26/05/2026
Shirika la RED CROSS limetoa Misaada ya Vitu mbalimbali kwa Wagonjwa waliopo katika Hospitali ya Wilaya ya Magu Katika kuadhimisha Siku ya RED CROSS DUNIANI .
Akiongoza Ujumbe wa Shirika hilo , Mkuu wa Wilaya ya Magu, Mheshimiwa JUBILATE LAWUO, amelipongeza Shirika la Msalaba Mwekundu Wilaya ya Magu mkoani Mwanza kwa jitihada zake za kuendelea kugusa na kusaidia jamii kupitia shughuli mbalimbali za kibinadamu.
Lawuo amesema Red Cross imekuwa mshirika muhimu wa Serikali katika utoaji wa huduma mbalimbali za kijamii, ikiwemo huduma ya kwanza kwenye matukio ya kijamii, makongamano na mbio za Mwenge wa Uhuru.
Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Red Cross Wilaya ya Magu, CHACHA KISUKA, amesema utoaji wa misaada hiyo ni sehemu ya kuonyesha upendo na kusaidia makundi yenye uhitaji katika jamii.
Msaada huo uliojikika kwa kina Mama waliojifungua, kwa kupatiwa Sabuni, pempas kwa ajili ya watoto na vitu vingine muhimu , Baadhi yao wameishukuru Red Cross kwa kuwafariji na kuwathamini katika kipindi hicho muhimu cha uzazi.