The Green Voice TV

The Green Voice  TV Karibu The Green Voice TV, usisahau ku "Subscribe" You tube channel yetu. "Yes we are Green".

30/05/2026
BAO! ⚽Ousmane Dembélé anafunga kwa mkwaju wa penalti na kuisawazishia Paris Saint-Germain katika fainali ya UEFA Champio...
30/05/2026

BAO! ⚽

Ousmane Dembélé anafunga kwa mkwaju wa penalti na kuisawazishia Paris Saint-Germain katika fainali ya UEFA Champions League Final.

Paris Saint-Germain 1-1 Arsenal

Mchezo umepamba moto! 🔥

30/05/2026

KUTOKA KWENYE BANDA UMIZA FURAHA YA PENATI YA PSG ✈️

Mnamo Mei 30, 2026 saa 12:20 asubuhi katika Kijiji cha Mambi, Kata ya Kongolo, Tarafa ya Ilongo, Wilaya ya Mbarali, Mkoa...
30/05/2026

Mnamo Mei 30, 2026 saa 12:20 asubuhi katika Kijiji cha Mambi, Kata ya Kongolo, Tarafa ya Ilongo, Wilaya ya Mbarali, Mkoa wa Mbeya katika barabara kuu ya Mbeya – Njombe, Gari yenye namba za usajili T115 DEH ikiwa na Tela namba T150 DFU aina ya Volvo Tank mali ya kampuni ya Syenergy ya Jijini Dar es Salaam ikiwa imebeba shehena ya mafuta aina ya Diesel ikitokea Dar es Salaam kuelekea Mkoa wa Songwe – Tunduma ikiendeshwa na Dereva Mohamed Seif maarufu Maurid [60] mkazi wa Dar es Salaam aliendesha Gari kwa uzembe na kuhama upande wake wa kushoto na kwenda upande wa kulia wa barabara na kuigonga Gari T200 ENQ aina ya Yutong Basi la abiria mali ya kampuni ya ABC Upper Class iliyokuwa inatoka Mbeya kuelekea Dar es Salaam ikiendeshwa na Dereva aitwaye Ased Asamu maarufu Tembo [40] mkazi wa Dar es Salaam na kusababisha vifo vya watu watatu na majeruhi mmoja na uharibifu wa magari yote mawili.

Waliofariki katika ajali hiyo ni Ased Asad maarufu Tembo [40] Dereva wa Basi, Letisia Bujabi [32] Kondakta wa Basi na Mohamed Seif maarufu Maurid [60] Dereva wa Lori. Aidha, katika ajali hiyo watu wanne walijeruhiwa kati yao watatu walitibiwa na kuruhusiwa na majeruhi mmoja aitwaye Mariam Abdul [25] mkazi wa Kijichi Dar es Salaam amelazwa katika Hospitali ya Inyala akiendelea kupatiwa matibabu.

Chanzo cha ajali ni uzembe wa Dereva wa Lori kutokuwa makini barabarani akiwa anapishana na Gari lingine.

Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya linatoa wito kwa madereva kuwa makini wawapo barabarani ikiwa ni pamoja na kuzingatia sheria za usalama barabarani ili kuepuka ajali.

30/05/2026

10’ PSG 0-1 Arsenal

⚽️Havertz 06’
PSG 0 - 1 Arsenal! Hili ndio shangwe lao hapa Viwanja vya Posta Kijitonyama! 🎥

Kai Havertz ameanza kwa kasi baada ya kujitoa kwa ustadi na kupiga shuti kali lililotinga moja kwa moja kwenye paa la ny...
30/05/2026

Kai Havertz ameanza kwa kasi baada ya kujitoa kwa ustadi na kupiga shuti kali lililotinga moja kwa moja kwenye paa la nyavu 💥

30/05/2026

USHINDI WA KISHINDO TANGA! Captain wa Polisi Tanzania afichua kilichoibeba timu kuizamisha African Sports 3-1, atangaza vita ya kupanda Ligi Kuu

Nahodha wa Polisi Tanzania amesema ushindi wa mabao 3-1 dhidi ya African Sports katika mchezo uliochezwa kwenye Uwanja wa CCM Mkwakwani jijini Tanga umetokana na nidhamu ya hali ya juu, kujituma kwa kila mchezaji uwanjani pamoja na kufuata kwa umakini maelekezo ya benchi la ufundi. Nahodha huyo amesema ushindi huo ni ishara ya dhamira kubwa waliyonayo ya kuhakikisha timu inafanikisha ndoto ya kupanda Ligi Kuu msimu huu. Aidha, amewapongeza mashabiki wa Polisi Tanzania kwa kuendelea kuisapoti timu kwa nguvu zote, akisisitiza kuwa ushirikiano wao ni chachu kubwa ya mafanikio na kwamba kikosi hicho kitaendelea kupambana kwa nguvu hadi kufikia lengo lao.

30/05/2026

USHINDI WA KISHINDO TANGA! Captain wa Polisi Tanzania afichua kilichoibeba timu kuizamisha African Sports 3-1, atangaza vita ya kupanda Ligi Kuu

Nahodha wa Polisi Tanzania amesema ushindi wa mabao 3-1 dhidi ya African Sports katika mchezo uliochezwa kwenye Uwanja wa CCM Mkwakwani jijini Tanga umetokana na nidhamu ya hali ya juu, kujituma kwa kila mchezaji uwanjani pamoja na kufuata kwa umakini maelekezo ya benchi la ufundi. Nahodha huyo amesema ushindi huo ni ishara ya dhamira kubwa waliyonayo ya kuhakikisha timu inafanikisha ndoto ya kupanda Ligi Kuu msimu huu. Aidha, amewapongeza mashabiki wa Polisi Tanzania kwa kuendelea kuisapoti timu kwa nguvu zote, akisisitiza kuwa ushirikiano wao ni chachu kubwa ya mafanikio na kwamba kikosi hicho kitaendelea kupambana kwa nguvu hadi kufikia lengo lao.

30/05/2026

Mashabiki wa Klabu ya Arsenal ya nchini England wakiingia kwa maandamano katika viwanja vya Posta Kijitonyama jijini Dar es Salaam, ambako hii leo saa 1:00 jioni watashuhudia mchezo wa fainali ya Klabu Bingwa Barani Ulaya (UEFA) baina ya timu yao na Paris Saint German (PSG) ya nchini Ufaransa.

Unadhani ni timu gani itatwaa ubingwa UEFA usiku wa leo?

Tuandikie kwenye uwanja wa comments.
Fainali inapigwa saa moja usiku katika dimba la Puskas Arena Mjini Budapest, Hungary.

Nani kubeba Kombe UEFA leo

Address

Rungwe
Mbeya

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when The Green Voice TV posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share