NCHI YETU TV

NCHI YETU TV Media

26/05/2026

Shirika la RED CROSS limetoa Misaada ya Vitu mbalimbali kwa Wagonjwa waliopo katika Hospitali ya Wilaya ya Magu Katika kuadhimisha Siku ya RED CROSS DUNIANI .

Akiongoza Ujumbe wa Shirika hilo , Mkuu wa Wilaya ya Magu, Mheshimiwa JUBILATE LAWUO, amelipongeza Shirika la Msalaba Mwekundu Wilaya ya Magu mkoani Mwanza kwa jitihada zake za kuendelea kugusa na kusaidia jamii kupitia shughuli mbalimbali za kibinadamu.

Lawuo amesema Red Cross imekuwa mshirika muhimu wa Serikali katika utoaji wa huduma mbalimbali za kijamii, ikiwemo huduma ya kwanza kwenye matukio ya kijamii, makongamano na mbio za Mwenge wa Uhuru.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Red Cross Wilaya ya Magu, CHACHA KISUKA, amesema utoaji wa misaada hiyo ni sehemu ya kuonyesha upendo na kusaidia makundi yenye uhitaji katika jamii.

Msaada huo uliojikika kwa kina Mama waliojifungua, kwa kupatiwa Sabuni, pempas kwa ajili ya watoto na vitu vingine muhimu , Baadhi yao wameishukuru Red Cross kwa kuwafariji na kuwathamini katika kipindi hicho muhimu cha uzazi.

ARUSHA | Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mhe. CPA Amos Gabriel Makalla amesisitiza umuhimu wa Mataifa ya Afrika kuimarisha usalam...
26/05/2026

ARUSHA | Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mhe. CPA Amos Gabriel Makalla amesisitiza umuhimu wa Mataifa ya Afrika kuimarisha usalama wa rasilimali zake ili kuhakikisha maendeleo endelevu, ustawi wa uchumi pamoja na kuhimili changamoto za kiusalama zinazoendelea kujitokeza duniani.

Mhe. CPA. Makalla amesema hayo wakati akimuwakilisha Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa Mhe. Dkt. Rhimo S. Nyansaho, kwenye ufunguzi wa Kongamano la Usalama wa Taifa jana Mei 25, 2026 Jijini Arusha, ambapo amesema mustakabali wa Afrika unategemea uwezo wa mataifa yake kuandaa na kutekeleza mikakati inayozingatia mazingira na mahitaji halisi ya bara hilo.

Ameongeza kuwa, Afrika imebarikiwa kuwa na rasilimali nyingi zinazoweza kuchochea maendeleo na ukuaji wa uchumi iwapo zitasimamiwa vizuri, huku akisisitiza umuhimu wa kuzilinda dhidi ya matumizi mabaya na vitisho vya nje kwaajili ya usalama na umoja wa bara hilo.

“Suala ya ulinzi na usalama ni mtambuka likihusisha mambo mengi ikiwemo Ulinzi na Usimamizi wa Rasilimali hivyo, ulinzi na usalama wetu ni pamoja na kuzisimamia rasilimali hizo.” Amesema Mhe. CPA Makalla mbele ya wajumbe wa Kongamano hilo kutoka Nchini Tanzania, Kenya, Uganda, Rwanda, Burundi, Afrika Kusini, Namibia na Botswana

Kwa upande wake, Mkuu wa Chuo cha Ukamanda na Unadhimu Tanzania, Meja Jenerali Stephen Mnkande, amesema Kongamano hilo lenye kaulimbiu ya “Maendeleo endelevu ya Afrika kwaajili ya Usalama wa Taifa”, limekuwa jukwaa muhimu la kubadilishana mawazo, uzoefu pamoja na kujadili mikakati mipya ya kukabiliana na changamoto za kiusalama, akisema Chuo hicho kinaendelea kujenga uelewa mpana wa masuala ya usalama wa taifa kwa wadau wa kijeshi na wananchi kwa Ujumla.

26/05/2026

DAR ES SALAAM | Hospitali ya Taifa Muhimbili inaendelea kuimarisha huduma jumuishi kwa wagonjwa wa saratani ya matiti kupitia warsha maalum inayowakutanisha wataalam wa afya pamoja na manusura wa ugonjwa huo. Warsha hiyo inalenga kutoa elimu, kubadilishana uzoefu na kuimarisha ushirikiano katika utoaji wa huduma bora kwa wagonjwa wanaopitia changamoto za saratani ya matiti.

