Karatu Online TV

Karatu Online TV The Official
We shoot • We edit • We Publish • Documentary Karatu Tv

21/03/2026
18/03/2026

Miaka Mitano Sasa Bila Jpm

📢 FURSA YA AJIRA – KARATUMsaka Liquor Store inatangaza nafasi za Wauzaji wa duka la vinywaji (Jumla na Reja Reja) kwa vi...
07/03/2026

📢 FURSA YA AJIRA – KARATU
Msaka Liquor Store inatangaza nafasi za Wauzaji wa duka la vinywaji (Jumla na Reja Reja) kwa vijana wenye bidii na uaminifu wanaotaka kufanya kazi katika mazingira ya biashara ya vinywaji.
K**a una sifa zinazohitajika na upo tayari kufanya kazi kwa kujituma, hii ni nafasi nzuri kwako kujiunga na timu yetu.
📍 Mahali: Karatu Mjini
📞 Wasiliana nasi: 0798422044
👉 Usikose fursa hii – tuma maombi au piga simu kwa maelezo zaidi.
Karibu ujiunge na timu ya MSAKA LIQUOR STORE. 🍾

06/03/2026

WAZIRI MKUU AAGIZA KUZUIWA HATI YA KUSAFIRIA YA MKANDARASI ALIYESHINDWA KUJENGA BWAWA LA EYASI Waziri Mkuu, Dkt. Mwigulu Nchemba, ameagiza kuzuiwa kwa Hati ya Kusafiria ya mkandarasi wa kampuni ya (Tunnel Sadd Ariana Company) Ariana Co, baada ya kushindwa kutekeleza ujenzi wa Bwawa la Eyasi lililopo Wilaya ya Karatu, Mkoa wa Arusha. Dkt. Mwigulu amesema mkandarasi huyo tayari alipokea malipo ya awali ya shilingi bilioni 3 kwa ajili ya utekelezaji wa mradi huo, lakini alishindwa kufanya hivyo. Amesisitiza kuwa Serikali haitamvumilia mkandarasi yeyote anayeshindwa kutekeleza wajibu wake baada ya kupokea fedha za umma, na kwamba hatua kali za kisheria zitachukuliwa ili kulinda rasilimali za Serikali na kuhakikisha miradi ya maendeleo inatekelezwa kwa wakati.

WAZIRI MKUU AWEKA JIWE LA MSINGI MRADI WA UMWAGILIAJI BONDE LA EYASI Waziri Mkuu, Dkt. Mwigulu Nchemba, leo Machi 6, 202...
06/03/2026

WAZIRI MKUU AWEKA JIWE LA MSINGI MRADI WA UMWAGILIAJI BONDE LA EYASI Waziri Mkuu, Dkt. Mwigulu Nchemba, leo Machi 6, 2026 ameweka jiwe la msingi la mradi wa ujenzi wa skimu za umwagiliaji katika Bonde la Eyasi, lililopo Wilaya ya Karatu, Mkoa wa Arusha. Mradi huo unaotekelezwa na Serikali kupitia Tume ya Taifa ya Umwagiliaji utagharimu shilingi bilioni 38.4. Hadi sasa utekelezaji wake umefikia asilimia 30 na unatarajiwa kukamilika ifikapo Novemba mwaka huu. Kukamilika kwa mradi huo utanufaisha zaidi ya wakulima 2,500 kutoka skimu za Mang’ola Barazani, Maleckchand, Laghangareri, Mbuga Nyekundu, Jobaji na Dumbechand, zenye zaidi ya hekta 5,000. Aidha, utekelezaji wa mradi huo utasaidia kupunguza kwa kiwango kikubwa upotevu wa maji unaotokea katika mifereji ya asili, hatua itakayoongeza ufanisi wa matumizi ya maji na kuimarisha uzalishaji wa mazao katika eneo hilo.

BARAZA LA MADIWANI KARATU LAPITISHA BAJETI YA BILIONI 56.08 KWA MWAKA 2026/2027. Baraza la Madiwani la Halmashauri ya Wi...
28/02/2026

BARAZA LA MADIWANI KARATU LAPITISHA BAJETI YA BILIONI 56.08 KWA MWAKA 2026/2027. Baraza la Madiwani la Halmashauri ya Wilaya ya Karatu limepitisha rasimu ya bajeti ya Mpango wa Maendeleo kwa mwaka wa fedha 2026/2027 yenye jumla ya Shilingi 56,081,491,253.33. Uamuzi huo umefikiwa katika kikao maalum cha Baraza la Bajeti kilichofanyika katika ukumbi wa Halmashauri, ambapo madiwani wamejadili kwa kina mapendekezo ya mapato na matumizi kwa lengo la kuhakikisha rasilimali za wilaya zinatumika kwa tija na kuwaletea wananchi maendeleo endelevu. Akiwasilisha mapendekezo ya bajeti, Mwenyekiti wa Halmashauri Mhe. Englibert Qorro amesema fedha hizo zitaelekezwa katika sekta mbalimbali ikiwemo elimu, afya, miundombinu ya barabara, pamoja na huduma za kijamii, kwa kuzingatia vipaumbele vya kitaifa na mahitaji halisi ya wananchi wa Wilaya ya Karatu. Madiwani wamepongeza maandalizi ya bajeti hiyo na kusisitiza uwajibikaji, usimamizi madhubuti wa miradi ya maendeleo, pamoja na ukusanyaji wa mapato ya ndani ili kufikia malengo yaliyowekwa. Kupitishwa kwa bajeti hiyo kunatoa dira ya utekelezaji wa shughuli za maendeleo kwa mwaka ujao wa fedha, huku wananchi wakitarajiwa kunufaika na maboresho ya huduma na miundombinu katika maeneo yao. .

