12/12/2025
KUTOKA KWA JONGWE AKA SUGU ;
SAKATA LA WASANII NA WANANCHI AMJIBU MAJIZO.
Mkongwe wa Hip Hop na Mwanasiasa, Joseph Mbilinyi ‘Sugu’, amemtolea uvivu Mkurugenzi wa EFM, Majizzo, akimuonya dhidi ya kutetea wasanii wanaolalamikiwa na wananchi kwa kukosa uzalendo.
Katika ujumbe mzito, Sugu amemkumbusha Majizzo historia yao, akifichua kuwa ndiye aliyempa gari yake ya kwanza mwaka 2003, hivyo anajua anavyouthamini muziki. Hata hivyo, amemwambia “kwa hili ni UDWANZI” kuwatetea wasanii walioitumia sanaa kuumiza, kudharau na kuwakosea heshima Watanzania waliowainua.
Sugu amesisitiza kuwa mgomo baridi wa sasa dhidi ya wasanii hao sio siasa, bali ni hasira ya umma kutokana na usaliti. Sugu akihitimisha kwa msimamo mkali akisema “Niko upande wa Watanzania,”