16/01/2026
NENO LA SIKU.
Na, Mtume na Nabii Josephat Elias Mwingira – Kanisa la Efatha.
TAREHE 16/01/2026.
SOMO: KUNA MAJARIBU.
Yakobo 1:14 “Lakini kila mmoja hujaribiwa na tamaa yake mwenyewe huku akivutwa na kudanganywa.”
Yesu wakati anajaribiwa hakutenda dhambi, alishinda jaribu mbele yetu ili nasi tumfuate na tuweze kupata ushindi wa kila siku.
Sote tunajaribiwa na adui huwa anatupitia katika madhaifu yetu. Maeneo tuliyo dhaifu ndiyo shabaha lake!
Ni muhimu kufahamu kuwa majaribu yenyewe si dhambi. Dhambi inaanza pale tunapoanza kuyatenda majaribu au kuyapokea mawazo mabaya katika maisha yetu. Mawazo mabaya yanapokujia, fahamu kwamba wazo hilo halitokani na wewe, bali linatoka kwa adui anayekuletea jaribu, akitegemea utalipokea.
Katika wakati huu, unatakiwa kufanya uamuzi wa kuyakataa majaribu katika Jina la YESU. Unapofanya hivyo, Roho Mtakatifu huja kukusaidia, hukupa nguvu na hekima ya kumpambanua adui.
Yakobo 4:7 “Basi mtiini Mungu. Mpingeni Shetani, naye atawakimbia.”