Aidha, hospitali hiyo imeeleza kuwa dhamira yake ni kuhakikisha matibabu hayaishii katika kuokoa maisha pekee, bali pia yanawasaidia wagonjwa kurejesha matumaini, nguvu na kujiamini baada ya matibabu. Kupitia huduma hizo jumuishi, wagonjwa wanapata msaada wa kiafya, kisaikolojia na kijamii ili kuwawezesha kurejea katika maisha yao ya kawaida kwa ujasiri zaidi.

WAZIRI MKUU Dkt. Mwigulu Nchemba ameondoka nchini Jana (Jumatatu, Mei 25, 2026) kwenda Brazzaville, Jamhuri ya Kongo kum...
26/05/2026

WAZIRI MKUU Dkt. Mwigulu Nchemba ameondoka nchini Jana (Jumatatu, Mei 25, 2026) kwenda Brazzaville, Jamhuri ya Kongo kumwakilisha Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwenye Mkutano wa 61 wa Mwaka wa Bodi ya Magavana wa Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB).

Mkutano huo utafanyika Mei 26 – 27, 2026, katika ukumbi wa mikutano wa kimataifa wa Kintele jijini Brazzaville, Jamhuri ya Kongo.

Mkutano huu ni jukwaa muhimu la majadiliano ya kimkakati kuhusu masuala muhimu ya maendeleo ya dunia, yakihusisha nchi wanachama, taasisi za kikanda na kimataifa ambalo linahusisha kuhamasisha upatikanaji wa rasilimali za fedha ili kuwezesha utekelezaji wa ajenda ya maendeleo ya Afrika na kuimarisha uwezo wa bara kukabiliana na changamoto mbalimbali za kiuchumi na kifedha duniani.

Mkutano huo utawakutanisha wajumbe wapatao 3000 ikiwemo Mawaziri wa Fedha na Magavana wa Benki Kuu za Afrika, Watunga Sera, wafanyabiashara, Taasisi za Kifedha, Washirika wa Maendeleo, Wajasiriamali pamoja na Wawekezaji.

26/05/2026

DAR ES SALAAM | Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Paul Makonda (Mb), amesema Tanzania itaendelea kuimarisha na kukuza ushirikiano wake na China katika sekta ya utamaduni, akibainisha kuwa utamaduni umeendelea kuwa daraja muhimu la kuunganisha mataifa hayo mawili kwa miaka mingi.

Makonda ametoa kauli hiyo wakati akizungumza katika maadhimisho ya Siku ya Kimataifa ya Mazungumzo kati ya Tamaduni (International Day for Dialogue among Civilizations) yaliyofanyika katika Hoteli ya Johari Rotana jijini Dar es Salaam.

Amesema Tanzania na China zimeendelea kushirikiana katika nyanja mbalimbali zikiwemo sanaa, utamaduni, elimu na diplomasia ya watu kwa watu, jambo ambalo limechangia kuimarisha uhusiano wa kihistoria uliopo kati ya nchi hizo mbili.

“Utamaduni umeendelea kuwa kiungo muhimu cha urafiki na mshikamano wetu. Tanzania itaendelea kushirikiana na China katika kukuza sekta hii muhimu kwa maendeleo ya kijamii na kiuchumi,” amesema Makonda.

Aidha, Makonda ameeleza kuwa Tanzania na China zina historia kubwa ya ushirikiano iliyoasisiwa na viongozi waasisi wa mataifa hayo, akitolea mfano ujenzi wa Reli ya TAZARA ambayo imeendelea kuwa alama muhimu ya ushirikiano wa kiuchumi pamoja na mchango wake katika harakati za ukombozi wa bara la Afrika.

Katika hatua nyingine, Waziri Makonda amesema Serikali imeanza ujenzi wa Kituo Kikuu cha Kisasa cha Uhifadhi wa Historia ya Ukombozi wa Afrika katika eneo la Kongwa mkoani Dodoma, ambacho kitakuwa sehemu muhimu ya kuhifadhi kumbukumbu za historia ya ukombozi wa bara hilo pamoja na kuendeleza mshikamano wa mataifa ya Afrika.

Maadhimisho hayo yaliambatana na maonesho mbalimbali ya sanaa na burudani za ngoma za asili kutoka Tanzania na China, yakionesha urafiki na ushirikiano wa kiutamaduni kati ya mataifa hayo mawili.

26/05/2026

MARA | Baada ya kutoweka kwa siku nne katika Kijiji cha Mwiseni, juhudi za kumtafuta mtoto Dotto Chigela mwenye umri wa miaka saba, aliyekuwa mwanafunzi wa darasa la kwanza, zimeendelea bila mafanikio.

