Bwabuke Tulia Mwansasu

Bwabuke Tulia Mwansasu ☀️Jipatie nguo za k**e 👗👗na Za kiume👔👔 Kwa bei nzuri
☀️Tunapatikana Kariakoo
0747360347

16/01/2026

NENO LA SIKU.

Na, Mtume na Nabii Josephat Elias Mwingira – Kanisa la Efatha.

TAREHE 16/01/2026.

SOMO: KUNA MAJARIBU.

Yakobo 1:14 “Lakini kila mmoja hujaribiwa na tamaa yake mwenyewe huku akivutwa na kudanganywa.”

Yesu wakati anajaribiwa hakutenda dhambi, alishinda jaribu mbele yetu ili nasi tumfuate na tuweze kupata ushindi wa kila siku.
Sote tunajaribiwa na adui huwa anatupitia katika madhaifu yetu. Maeneo tuliyo dhaifu ndiyo shabaha lake!

Ni muhimu kufahamu kuwa majaribu yenyewe si dhambi. Dhambi inaanza pale tunapoanza kuyatenda majaribu au kuyapokea mawazo mabaya katika maisha yetu. Mawazo mabaya yanapokujia, fahamu kwamba wazo hilo halitokani na wewe, bali linatoka kwa adui anayekuletea jaribu, akitegemea utalipokea.

Katika wakati huu, unatakiwa kufanya uamuzi wa kuyakataa majaribu katika Jina la YESU. Unapofanya hivyo, Roho Mtakatifu huja kukusaidia, hukupa nguvu na hekima ya kumpambanua adui.

Yakobo 4:7 “Basi mtiini Mungu. Mpingeni Shetani, naye atawakimbia.”

16/01/2026

NAIBARIKI IJUMAA YANGU.

Nafurahi katika BWANA, maana amenipa KUSHINDA.

Haleluya, YESU ni Mzuri sana.

15/01/2026

NAIBARIKI ALHAMISI YANGU.

BABA yangu wa Mbinguni ni Mpaji wangu; Mimi sitapungukiwa na Kitu. Upendo, Kicheko, Furaha, Karamu, Utele, Chakula vitakuwa pamoja nami.

Haleluya, YESU ni Mzuri.

02/10/2025
02/08/2025

NENO LA SIKU

Na Mtume na Nabii Josephat Elias Mwingira, Kanisa la Efatha

Tarehe 2/8/2025

SOMO: JIFUNZE KUONGEZA KABLA HAUJATOA ILI UWEZE KUFIKIA UKUU WAKO

Pesa haiwezi kukaa mfukoni mwako k**a haijaweza kukaa katika akili yako. Lazima ujue hesabu, siku utakapojua kuongeza kabla haujatumia utakuwa tajiri.
K**a Akili yako ni masikini hata ukipewa milioni kumi utapoteza zote, hivyo hakikisha Akili yako inakuwa tajiri kwanza. Akili ya kimasikini ikoje? Ni ile ya kuwaza kuwa unaweza kutajirika kwa kudhulumu mali ya mwenzako.

Umasikini ni nini? Mara zote walaji ni masikini, huwezi kuwa tajiri k**a wewe ni mlaji. Nikikupa milioni moja kabla haujaitumia hakikisha unaizalisha kwanza, lakini ukianza kuitumia kabla haujajua ni jinsi gani utaizalisha wewe ni mlaji na kila mara utakuwa unafilisika na kuanza upya. Mara zote mwenye harufu ya utajiri ana akili ya kuzidisha na sio kutoa, ukimpa kitu kinaongezeka na sio kupungua.

Wewe hauna pesa kwa sababu AKILI, MOYO na KINYWA chako hakijakubali kwamba unaweza kupata pesa. Unapoamini kwa Moyo, Akili yako ikaelewa na Kinywa chako kikanena sauti yako inakuwa sauti ya Mungu na kila ulitendalo linafanikiwa.

19/07/2025

NENO LA SIKU.

Na Mtume na Nabii Josephat Elias Mwingira - Kanisa la Efatha.

Tarehe 19/7/2025.

SOMO: IBADA.

Yohana 4:23 “Lakini saa inakuja, nayo sasa ipo, ambayo waabuduo halisi watamwabudu Baba katika Roho na kweli. Kwa maana Baba awatafuta watu k**a hao wamwabudu.”

Biblia inasema Mungu anawatafuta waabuduo na akiwapata anawaleta ili wamwabudu, watu wengine wanataka sana kuabudu lakini hawawezi, kwa nini? Kwa sababu hawajakubaliwa kuabudu.

