14/02/2021
Kwa sababu ya kukosa elimu ya masuala ya kifedha, ndoa nyingi na familia nyingi sana zimeishia katika maisha ya kimaskini, ugomvi wa kifamilia na kupoteza upendo kati ya wanandoa.
Kwa mujibu wa taasisi ya SunTrust, changamoto za kifedha ndizo zinazoongoza kuleta migogoro ya kifedha katika familia kwa sasa.
Uchunguzi uliofanywa na Institute for Divorce Financial Analysis umeonyesha kuwa 22% ya wanandoa wanaoachana sababu kubwa ni masuala ya mambo ya pesa.
Bila kujali umri wa wanandoa husika, pesa huwa ina nafasi kubwa sana katika mahusiano ya wanandoa.
Ili kuondoa changamoto za kifedha katika ndoa yenu, ni lazima mfanye juhudi za makusudi zitakazoshughulikia vyanzo vya matatizo ambavyo tumevizungumza kwenye sura ya tatu.
Jambo la muhimu la kulielewa hapa, ni kuhakikisha kuwa kila mmoja wenu anahusika kwa 100% na anakuwa tayari kubadilisha hali ambayo hamuipendi
kwa sasa.
Mbinu ya kwanza: Kukubaliana Falsafa Yenu Ya Pesa.
K**a tulivyoona hapo mwanzoni kuwa, falsafa yenu kuhusu pesa huwa ni muhimu sana katika mafanikio yenu.
Kujua falsa yako ya fedha na ya mwenza wako ujiulize maswali ya msingi yafuatayo:
• Alilelewa kwenye familia yenye uwezo kiasi gani kipesa?
Aidha zilikuwa zinapatikana sana au hazipatikani, zote kuna mitazamo huwa inajengwa.
• Alikuwa anaambiwa nini kuhusiana na pesa akiwa mdogo?
• Anaamini nini kuhusiana na pesa?
• Alipitia changamoto gani za kifedha ambazo zimempa mtazamo fulani wa pesa?
Baada ya kuzijua falsa zote mbili ya kwako na ya mwenza wako kuna maswali yafuatayo unatakiwa kujiuliza:
i. Kuna tofauti gani kati ya falsafa yangu ya kifedha na ile ya mwenzangu?
ii. Ni maeneo gani makubwa ambayo hasa tunatofautiana mitazamo yetu kuhusu pesa?
iii. Je, tunaweza kufanya nini ili kupata maelewano na kuunganisha falsafa zetu?
Majibu ya maswali haya yatakusaidia kujua maeneo makubwa ambayo hasa mnatofautiana na ambayo mnataka kujenga makubaliano ili muweze kufanikiwa kwa haraka kwenye eneo la pesa.
Itakuwa ni vizuri sana k**a maswali haya mtayajibu kwa pamoja ili kutengeneza mkakati wenye nguvu utakaowasaidia.
Mbinu ya pili: Kuwa na Maono Ya Pamoja Kuhusu Pesa.
Hapa k**a wanandoa mnatakiwa mkae chini na mjiulize, hivi sisi maono yetu kuhusu pesa ni yapi?
K**a utapenda kujifunza kwa kina nashauri ujinyakulie VALENTINE'S DAY eBook Bando kwa Tsh 12,000 Tu! Badala ya Tsh 60,000+
Kupata bando hili
Tuma Tsh 12,000 Tu!
Kwenda M-PESA
0756 094 875 (Ipyana Mwangoka)
Kisha tuma UTHIBITISHO WA MUAMALA WHATSAPP 0756 094 875
NB: NDANI YA MASAA 24 UTATUMIWA eBook Yako.
See You At The Top
Joel Nanauka.
PS. OFA Hii Inaisha Ndani Ya Masaa 72 Tu! (Inaisha Tarehe 17/02/2021) Na Baada ya hapo Bei Itapanda.