24/07/2023
UNAFAHAMU SABABU ZA KIFO CHA GAFLA WAKATI WA TENDO LA NDOA?
Tendo la ndoa hufurahisha, na kadiri siku zinavyozidi kusonga tangu enzi za mababu zetu, ni tendo ambalo limetokea kufurahiwa na wanaume na wanawake.
Hatahivyo wale wanaofanya tendo la ndoa wanaweza kuwa katika hatari ya kufa kifo cha ghafla, au wote wanaweza kupata maambukizi au kuugua wakati wa tendo hilo.
Mwanaume anaweza kufia juu ya mwanamke, na mwanamke anaweza kufia chini ya mwanaume wakati wanapokuwa katika tendo la kujamiiana, jambo linalowashangaza wengi.
Wengi huwa hawaamini tukio k**a hili linapotokea.
Lakini wataalamu wa masuala ya tiba wameelezea mambo yanayoweza kusababisha mtu kufa wakati wa tendo hilo, iwe kwa wanawake au wanaume.
Yafuatayo ni mambo matatu yanayoweza kusababisha mtu kufa wakati wa kujamiiana.
1. Matumizi mabaya ya dawa:
Wanaume mara nyingi hutumia dawa za kitamaduni au miti shamba ili kuwasaidia kuwa thabiti wakati wa tendo jambo ambalo sio baya k**a zitatumika vizuri. Lakini Wengine huzichanganya na bia wakiamini kuwa zitawasaidia katika kuongeza nguvu za kiume na hivyo kuweza hata kujamiiana na wanawake zaidi ya mmoja Kwa wakati mmoja kitu ambacho ni hatari sana Kwa afya.
Wakati mwingine, baadhi ya wanaume huvuta sigara, na madawa mengine ya mihadarati ili kuongeza nguvu zao za kiume huku wakiwa tayari wameitumia dawa za kuongeza nguvu za kiume..
Kile ambacho hawajui ni kwamba sigara na madawa hayo ya mihadarati huwa na kemikali inayoitwa "Nitrate", ambayo inaweza kusababisha shinikizo la juu la damu na kusababisha kifo cha ghafla wakati wa tendo hilo
Mwisho wa yote, athari zake huwa ni mbaya,licha ya heshima wanayoitaka kutoka kwa mwanamke wanayefanya naye tendo la ndoa
2. Maradhi ya moyo:
Matatizo ya kiafya sio jambo linalopaswa kupuuzwa inapokuja katika suala la kushiriki mapenzi
Mtu mwenye historia ya ugonjwa wa moyo anaweza kufa wakati wa tendo hilo kwasababu moyo wake utafanya kazi ngumu kuliko wakati wa kawaida
Sababu za mara kwa mara za magonjwa ya moyo, hususan kwa wanawake wenye zaidi ya miaka 50 na wanaume wenye miaka 40 ni shinikizo la damu , uvutaji wa sigara, kisukari, kiharusi na magonjwa mengine.
Sababu nyingine ambayo mara nyingi husababisha magonjwa ya moyo ni msongo mkubwa wa mawazo.
Mshtuko wa moyo wakati wa tendo la ndoa mara nyingi unawakumba wanaume kuliko wanawake, utafiti unaonyesha hivyo.
Kumbuka watu 34 hupata mshtuko wa moyo kati ya 4,557 wakati au ndani ya saa moja ya kujamiiana na 32 ya wale walioathiriwa walikuwa wanaume.
Dr Sumeet Chugh, wa Taasisi ya Moyo ya Cedars-Sinai Heart Institute alisema utafiti wake ni wa kwanza kutathmini shughuli za ngono k**a sababu inayowezesha kusababisha mshutuko wa moyo. Utafiti wake huo uliwasilishwa katika mkutano wa American Heart Association wakati wa kutathmini vichocheo vinavyosababisha mshtuko wa moyo .
Hatua hiyo hutokea wakati moyo unapopata matatizo na kuacha kupiga . Mtu hupoteza fahamu na kukosa kupumua Iwapo hatofanyiwa utaratibu wa CPR ili kumuokoa huweza kupoteza maisha.
Mshutuko wa moyo ni tofauti na shambulio ambalo hukumba moyo na kuzuia damu kuufikia .
3. Matumizi ya kupindukia ya dawa za kuongeza nguvu za kiume
Dawa ya Vi**ra zimekuwa zikiuzwa katika maduka mbalimbali ya dawa duniani kote, kwa lengo la kuwasaidia wanaume hususan wenye magonjwa yaliyoathiri nguvu zao za kiume kuweza kurejesha uwezo huo. Kulingana na wataalamu dawa hii zinapaswa kutolewa na Daktari kwa vipimo vinavyohitajika kulingana na tatizo lenyewe la kiafya alilonalo mhusika.
Hatahivyo kutokana na upatikanaji wake kwa njia rahisi wa dawa hizi, baadhi ya vijana na wanaume wamekuwa wakizinunua kiholela kwenye maduka ya dawa na kuzitumia ili kuwaridhisha wapenzi wao bila kupata ushauri wa daktari.
Kulingana na wataalam matumizi yasiofaa ya dawa hizi yanaweza kusababisha matatizo ya moyo na hivyo kuweza kuchochea kutokea kwa kifo wakati wa tendo hilo.