07/10/2024
JINSI YA KUJUA FAIDA NA HASARA KATIKA BIASHARA
1. Orodhesha gharama za manunuzi ya mzigo
2. Orodhesha gharama za kufikisha mzigo ofsini kwako (K**a nauli,usafiri, uchukuzi, ushuru nk)
3. Orodhesha mauzo ya siku kwa kila bidhaa/huduma
4. Funga hesabu ujue mauzo ya siku/wiki/mwezi/mwaka
5. Toa gharama zote pamoja za ununuzi wa bidhaa(Kodi,chakula,maji,umeme nk)
6. Kinachobakia ndio faida yako
7. Unaweza kutumia electronic systems za kukokotoa
NB:
Usitumie mauzo katika biashara bali tumia faida, kwasababu katika mauzo ya 200,000/= ukikokotoa vizuri utakuta faida yako ni 20,000/= na wewe umetumia 50,000/=
Kwamaana hiyo utakua umepunguza mtaji 30,000/=
Baada ya muda fulani utaona biashara inaporomoka na huo ndio mwanzo wa kufa kwa biashara
Tuambie wewe unatumia njia gani kujua faida na hasara kwenye biashara zako?...Comment