29/03/2025
Asante kushukuru ๐๐
SHUKRANI ZA KAMATI YA TUZO YA USHAIRI CHAGUO LA WASOMAJI (TUCHAWA)
Kamati ya Tuzo ya Ushairi Chaguo la Wasomaji (TUCHAWA) inatoa shukrani za dhati kwa mahudhurio ya tukio la kilele cha Tuzo ya Ushairi Chaguo la Wasomaji 2024-2025, lililofanyika katika Ukumbi wa Ngome Holding Hall, Sinza โ Afrika Sana, Dar es Salaam, Tanzania, siku ya Ushairi Duniani, tarehe 21 Machi 2025.
Tunamshukuru sana Mgeni Rasmi, Mheshimiwa Nyambari Nyangwine, Mwenyekiti wa Makampuni ya Nyambari Nyangwine, kwa heshima kubwa aliyotupa ya kushiriki nasi na kupendezesha shughuli yetu kwa namna ya kipekee.
Shukrani za pekee pia kwa viongozi na wawakilishi kutoka taasisi mbalimbali ambao waliheshimu mwaliko wetu na kushiriki nasi:
BASATA
BAKITA
BAKIZA
CHAKUWAZA
WAKITA
UKUTA
UBALOZI WA INDIA
TPAKI
Tunawashukuru pia wadau wa vyombo vya habari waliotufanikishia kufikisha sauti ya ushairi kwa jamii:
TBC
Radio One
UFM
EATV
Tungo Tata TV
Mdundo FM
Top Plus TV
Shukrani za dhati pia ziwafikie wadhamini wetu waliotuunga mkono na kuhakikisha mafanikio ya hafla hii:
Nyambari Nyangwine Group of Companies
Mtalimbo Books
Marmโz Relationship Hub
Kuabedgo Events
Indomie
Kalamu Tulivu
Adroit Decor
Jawa Graphic Services
Sales Malula G.E
Jike la Simba FPP
Mpakani Tunaweza Organization
Hatutasahau mchango mkubwa wa washairi wetu, wageni waalikwa kutoka tasnia za habari, filamu, ucheshi, na muziki ambao walifanya tukio hili kuwa la kipekee.
Mwisho, tunawashukuru wageni wote waalikwa kwa kujumuika nasi. Hakika, mmeuinua na kuheshimisha Ushairi wa Afrika Mashariki!
Asanteni Sana!
Sheikh Hussein Kondo Abdallah
Katibu wa TUCHAWA