Inaelezwa kuwa majira ya mchana mtoto huyo alikwenda kuogelea ziwani pamoja na wenzake, jambo ambalo ni la kawaida kwa watoto wa eneo hilo kutokana na wakazi kutumia chanzo hicho cha maji kwa shughuli mbalimbali za nyumbani, ikiwemo kupata maji kwa matumizi ya kila siku.

Mtendaji wa Kijiji cha Mwiseni, Naka Athuman, ametangaza kusitishwa kwa zoezi la utafutaji lililokuwa likifanywa na wananchi, huku akieleza kuwa shughuli zilizobaki sasa zitaendelea chini ya mamlaka husika, ikiwemo TAWA.

TANZIA | Mama Mzazi wa aliyekuwa Rais wa Awamu ya Tano wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Hayati John Pombe Magufuli, S...
25/05/2026

TANZIA | Mama Mzazi wa aliyekuwa Rais wa Awamu ya Tano wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Hayati John Pombe Magufuli, Suzana Magufuli amefariki dunia leo Mei 25, 2026, Chato Mkoani Geita baada ya kuugua kwa muda mrefu.

Akizungumza kwa njia ya simu, Mtoto wa Hayati Magufuli, Jesca Magufuli amethibitisha kutokea kwa msiba huo akieleza kuwa Bibi Suzana amefariki saa 1 usiku Nyumbani kwake Chato.

“Bibi yetu (Suzana M***a) amefariki saa moja nyumbani kwake Chato baada ya kuugua kwa muda mrefu, taratibu za msiba familia itawajulisha, Bwana ametoa na Bwana ametwaa” Jesca.

24/05/2026

MWANZA | Jeshi La Polisi Mkoani Mwanza Limefanikiwa Kuwakamata Watu Wawili Kwa Tuhuma Za Kujihusisha Na Kilimo Cha Zao Lililopigwa Marufuku La Bangi Kwenye Shamba Lenye Ukubwa Wa Zaidi Ya Ekari 10, Pamoja Na Kukutwa Na Shehena Ya Dawa Hiyo Ikiwa Tayari Imeshafungashwa Kwa Ajili Ya Kusafirishwa Kwenda Maeneo Mbalimbali Nchini.

Akitolea Ufafanuzi Wa Mafanikio Hayo , Kamanda Wa Polisi Mkoa Wa Mwanza, Naibu Kamishna Wa Polisi DCP Wilbroad Mutafungwa, Amesema Kuwa Oparesheni Hiyo Ni Muendelezo Wa Mikakati Thabiti Na Endelevu Ya Jeshi La Polisi Katika Kudhibiti Na Kutokomeza Kilimo, Mtandao Wa Usafirishaji, Pamoja Na Biashara Haramu Ya Dawa Za Kulevya.

Kamanda Mutafungwa Ameeleza Kuwa , Jeshi La Polisi Lilipokea Taarifa Kutoka Kwa Wananchi Wema Zikieleza Uwepo Wa Shamba Hilo Kubwa La Bangi Katika Kitongoji Cha Nyerere, Kijiji Cha Busekeseke Kilichopo Tarafa Ya Buchosa, Wilayani Sengerema.

Katika Msako Huo, Polisi Walifanikiwa Pia Kumtia Mbaroni Mtuhumiwa Wa Pili Aliyefahamika Kwa Jina La Mawazo Petro Manisha, Mwenye Umri Wa Miaka 50, Mkulima Na Mkazi Wa Kijiji Cha Busekeseke, Akiwa Eneo La Tukio Ambapo Alikutwa Na Mafurushi Ya Bangi Yaliyokuwa Tayari Kwa Ajili Ya Kusafirishwa.

Kamanda Mutafungwa Ametoa Onyo Kali Na Rai Kwa Jamii Kuacha Mara Moja Kujihusisha Na Kilimo Cha Bangi Na Badala Yake Wajikite Kwenye Kilimo Cha Mazao Halali Ya Chakula Na Biashara Yatakayowaletea Maendeleo

23/05/2026

MTWARA | Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya (DCEA) imeteketeza kilogramu 504.36 za dawa za kulevya aina ya he**in katika kiwanda cha saruji cha Dangote kilichopo mkoani Mtwara. Uteketezaji huo umefanyika kufuatia amri ya Mahakama Kuu Masijala Ndogo ya Mtwara baada ya kukamilika kwa hatua za kisheria dhidi ya watuhumiwa waliohusika na dawa hizo.