Ibada ni mapenzi ya Mungu, ukiwa nje ya mapenzi ya Mungu hauwezi kuabudu ukipata neema ya kuabudu mshukuru sana Mungu wako kwa maana upo ndani ya mapenzi yake. Watu walio nje ya mapenzi ya Mungu hawaabudu na ndiyo maana unaweza kuona siku ya ibada (Jumapili) wengine wamelala, wengine wako mahali pao pa kazi, wengine kwenye vikao au kwenye shughuli zao; kwa nini? Kwa sababu hawajakubaliwa kuabudu. Unapoamka siku na ukasema unakwenda Kanisani inamaana kuwa umeamriwa hiyo siku kuabudu.

Kuabudu siyo mapenzi yako bali ni mapenzi Yake, ni Yeye ndiye anayewatafuta waabuduo na sio wewe unamtafuta Yeye, hii ndiyo maana kuna wengine wanaabudu mizimu, wengine wanaabudu biashara au kazi zao, utajuaje? Wanajua kuwa Jumapili ni siku ya ibada lakini ndiyo wanapanga vikao au wanakwenda kwenye kazi zao, kwa nini? Kwa sababu Mungu amewazuilia kuabudu kwa sababau mikutano au kazi zao ndiyo ibada zao; lakini kwa wewe ambaye umekubaliwa kuabudu hakikisha unakwenda mbele za Mungu na umwabudu Yeye kwa sababu umekubaliwa.

Kesho ni siku ya ibada (Jumapili) mwanangu jiandae vyema kwa ajili ya ibada, Mungu ameandaa jambo jipya kwa ajili yako na anasubiri uende mbele zake ili ukalipokee; acha likawe la kwako na asiwepo wa kukunyang'anya.

23/06/2025

NENO LA SIKU

Na Mtume na Nabii Josephat Elias Mwingira, Kanisa la Efatha

Tarehe 23/6/2025

SOMO: NENO LA MAARIFA

Kutoka 31:3-4 "nami nimemjaza roho ya Mungu, katika hekima, na maarifa, na ujuzi, na mambo ya kazi ya kila aina, ili abuni kazi za ustadi, kuwa fundi wa dhahabu, na wa fedha, na wa shaba"

Neno la Maarifa litakupa nini katika maisha yako?
● Hukuwezesha kufahamu kinachoendelea Duniani na jinsi ya kufanya kazi ili upate Mali.
● Hukusaidia kuwa Mvumbuzi na Mbunifu ili ufanye mambo yenye ubora na yatakayokuwezesha kufanikiwa.
● Utapanda daraja na kuwa Mtu Mkuu kwa sababu ni Mtendaji mzuri.
● Litakupa kujitegemea kwa kuwa kile unachokifanya kitakupa fedha na hautakuwa maskini wala omba omba. Hali hii itakufanya usiwe mkia bali utakuwa Kichwa wakati wote. Ukiwa mvivu hauwezi kumiliki kitu kwa sababu uvivu hukaa akilini na haikuwezeshi kuwaza mambo makubwa.

Kila wakati omba Roho wa Maarifa afungue macho yako ili ujue chakufanya na kuwa k**a Mungu alivyokukusudia. Ukijifunza na kutafakari Biblia na mafundisho unayofundishwa itakufanya uendelee mbele lakini usipofanya hivyo utarudi nyuma.

TANGAZO
Nakuamuru uwe na Maarifa ili uweze kupata Mali; kwa Jina la Yesu.

11/06/2025

NAIBARIKI JUMATANO YANGU.

Maana Mimi ni MBARIKIWA; Nitamiliki vilivyo vya BWANA, Nitamiliki, na wote watajua, kwamba MIMI NIMEBARIKIWA na BWANA.

Haleluya, YESU ni Mzuri.

27/05/2025

NAIBARIKI JUMANNE YANGU.

Jumanne yangu IMEBARIKIWA na BWANA; Mke wangu Mzuri (Mume wangu Mzuri), Watoto wazuri, Familia yangu nzuri, Wote TUMEBARIKIWA na BWANA, kwetu ni KWEMA.

Haleluya , YESU ni Mzuri.

26/05/2025

NENO LA SIKU.

Na, Mtume na Nabii Josephat Elias Mwingira- Kanisa la Efatha.

TAREHE: 26/05/2025.

SOMO: ANGALIA NAMNA YA KUONGEA KWAKO.

Lugha inaweza kubadilisha hali ya hewa katika ndoa yako, jinsi unavyoongea na mume wako au mke wako inaweza kusababisha Mungu akawanyima mnachoomba, lakini lugha zenu zikiwa pamoja mtashinda katika yote.

Lugha unayotumia inafungua mlango wa Mungu kushughulika na wewe au shetani. Namna unavyoishi January mpaka December inafungua au kufunga mlango wa kushinda au kushindwa kwako, hivyo kila siku uwe makini sana namna unavyoongea na kutenda, uwe na maneno Machache ili uweze kumshinda shetani.

Address

Dar Es Salaam
Dar Es Salaam

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Bwabuke Tulia Mwansasu posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share