Koncept TV

Koncept TV Koncept TV is Africa's boldest voice in news, business & culture, Sports,Wildlife,Tech— 24/7 📞 Contact: +255 658 123 310

Pata Habari za Hivi Punde/Kitaifa/Kimataifa/Biashara na Uchumi/Siasa, Michezo/Burudani/Teknolojia na Hamasa


LIKE PAGE Kisha Tembelea Website Yetu Kupata UHONDO Zaidi

13/06/2026
KOMBE LA DUNIAfT’ Mexico 🇲🇽 2-0 Afrika Kusini   🇿🇦⚽  Julián Quiñones⚽ Raúl Jiménez                #ᴛʀᴇɴᴅɪɴɢɴᴏᴡ
11/06/2026

KOMBE LA DUNIA

fT’ Mexico 🇲🇽 2-0 Afrika Kusini 🇿🇦
⚽ Julián Quiñones
⚽ Raúl Jiménez

#ᴛʀᴇɴᴅɪɴɢɴᴏᴡ

Waziri wa Fedha, Balozi Khamisi M***a Omar, amesema Serikali inapendekeza maboresho kwenye Sheria ya Fedha za Serikali z...
11/06/2026

Waziri wa Fedha, Balozi Khamisi M***a Omar, amesema Serikali inapendekeza maboresho kwenye Sheria ya Fedha za Serikali za Mitaa, Sura 290, ili kuwezesha Mamlaka za Serikali za Mitaa kutenga asilimia 15 ya mapato yao ya ndani badala ya asilimia 10 iliyopo sasa ya mikopo ya wanawake, Vijana na Watu Wenye Ulemavu.

Akiwasilisha Bungeni mapendekezo ya Serikali kuhusu makadirio ya mapato na matumizi kwa mwaka 2026/2027, Waziri Khamis amesema

“kati ya asilimia 15 itakayotengwa, asilimia 10 itaelekezwa kwenye mikopo ya Wanawake, Vijana na Wenye Ulemavu kwa uwiano k**a ilivyokuwa awali na asilimia tano (5) itatumika kwa ajili ya uwekezaji kwenye miradi ya ujenzi na maboresho ya Masoko na maeneo ya biashara na ujasiriamali ili kuvutia na kuongeza fursa za ajira hususan kwa Vijana, Wanawake na makundi maalum”

Serikali imepanga kuondoa matumizi ya vocha za simu za kukwangua kwa mkono katika maeneo yote ya mijini kuanzia mwaka wa...
11/06/2026

Serikali imepanga kuondoa matumizi ya vocha za simu za kukwangua kwa mkono katika maeneo yote ya mijini kuanzia mwaka wa fedha 2026/27, ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuhamasisha matumizi ya mifumo ya kidijitali nchini.

Akiwasilisha Bungeni Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa mwaka wa fedha 2026/27, Waziri wa Fedha, Balozi Khamis M***a Omar, amesema utekelezaji wa hatua hiyo utaanza katika maeneo ya mijini ili kutoa fursa ya kujifunza kabla ya kuipanua katika maeneo mengine ya nchi.

Aidha, Serikali kwa kushirikiana na wadau wa sekta ya fedha itaendelea kuimarisha miundombinu ya malipo ya kidijitali kwa kuongeza kasi ya utoaji wa huduma k**a LIPA NAMBA na QR Code kwa wafanyabiashara wadogo wakiwemo bodaboda, mama na baba lishe pamoja na wafanyabiashara wa masoko ya wazi.

Waziri huyo amesema wafanyabiashara watakaotumia njia za kidijitali kupokea malipo watapata sifa za ziada wakati wa kuomba mikopo kutoka serikalini na taasisi za fedha.

Katika hatua nyingine, Serikali imetangaza kuwa kuanzia Julai 1, 2026 uthibitisho wa malipo ya kidijitali utakuwa sharti la lazima katika kuidhinisha maombi ya uhamishaji wa mali mbalimbali ikiwemo ardhi, majengo na magari.

Hatua hiyo itazihusisha taasisi zote za umma zikiwemo Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, BRELA na taasisi nyingine zinazohusika na usajili na uhamishaji wa mali.

Waziri wa Fedha, Balozi Khamis M***a Omar, amesema hadi Machi 2026 deni la Serikali lilifikia shilingi trilioni 114.34, ...
11/06/2026

Waziri wa Fedha, Balozi Khamis M***a Omar, amesema hadi Machi 2026 deni la Serikali lilifikia shilingi trilioni 114.34, ambapo shilingi trilioni 38.45 ni deni la ndani na shilingi trilioni 75.89 ni deni la nje.

Akiwasilisha Bungeni Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa mwaka wa fedha 2026/27, Waziri huyo amesema deni hilo limetokana na mikopo iliyochukuliwa kwa ajili ya kugharamia miradi ya kimkakati inayochochea ukuaji wa uchumi, ikiwemo miundombinu ya usafirishaji, nishati na mawasiliano.

Aidha, amesema hadi Aprili 2026 Serikali ilikuwa imekopa jumla ya shilingi trilioni 11.29 kutoka soko la ndani na nje, sawa na asilimia 89.5 ya lengo lililowekwa.

Kati ya kiasi hicho, shilingi trilioni 5.08 zilikopwa ndani ya nchi ambapo trilioni 2.55 zilitumika kulipa hati fungani zilizoiva na trilioni 2.53 kuelekezwa kwenye miradi ya maendeleo.

Kwa upande wa mikopo ya nje, Serikali ilikopa shilingi trilioni 6.20, zikiwemo trilioni 4.61 za mikopo nafuu na trilioni 1.59 za mikopo yenye masharti ya kibiashara.

Address

Mikocheni B, Malezi Bora , House No 30,Cocacola Road
Dar Es Salaam
00255

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Koncept TV posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share