The Green Voice TV

The Green Voice  TV Karibu The Green Voice TV, usisahau ku "Subscribe" You tube channel yetu. "Yes we are Green".

19/06/2026

Rose Muhando Atikisa Dodoma Kwenye Kongamano la Operation Washa Taa Malango Yako Kufunguka

WIMBO GANI WA ROSE MUHANDO UNAKUKOSHA SANA?? MUHANDO

19/06/2026

Je hoja ya Mbunge wa Mbeya Mjini Mhe. Mwalunenge inaweza kutekelezeka,.? πŸ€”πŸ€”

SERIKALI YAHIMIZA WAZAZI/WALEZI   MALEZI YA WATOTONa Jackline Minja, DodomaNaibu Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, W...
19/06/2026

SERIKALI YAHIMIZA WAZAZI/WALEZI MALEZI YA WATOTO

Na Jackline Minja, Dodoma

Naibu Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum, Mhe. Mhandisi Maryprisca Mahundi, amewahimiza wazazi na walezi kuimarisha malezi ya watoto wao na kutoa taarifa mapema kwa maafisa ustawi wa jamii pale wanapobaini changamoto zinazoweza kuhatarisha ustawi wa mtoto.

Mhe. Mahundi ametoa wito huo wakati akijibu swali la Mbunge wa Viti Maalum, Martha Festo Mariki leo Juni 19, 2026 bungeni Dodoma, ambapo amebainisha kuwa Serikali imeendelea kuimarisha mikakati mbalimbali ya kukabiliana na tatizo la watoto wanaoishi na kufanya kazi mitaani nchini, ikiwemo kutoa elimu kwa wazazi na walezi, kuimarisha uchumi wa kaya na kuboresha huduma za ustawi wa jamii.

Amesema Serikali imeweka mkazo katika kuelimisha wazazi na walezi kuhusu wajibu wao wa kuwalea na kuwatunza watoto ili kuwazuia kukimbilia maisha ya mitaani.

"Serikali inaendelea kutoa elimu kwa walimu na jamii kwa ujumla kuhusu umuhimu wa kutoa taarifa kwa vyombo vya dola mara mtoto anapopotea nyumbani au shuleni, hatua ambayo imekuwa ikisaidia kuzuia watoto wengi kuingia katika mazingira ya kuishi mitaani." Amesema Mahundi

Katika hatua nyingine, Mhe. Mahundi amesema Serikali imeanzisha Madawati ya Huduma za Ustawi wa Jamii katika vituo vya usafirishaji nchini kwa lengo la kuwabaini na kuwasaidia watoto wanaotoroka majumbani kuelekea mitaani ambapo Madawati hayo yanasaidia kubaini watoto walio katika hatari na kuwaunganisha na familia zao kabla hawajaingia katika maisha mtaani aidha kuimarisha uchumi wa kaya ni sehemu muhimu ya suluhisho la changamoto hiyo, kwani umasikini ni miongoni mwa sababu zinazochangia baadhi ya watoto kuondoka nyumbani.

Takwimu zinaonesha kuwa kati ya Julai 2025 na Februari 2026, jumla ya watoto 6,182 waliokolewa kutoka mitaani, huku watoto 5,663 kati yao wakiunganishwa tena na familia zao na wengine kupatiwa huduma mbalimbali kulingana na mahitaji yao.

Hata hivyo Serikali imesisitiza kuwa itaendelea kushirikiana na wadau mbalimbali kuhakikisha tatizo la watoto wa mtaani linapungua na hatimaye kutokomezwa kabisa nchini.

18/06/2026
18/06/2026

Depu anataka kufunga goli k**a la Chama,lile goli sio kila mchezaji anaweza kufunga

18/06/2026

Ukiishi maisha haya wewe ni MASIKINI PROFESA SOSPETER

SERIKALI YAIMARISHA USIMAMIZI WA MIKOPO YA WAFANYABIASHARA NDOGONDOGO.Na Jackline Minja, WMJWM- DodomaSerikali imeendele...
18/06/2026

SERIKALI YAIMARISHA USIMAMIZI WA MIKOPO YA WAFANYABIASHARA NDOGONDOGO.

Na Jackline Minja, WMJWM- Dodoma

Serikali imeendelea kuimarisha mfumo wa usimamizi wa mikopo yenye masharti nafuu inayotolewa kwa wafanyabiashara ndogondogo ili kuhakikisha fedha hizo zinawanufaisha walengwa na kudhibiti upotevu wa fedha za umma.

Kauli hiyo imetolewa Juni 18, 2026 bungeni na Naibu Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum Mhe. Mhandisi Maryprisca Mahundi wakati akijibu swali la Mbunge wa Viti Maalum, Mhe. Tamima Haji Abass, aliyehoji kuhusu uwepo wa mwongozo na utaratibu wa kusimamia mikopo hiyo.

Mhe. Mahundi amebainisha kwamba, Serikali imeingia makubaliano na Benki ya NMB kusimamia utoaji wa mikopo yenye riba nafuu ya asilimia saba kwa mwaka kwa wafanyabiashara ndogondogo wanaokidhi vigezo vilivyowekwa, ikiwemo kuwa na kitambulisho cha kidijitali.

Amefafanua kuwa kabla ya mkopo kutolewa, biashara husika hutembelewa na kutathminiwa ili kujiridhisha k**a inakidhi masharti ya kupata mkopo. Baada ya hapo, waombaji hupatiwa mafunzo ya usimamizi wa fedha na biashara kabla ya kupokea mkopo, hatua inayolenga kuongeza ufanisi wa matumizi ya fedha hizo na kuimarisha uwezo wa kurejesha mikopo kwa wakati.

β€œMarejesho ya mikopo hiyo yanafuatiliwa na maafisa wa Benki ya NMB kwa karibu ili kuhakikisha fedha za Serikali zinaendelea kuzunguka na kuwafikia walengwa wengi zaidi. Mfumo huo umewekwa mahsusi kuimarisha uwajibikaji na kupunguza changamoto za ucheleweshaji au kutorejeshwa kwa mikopo" amesema Mhe. Mahundi

Aidha, amesema utaratibu huo umeainishwa katika Mwongozo wa Utoaji wa mikopo yenye masharti nafuu kwa Wafanyabiashara ndogondogo kupitia Taasisi za Fedha wa mwaka 2024, ambao umeweka misingi ya utoaji na usimamizi wa mikopo hiyo nchini. Mwongozo huo unalenga kujenga mfumo endelevu wa uwezeshaji wananchi kiuchumi kupitia sekta ya biashara ndogo ndogo.

Hatua hizo zinaendelea kuonesha dhamira ya Serikali ya Awamu ya Sita ya kuwawezesha wananchi kiuchumi kupitia mikopo nafuu huku ikiimarisha mifumo ya usimamizi na ufuatiliaji wa fedha za umma ili ziweze kuleta matokeo chanya kwa walengwa na maendeleo ya uchumi wa Taifa kwa ujumla.

MWISHO

🐐⚽ MESSI ANA MAGOLI 3, MASHABIKI WA RONALDO WANA DAKIKA 3 ZA KUJIELEZA! πŸ˜‚πŸ”₯
17/06/2026

🐐⚽ MESSI ANA MAGOLI 3, MASHABIKI WA RONALDO WANA DAKIKA 3 ZA KUJIELEZA! πŸ˜‚πŸ”₯

17/06/2026

Rayvanny Afunguka Mazito Aliyopitia Kabla ya Kutumbuiza Ufunguzi wa Kombe la Dunia 2026

Address

Rungwe
Mbeya

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when The Green Voice TV posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share