Am .Kiswahili Tanzania

Am .Kiswahili Tanzania A.M. kiswahili tanzania. facebook.com/amkiswahilitanzania

TV | To The World
📍 Habari na Matukio Ulimwenguni.
🎥 Tunakuletea ukweli wa mambo popote ulipo.
✨ Habari | Elimu | Burudani
👉 Gusa Follow uwe wa kwanza kujua!

21/03/2026

Unamshauri nini huyu deleva

Huyu mubaba  kazi yake ni kuendesha boda-boda hapa mtaani kwetu Mimi natokea Nairobi. Alikuwa mtu wa kawaida tu, anatafu...
19/03/2026

Huyu mubaba kazi yake ni kuendesha boda-boda hapa mtaani kwetu Mimi natokea Nairobi. Alikuwa mtu wa kawaida tu, anatafuta maisha yake ya kila siku. Sasa siku moja, k**a ilivyo kawaida, alimpakia abiria — ambaye Alikuwa ni mwanafunzi wa shule. Akampeleka mpaka shule salama kabisa.

Lakini hapo ndipo mambo yalianza kubadilika kidogo kidogo.

Yule mwanafunzi akaanza kumzoea. Kila siku akimkuta, anapewa lifti bure. Mara nyingine anapewa hata hela ya kununua chakula. Mwanzoni ilionekana k**a msaada tu wa kawaida, mtu mzima kumjali mtoto. Lakini yule mbaba moyoni alikuwa na nia nyingine kabisa.

Siku moja akamwambia yule mtoto, “Leo twende sehemu nzuri, tukale vizuri.” Yule mwanafunzi, kwa sababu bado mdogo na hajui mengi, akakubali. Wakenda kwenye gesti. Wakakaa, wakala, wakanywa soda, maisha yakawa laini. Yule mtoto akaanza kunogewa na ile hali.

Kuanzia hapo, mambo yakaharibika kabisa.

Yule mwanafunzi akaanza kuacha shule taratibu. Asubuhi anavaa nguo za shule, anajifanya anaenda shule, lakini anaishia gesti kwa yule mbaba. Wiki ikapita nzima hajakanyaga shule.

Sasa kuna mwalimu mmoja, siku moja Alikuwa na yeye ameenda gesti kufanya yake kwenye ile gesti Alikuwa na gari yake. Kwa macho ya haraka haraka, akahisi k**a amemwona mwanafunzi wake akiingia pale. Hakuchukulia poa. Akaamua kuchunguza kimya kimya.

Kesho yake akaenda shule, akapiga hesabu ya wanafunzi — kumbe yule mtoto hayupo kabisa siku kadhaa. Akaenda kwa wazazi wake kuwauliza, nao wakasema, “Kila siku anaenda shule.” Hapo mwalimu akajua kuna kitu hakipo sawa.

Basi akaamua kufuatilia mpaka mwisho.

Siku moja akaenda moja kwa moja kwenye ile gesti. Akaingia ghafla. Alipofika ndani, akamkuta yule mwanafunzi yupo pamoja na yule mbaba wa boda-boda.

Hasira zikampanda mwalimu.

Akamwambia yule jamaa, “Hii haiwezekani! Unaishi na mwanafunzi? Hii ni kosa kubwa. Nitaita polisi sasa hivi!”

Yule mbaba akaanza kutetemeka. Akajua kabisa hapa mambo yameharibika. Akaanza kuomba msamaha, “Nisamehe, ukinipeleka polisi nitafungwa miaka mingi…”

Mwalimu akamwangalia kwa ukali, kisha akasema, “Sikukupeleka kwa wazazi, wala sijaita polisi bado. Lakini nataka haki ifanyike. Huyu mtoto mwenyewe lazima akushtaki. Asipofanya hivyo, mimi nitakushtaki mwenyewe.”

Basi yule mwanafunzi, akaambia akawaambia wazazi wake kilichomkuta

Lakini cha ajabu…

Baada ya tukio hilo, yule mwanafunzi akatoweka ghafla. Mpaka leo hajulikani alipo. Wazazi wakaanza wasiwasi, watu wakaanza kujiuliza, “Ameenda wapi?”