28/02/2026

Mh Cecilia Paresso, Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Arusha na Mwenyekiti wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania leo tar 27/2/2026 afuturisha Waislam wa msikiti wa Karatu mjini. Vile vile ametoa Juzuu 100, msahafu 50, tasbihi, kanzu pamoja na kofia(baraghashe)kwa ajili ya kuwalea vijana katika maadili ya dini sambamba na mkono wa sadaka kiasi cha shilingi 1,000,00 . .tanzania

Mheshimiwa Cecilia Paresso,  Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Arusha na Mwenyekiti wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanza...
27/02/2026

Mheshimiwa Cecilia Paresso, Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Arusha na Mwenyekiti wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, leo tarehe 27/02/2026 amefuturisha Waislamu katika Msikiti wa Karatu Mjini, wilayani Karatu. Katika tukio hilo la kihistoria lenye lengo la kuimarisha mshik**ano na maadili ya dini, Mheshimiwa Paresso ametoa msaada wa:
Juzuu 100, Misahafu 50, Tasbihi, Kanzu, Kofia (baraghashe) Misaada hiyo imelenga kuwalea na kuwaimarisha vijana katika misingi ya maadili ya dini na hofu ya Mungu. Aidha, amekabidhi mkono wa sadaka kiasi cha shilingi 1,000,000 kwa ajili ya kusaidia shughuli za msikiti na jamii kwa ujumla. Akizungumza na waumini, Mheshimiwa Paresso Amesisitiza umuhimu wa umoja, mshik**ano na kuendeleza maadili mema katika jamii.
“KAZI NA UTU, TUNASONGA MBELE.”

27/02/2026

Asanterabi Ndiyo Bus Bora kwa Wananchi wa Jimbo la Karatu

Wananchi wa jimbo la Karatu wameendelea kunufaika na huduma bora za usafiri zinazotolewa na Asanterabi Express, kampuni inayojulikana kwa ubora, usalama na uhakika wa safari. Kupitia mabasi yake ya kisasa na huduma rafiki kwa wateja, Asanterabi imeendelea kuwa chaguo la kwanza kwa wasafiri wanaosafiri kwenda na kutoka Karatu.

Huduma za Asanterabi zinajumuisha tiketi zinazopatikana kwa urahisi mtandaoni au kwa kupiga simu kwa huduma kwa wateja, hatua ambayo imepunguza usumbufu wa kufika ofisini. Hii imewafanya wananchi wengi kupata usafiri kwa urahisi zaidi, hasa katika vipindi vya shughuli nyingi k**a msimu wa sikukuu na safari za kikazi.

Mbali na hilo, kampuni imeweka kipaumbele katika usalama wa abiria, muda sahihi wa kuondoka na kufika, pamoja na mazingira mazuri ndani ya basi. Haya yote yameifanya Asanterabi kuendelea kujenga imani kubwa kwa wananchi wa Karatu na maeneo jirani.

Kwa ujumla, Asanterabi Express inaendelea kuthibitisha kuwa ni bus bora na ya kuaminika kwa wananchi wa jimbo la Karatu, ikitoa huduma inayokidhi mahitaji ya wasafiri wa kisasa.

27/02/2026

Shirika lisilo la kiserikali la SOS Children's Villages tawi la Karatu limekabidhi pikipiki saba kwa vikundi vya vijana wilayani humo ikiwa ni sehemu ya juhudi za kuwawezesha kiuchumi na kuwainua kimaisha. Pikipiki hizo zimekabidhiwa na Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Karatu, Ndg. Juma Hokororo, katika hafla iliyofanyika wilayani Karatu. Akizungumza wakati wa makabidhiano hayo, Hokororo amelipongeza shirika hilo kwa hatua hiyo muhimu ya kuwekeza kwa vijana, akieleza kuwa uwezeshaji huo utasaidia kuongeza ajira na kipato kwa wanufaika pamoja na familia zao. Amesema kuwa serikali itaendelea kushirikiana na mashirika yasiyo ya kiserikali katika kuwaletea wananchi maendeleo endelevu, hasa kwa makundi ya vijana ambao ni nguvu kazi ya taifa. Aidha, amemshukuru Mhe. Dkt, Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kwa kuimarisha mazingira rafiki ya ushirikiano kati ya serikali na mashirika yasiyo ya kiserikali, ushirikiano huo umewezesha mashirika mengi kukua na kutoa mchango mkubwa katika kukuza uchumi wa taifa na wa mtu mmoja mmoja. Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa, pikipiki hizo saba zimegharimu zaidi ya shilingi milioni 19, na zinatarajiwa kusaidia vijana hao katika shughuli za usafirishaji na biashara ndogo ndogo, hivyo kuongeza fursa za ajira na kipato katika jamii ya Karatu. . ..

27/02/2026

Kampuni ya usafirishaji ya AsanteRabi Express inapenda kuwataarifu wananchi kuwa safari kutoka Karatu kuelekea Dar es Salaam na kutoka Dar es Salaam kurejea Karatu zinaendelea k**a kawaida.
🚌 Safari zinapatikana kila siku
🕐 Muda wa kuondoka: Saa 1:00 Jioni
Tunawahimiza wasafiri kufika mapema kwa maandalizi ya safari na kupata huduma bora na salama.
AsanteRabi Express – Tunajali muda wako na usalama wako.

Address

Karatu

Opening Hours

Monday 09:00 - 16:00
Tuesday 09:00 - 16:00
Wednesday 09:00 - 16:00
Thursday 09:00 - 16:00
Friday 09:00 - 17:00
Saturday 09:00 - 12:00
Sunday 09:00 - 12:00

Telephone

+255673941419

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Karatu Online TV posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Karatu Online TV:

Share