Kimath Marketing Investiment

Kimath Marketing Investiment Contact information, map and directions, contact form, opening hours, services, ratings, photos, videos and announcements from Kimath Marketing Investiment, Advertising/Marketing, ELIZARACHELREBEKA INVESTIMENT, Moshi.

25/08/2025

Huko Tanzania, chama tawala CCM kimekamilisha mchakato wake wa kuteua makada watakaowania nafasi za ubunge, uwakilishi na udiwani. Mchora vibonzo wetu Said Michael 'Wakudata' amekuja na taswira ya vilio na vicheko kwenye uteuzi huo. Je, kibonzo kinaakisi kinachoendelea kwenye chama hicho?

02/06/2025

KUFUNGWA KWA SHUGHULI ZA KANISA LA GLORY OF CHRIST CHURCH - KANISA LA UFUFUO NA UZIMA

Chini ya Kifungu cha 17(b) na kifungu cha 2 cha Sheria ya Jumuiya Sura ya 337 k**a kilivyorekebishwa na kifungu cha 39(b) cha Sheria ya Marekebisho Mbalimbali ya Sheria Namba. 3 ya Mwaka 2019

Tafadhali, rejea somo tajwa hapo juu.

2. Katika siku za hivi karibuni, kupitia vyombo vya habari na mitandao ya kijamii, umeonekana ukiwa katika mimbari ya Kanisa la Glory of Christ Church @ Kanisa la Ufufuo na Uzima, ukitoa mahubiri yenye mwelekeo wa kisiasa na nia ya kuichonganisha Serikali na wananchi. Vitendo hivi ni kinyume cha Sheria ya Jumuiya Sura ya 337na vinaweza kuhatarisha amani na utulivu nchini.

3. Kwa Mamlaka niliyopewa, Ofisi ya Msajili wa Jumuiya za Kiraia inafuta usajili wa Glory of Christ Church @ Kanisa la Ufufuo na Uzima, kuanzia leo tarehe 02 Juni 2025. Hivyo, unatakiwa kusitisha shughuli za Kanisa lako mara moja.

4. Chini ya kifungu cha 19(1) cha Sheria ya Jumuiya Sura ya 337, Kanisa lina haki ya kukata rufaa juu ya uamuzi huu kwa Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi kupitia kwa Katibu Mkuu, ndani ya siku 21 kuanzia tarehe ya barua hii.

5. Kwa Amri ya Msajili wa Jumuiya za Kiraia.

02/06/2025
02/06/2025
02/06/2025

Msanii wa Bongo fleva lavalava rasmi ameondoa utambulisho wake chini ya lebo ya WCB ( Wasafi Classic Baby), ambayo ilikuwa ikisimamia kazi zake toka alipojiunga nayo mwaka 2015.

Lavalava alijiunga na lebo hiyo ya muziki na alikuwa mmoja wa wasanii wa mwanzo kabisa kusainiwa chini ya lebo hiyo inayomilikiwa na

Kabla ya kusainiwa rasmi, Lavalava alikuwa akifanya kazi nyuma ya pazia k**a mtunzi wa nyimbo (songwriter) kwa baadhi ya wasanii wa WCB, na baadaye akaibuka k**a msanii kamili kupitia wimbo wake wa kwanza maarufu "Dede" ulioachiwa mwaka 2017.

Diamond aliwahi kuongea kwenye mahojiano kuhusu Lavalava na kusema ni miongoni mwa Wasanii waliokuwa na heshima na nidhamu sana hivyo hata akitaka kutoka kwenye lebo hiyo hata mtoza chochote tena atampatia na mtaji

Je, Unahisi Lavalava kweli ametoka WCB?

02/06/2025

Nay wa Mitego akerwa na stori za Ndoa ya Diamond Platnumz na Zuchu Akisema kuwa ni Umbea

"Wabongo wanapenda sana umbea Yani mpaka unashangaa ivi awa ni watu wa aina gani.? Kuna mambo ya msingi yanaendela kuhusu nchi mjadala mikubwa ipo, wameletewa umbea kwa makusudi now wamehamia kwenye umbea. My Country" Ameandika

02/06/2025

Gwiji wa soka duniani, Zinedine Zidane, amethibitisha kile ambacho wengi wamekuwa wakikisia kwa muda mrefu, kuwa anataka kuwa kocha wa timu ya taifa ya Ufaransa.