Sasa na yule mubaba mwenyewe kakimbia afu na yule mwalimu hajamwambia mtu Siri imebaki ya watu watatu tu

 : Serikali ya Senegal imetoa msimamo mkali sakata linalohusu Kombe la Africa Cup of Nations (AFCON), ikitangaza kuwa ha...
19/03/2026

: Serikali ya Senegal imetoa msimamo mkali sakata linalohusu Kombe la Africa Cup of Nations (AFCON), ikitangaza kuwa haitalirejesha kombe hilo kwa sasa hadi pale Court of Arbitration for Sport (CAS) itakapotoa uamuzi wake rasmi.

Hatua hiyo imekuja muda mfupi baada ya Rais wa Senegal, Bassirou Diomaye Faye, kubadilisha picha yake ya wasifu kwenye mitandao ya kijamii, kitendo hicho kimetafsiriwa na wengi k**a ujumbe wa kisiasa na kimkakati unaoashiria msimamo wa taifa hilo.

Kwa mujibu wa taarifa zilizosambaa, Senegal tayari imelijulisha Confederation of African Football (CAF) kuwa haitarejesha kombe hilo hadi mchakato wa kisheria utakapokamilika, kwa kawaida mabingwa hutakiwa kulirejesha kombe kabla ya mashindano yanayofuata ili maandalizi ya toleo jipya yaanze.

Uamuzi huo unatazamwa k**a hatua ya ujasiri inayochanganya siasa, sheria na michezo, huku wachambuzi wanasema hatua ya kuhusisha CAS inaonesha kuwa Senegal inataka suala hilo litazamwe katika misingi ya kisheria badala ya kiutawala pekee.

Hadi sasa, CAF haijatoa tamko rasmi kuhusu hatua zinazoweza kuchukuliwa iwapo kombe hilo halitarejeshwa kwa kombe hili

USHIRIKINA NI UTAPELI UNAOWEKA MAKAO KWA MTU ALIYEKUBALI KUWA MJINGA. UKEMEWE NA UKATALIWE. Hivi waamini ushirikina nawa...
18/03/2026

USHIRIKINA NI UTAPELI UNAOWEKA MAKAO KWA MTU ALIYEKUBALI KUWA MJINGA. UKEMEWE NA UKATALIWE.

Hivi waamini ushirikina nawauliza, nani aliwaambia huwa unasaidia kwenye lolote la mafanikio? Mbona wengine tangu tuzaliwe hatujawahi kuutegemea wala kuufikiria wala kuuamini wala kuwaza tu kuutumia k**a nyenzo ya mafanikio na tunafanikiwa kwa bidii ya kazi za mikono yetu ?

Mbona wategemea ushirikina kila leo mnaishia kufanya uhalifu na kuk**atwa na kufungwa bila msaada wa hao waganga wenu matapeli wakubwa. Hivi mtafunguka lini hizo akili zenu 🧠 mvue koti la ujinga muwe wajanja mtambue kuwa, hao wanaojiita wataalamu wa ushirikina wa ili ufanikiwe hawana lolote ni matapeli k**a matapeli wengine wowote ambao wamepima akili zako wakaona wanazimudu yaani huelewi elewi msingi wa mafanikio na wewe umekubali a.k.a wamekuona mjinga.

Ujumbe; enyi Waamini Ushirikina badilikeni ama mtaishia jela kila siku huku waliowadanganya wakifaidi maisha kwa kuwatapeli.

Kasome zaidi kisa cha huyu kwenye picha.

kikundi cha mila na tamaduni hasi mhusike hapa kwenda kuelimisha jamii jinsi gani inatapeliwa na wajanja kwa wao kufanywa wajinga.

MWISHO; Tafsiri ya Mjinga ni nani? Mjinga ni neno la Kiswahili lenye maana ya mpumbavu, mtu asiye na ufahamu, au anayefanya maamuzi yasiyo na hekima. Mara nyingi hutumika kuelezea mtu anayekosa akili ya mambo au anayefanya makosa ya kijinga. Katika muktadha wa kijamii, inaweza kumaanisha mtu anayedanganyika kirahisi au asiyejifunza kutokana na makosa.

TUBADILIKE, UJINGA SIYO GONJWA DUGU, UNAWEZA KUWA MJANJA.

