Umri siyo mwaka kwa mwaka. Ni sekunde na dakika. Ndo maana matajiri wanalinda muda wao kwa wivu mkali. Coz TIME IS MONEY. Utashangaa unapoteza muda afu unafika 40 years ndo unawaza uanzie wapi. Mungu siyo mjinga kukupa umri huu wa ujana. Hajakupa uuchezee chezee tu. Be careful. Time flies.

*Life Begins at 40 my friend.. How Old Are You?* So k**a wewe unasema "Mimi bado mdogo.." endelea tu kupoteza muda wako utakumbuka tu siku moja but it might be too late. Endelea tu kupoteza muda na skendo za wasanii. Au unakuta mtu ameajiriwa au amejiajiri miaka inaenda hajui kwa nini hapigi hatua kipato hakikui lakini yupo tu hatafuti maarifa ya jinsi gani ya kutumia muda wake wa ziada kutengeneza kipato hata mara mbili ya mshahara wake. Wengine wanafanya hivyo na wanapiga hatua kubwa hadi wengine wanafikiria sasa kuachana na ajira. Ni muhimu kujifunza haya mambo. Siasa hazitaisha. Angalia your life. Ukifika 40 years uwe very established. Bila hivyo utashangaa kweli. Wakati wenzako wachache wa rika lako mtakapofika miaka 40 wakati wenzako unasikia amenunua kiwanja Kurasini kwa *sh Bilioni mbili kwa ajili ya kupaki* tu Masemitrela zake k**a 20 hivi wewe wakati huo unashangaa K**a Kurasini kumbe kuna viwanja? Wakati huo wewe unamiliki kigari cha mkopo unakipaki uwanja wa CCM unalipia sh 1000/- tu, *mnaita buku*. Fikiria vitu k**a hivi. Utajua vizuri umuhimu wa kutumia muda wako vizuri. Ilikuwa *January* sasa *March* hii. Mwaka unayoyoma. Wewe mwaka huu nini kipya hasa umefanya kimaendeleo. Kupost kuhusu *Lipumba*? Au Nani mkal kati ya Kiba na Diamond?*

*Life begins at 40 my friend.... How Old are you now?*

You can change your life even now!

08/03/2017


Je! Ukipoteza kibarua chako Leo,Utaweza ku-survive kwa muda gani bila ajira???
- Wiki 12?
- Wiki 52?
Je! Umetafuta kaz kwa muda gan baada kumaliza chuo na bado unasuffer?
Umeshajiandalia PLAN 'B' yako?

Personally napenda kutengeneza marafiki wapya wenye malengo makubwa kila siku.
K**a wewe pia unapenda kutengeneza marafiki wapya wenye malengo na kushirikishana mbinu za mafanikio kwenye maisha na ukiwa na SIFA hizi hapo chini...

Focused, Driven, Ambitious,Committed.....then tuwasiliane,tuwe friends na tujadili na kushirikishana PLAN B zenye tija.

SMS/WhatsApp +255 719634757
: Only for serious people!!!!


Address

Gongo La Mboto
Dar Es Salaam

Telephone

0719634757

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Business And Employment Motives posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share