11/06/2026
Serikali imepanga kuondoa matumizi ya vocha za simu za kukwangua kwa mkono katika maeneo yote ya mijini kuanzia mwaka wa fedha 2026/27, ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuhamasisha matumizi ya mifumo ya kidijitali nchini.
Akiwasilisha Bungeni Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa mwaka wa fedha 2026/27, Waziri wa Fedha, Balozi Khamis M***a Omar, amesema utekelezaji wa hatua hiyo utaanza katika maeneo ya mijini ili kutoa fursa ya kujifunza kabla ya kuipanua katika maeneo mengine ya nchi.
Aidha, Serikali kwa kushirikiana na wadau wa sekta ya fedha itaendelea kuimarisha miundombinu ya malipo ya kidijitali kwa kuongeza kasi ya utoaji wa huduma k**a LIPA NAMBA na QR Code kwa wafanyabiashara wadogo wakiwemo bodaboda, mama na baba lishe pamoja na wafanyabiashara wa masoko ya wazi.
Waziri huyo amesema wafanyabiashara watakaotumia njia za kidijitali kupokea malipo watapata sifa za ziada wakati wa kuomba mikopo kutoka serikalini na taasisi za fedha.
Katika hatua nyingine, Serikali imetangaza kuwa kuanzia Julai 1, 2026 uthibitisho wa malipo ya kidijitali utakuwa sharti la lazima katika kuidhinisha maombi ya uhamishaji wa mali mbalimbali ikiwemo ardhi, majengo na magari.
Hatua hiyo itazihusisha taasisi zote za umma zikiwemo Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, BRELA na taasisi nyingine zinazohusika na usajili na uhamishaji wa mali.