Akizungumza na waandishi wa habari leo mkoani humo, Kamishna Jenerali Lyimo amesema, Dawa hizo zilikamatwa ndani ya jahazi la Al Arab lililokuwa na raia saba wa Iran katika Bahari ya Hindi ndani ya eneo la kiuchumi la Tanzania.

Uteketezaji huo umefanyika kwa mujibu wa Sheria ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya Sura ya 95 inayoruhusu kuteketezwa kwa vielelezo vya dawa za kulevya baada ya taratibu za kisheria kukamilika au wakati shauri linaendelea kwa idhini ya mahakama.

Sambamba na hatua hiyo, Kamishna Lyimo amesema Mamlaka imejipanga kuimarisha huduma za tiba na utengemao kwa watu wenye uraibu wa dawa za kulevya hususan katika ukanda wa kusini mwa Tanzania kwa kushirikiana na wadau kuanzisha kliniki ya MAT pamoja na nyumba ya upataji nafuu (sober houses) ili kusaidia waraibu kupata huduma stahiki na kurejea katika maisha yenye tija kwa jamii.

ZANZIBAR | Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi, amesema hana nia ya kuon...
23/05/2026

ZANZIBAR | Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi, amesema hana nia ya kuongeza muda wa Urais zaidi ya muda uliowekwa kikatiba na kuagiza kusitishwa mara moja kwa mijadala kuhusu suala hilo.

Dkt. Mwinyi amesema kupitia majukwaa mbalimbali, ikiwemo Baraza la Wawakilishi, kumekuwa na mijadala na mapendekezo ya kuongeza muda wa Urais badala ya miaka 10 iliyowekwa na Katiba ya Zanzibar, lakini amesisitiza kuwa hana dhamira hiyo na kwamba mjadala huo hauna tija kwa nchi kwa sasa.

Amesema viongozi wameapa kuilinda Katiba ya Nchi na kuwataka wananchi na viongozi kuelekeza nguvu katika utekelezaji wa maendeleo ya taifa. Ameeleza kuwa kipindi kilichobaki cha uongozi wake kitakuwa cha utekelezaji mkubwa na wa kasi zaidi kwa ajili ya maendeleo ya wananchi na nchi kwa ujumla.

Rais Dkt. Mwinyi ameyasema hayo leo tarehe 23 Mei 2026 alipofungua Jukwaa la Wenyeviti na Wakuu wa Taasisi za Umma lililofanyika katika Hoteli ya Golden Tulip Airport, Mkoa wa Mjini Magharibi.

Wakati huo huo, Rais Dkt. Mwinyi amesema Serikali haitakuwa tayari kuendelea kubeba mashirika ya umma yanayoshindwa kujiendesha na kuendelea kutegemea ruzuku kutoka Serikalini.

Amesema bado yapo mashirika ya umma yanayolipwa mishahara na kuendeshwa kwa fedha za Serikali jambo alilosema limepitwa na wakati, huku akiitaka taasisi hizo kujipanga na kujiendesha kwa tija na faida.

Halikadhalika Dkt. Mwinyi amesema Serikali itatoa muda kwa mashirika hayo kufanya mageuzi ya kiutendaji na yale yatakayoshindwa kujiendesha Serikali haitakuwa tayari kuendelea nayo.

ZANZIBAR | Wizara ya Elimu kupitia Idara ya elimu sekondari imekabidhi laptop 3763 kwa walimu wakuu wa unguja  kwa ajili...
23/05/2026

ZANZIBAR | Wizara ya Elimu kupitia Idara ya elimu sekondari imekabidhi laptop 3763 kwa walimu wakuu wa unguja kwa ajili ya wanafunzi walofanya vizuri na kupata division 1 kwa miaka tofauti ikiwemo 2022 kwa laptop 23, 2023 kwa laptop 873 kwa wanfunz w kidato cha 4 na mwaka 2024 laptop 1150 kwa kidato cha 4 na 796 kwa kidato cha 6 aidha ilikabidhi laptop 922 kwa mwaka 2025.

Wizara inatoa pongezi kwa wanafunzi na wadau wote wa elimu na kuahidi kuwa utaratibu wa kukutana na Mhe. Rais itakuwa endelevu ikiwa ni utekelezaji wa ahadi aliotoa Rais Dkt. Hussein Ally Mwinyi.

Address

DODOMA
Dodoma
0255

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when NCHI YETU TV posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share

Category