18/03/2026

Wasiliana na polisi mara moja – uwepo wao husaidia kudhibiti watu na kulinda mali.
Linda eneo la ajali – tumia triangle/reflection signs kuzuia watu wasikaribie ovyo.
Usiache gari bila ulinzi – dereva au msaidizi abaki karibu na mzigo.
2. Ulinzi wa mzigo
Tumia seal (muhuri) za kontena – zikivunjwa inajulikana mara moja.
Lock imara kwenye milango ya lori.
Tracking system (GPS) – kufuatilia gari na kujua lilipo muda wote.
3. Kuwa na walinzi au usimamizi
Kwa mizigo ya thamani kubwa, weka mlinzi (security es**rt) hasa kwenye safari ndefu.
Kampuni iwe na team ya dharura ya kufika haraka eneo la ajali.
4. Ushirikiano na jamii
Waombe watu wa karibu kusaidia lakini kwa usimamizi wa polisi.
Epuka vurugu kwa kuzungumza vizuri na watu waliokusanyika.
5. Mafunzo kwa madereva
Madereva wafundishwe:
Jinsi ya kushughulikia ajali
Namna ya kulinda mzigo
Kuwasiliana haraka na mamlaka
6. Bima (Insurance)
Hakikisha gari na mzigo una insurance ya kutosha ili kupunguza hasara ikitokea wizi.
7. Teknolojia za ziada
Dash cams na cameras za nje
Alarm systems zinazolia gari likifunguliwa vibaya

18/03/2026
18/03/2026

Wasiliana na polisi mara moja – uwepo wao husaidia kudhibiti watu na kulinda mali.
Linda eneo la ajali – tumia triangle/reflection signs kuzuia watu wasikaribie ovyo.
Usiache gari bila ulinzi – dereva au msaidizi abaki karibu na mzigo.
2. Ulinzi wa mzigo
Tumia seal (muhuri) za kontena – zikivunjwa inajulikana mara moja.
Lock imara kwenye milango ya lori.
Tracking system (GPS) – kufuatilia gari na kujua lilipo muda wote.
3. Kuwa na walinzi au usimamizi
Kwa mizigo ya thamani kubwa, weka mlinzi (security es**rt) hasa kwenye safari ndefu.
Kampuni iwe na team ya dharura ya kufika haraka eneo la ajali.
4. Ushirikiano na jamii
Waombe watu wa karibu kusaidia lakini kwa usimamizi wa polisi.
Epuka vurugu kwa kuzungumza vizuri na watu waliokusanyika.
5. Mafunzo kwa madereva
Madereva wafundishwe:
Jinsi ya kushughulikia ajali
Namna ya kulinda mzigo
Kuwasiliana haraka na mamlaka
6. Bima (Insurance)
Hakikisha gari na mzigo una insurance ya kutosha ili kupunguza hasara ikitokea wizi.
7. Teknolojia za ziada
Dash cams na cameras za nje
Alarm systems zinazolia gari likifunguliwa vibaya

18/03/2026

.AM KISWAHILI.TANZANIA.Bodi ya Rufaa ya Shirikisho la Soka Afrika (CAF) Machi 17, 2026 imetoa uamuzi mzito kwa kuinyang’anya Senegal ubingwa wa Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON) 2025.

Kwa mujibu wa Kifungu cha 84 cha kanuni za mashindano hayo, CAF imetangaza kuwa timu ya taifa ya Senegal imepoteza rasmi mchezo wa fainali dhidi ya Morocco kwa kufungwa mabao 3-0 kwa njia ya mezani.

Kutokana na uamuzi huo, Senegal imelazimika kurejesha kombe la AFCON 2025 pamoja na medali walizokuwa wamekabidhiwa hapo awali. Kombe hilo sasa litakabidhiwa rasmi kwa Shirikisho la Soka la Morocco (FRMF), ambao wametangazwa mabingwa wapya wa mashindano hayo.

Uamuzi huo umeibua mjadala mkubwa miongoni mwa wadau wa soka barani Afrika, huku wengi wakisubiri ufafanuzi zaidi juu ya sababu zilizopelekea hatua hiyo kali kuchukuliwa dhidi ya Senegal.

CAF inatarajiwa kutoa taarifa ya kina zaidi kuelezea tukio hilo, huku mashabiki na wachambuzi wa soka wakifuatilia kwa karibu maendeleo ya sakata hili kubwa katika soka la Afrika.

Life🤑🤑
31/01/2024

Life🤑🤑

Address

Dar Es Salaam

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Am .Kiswahili Tanzania posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share