🗣️ "Timu ya taifa ya Ufaransa bado ipo moyoni mwangu. Natamani sana kuifundisha. Natumaini siku moja nitapata nafasi hiyo. Ningependa kumaliza safari yangu ya soka nikiwa kocha wa timu ya taifa," alisema Zidane alipokuwa akizungumza na gazeti la L’Équipe.

Tangu aondoke Real Madrid mwaka 2021, Zidane hajapata timu ya kuifundisha rasmi. Akiwa kocha wa Real Madrid, alishinda Ligi ya Mabingwa Ulaya mara tatu mfululizo, jambo lililomfanya kuwa mmoja wa makocha bora kabisa duniani.

Kwa sasa, kocha wa Ufaransa ni Didier Deschamps, lakini tayari amesema ataondoka baada ya Kombe la Dunia mwaka 2026. Hili linaibua matumaini kuwa huenda wakati wa Zidane kuwa kocha wa Les Bleus umefika.

âš˝ Zidane ana historia kubwa na timu ya taifa ya Ufaransa. K**a mchezaji, aliisaidia kushinda Kombe la Dunia mwaka 1998 na Euro mwaka 2000.

POWERED BY:
✍️ |

02/06/2025

Kumbe shida inakuaga United🤣

Gazeti la Mpasho

02/06/2025

FEISAL SALUM ni kweli anahitajika na timu kadhaa ikiwemo Simba, Kaizer Chiefs na Young Africans, Mchezaji huyo ili ununue mkataba wake wa mwaka mmoja uliosalia unapaswa kulipa dola 500,000 kwa Azam FC ambayo haina tabu kufanya biashara ikiwa ni sawa na Billion 1.3 za Kitanzania.

Bado mkataba wa Feisal Salum ni kuwa endapo Azam watamuuza nje ya nchi basi Yanga anakula 25% ya mauzo na k**a atauzwa ndani basi Yanga anapaswa kupewa BILLION MOJA.

UHALISIA ni kuwa Simba ya Msimbazi ndio mpaka sasa ina nafasi kubwa zaidi ya kumnasa Mwanandinga huyo kutoka Visiwani ambapo wapo tayari kumpa Mshahara wa Million 50, nyumba Masaki na Usafiri, huku bonus mbalimbali pia watakuwa wanamlipa, Kambi ya Mchezaji na Mchezaji wamevutiwa zaidi na ofa ya Simba.

Kwa mujibu wa vyanzo vyangu ni kuwa Yanga walipeleka ofa yao ambayo Simba wameenda juu zaidi na inadaiwa Wananchi hawapo tayari kupanda juu ya hapo, lakini utata unasalia kuwa Simba watatumia pesa nyingi kumlipa Feisal halafu bado wana kipengele kwa Azam cha Billion 1.5 za Kumnunua, huku Azam nao wanapaswa kuwapa Yanga Billion moja, utata pekee upo hapo, fuatilia vyema cinema hii nyingine vizuri.

Ila hisia, mawazo na kila kitu cha Feisal kwa mujibu wa taarifa, zaidi ya 80% ni kucheza Simba msimu ujao."

02/06/2025

: Lionel Messi na Luis Suárez wamethibitisha kuanzisha klabu yao inayoitwa Deportivo LSM, timu hiyo itaanza kushiriki mashindano katika daraja la nne nchini Uruguay.

Nembo ya klabu ya LSM inaunganisha chapa binafsi za majina ya nyota hao wawili.

02/06/2025

Msanii wa mziki wa bongo fleva kutokea nchini Tanzania Mbosso Khan amesema kuwa kwa Vijana ambao wanamiliki mishangazi waendelee kuinjoi.

Kauli hii imefuatia baada ya kuulizwa swali na muhandishi wa habari kuhusu kutafutwa na mishangazi akasema hapana hajawahi kutafutwa .

''hamna sijapata nafasi hiyo nafurahi swali lako zuri waendelee kuinjoy.Amesema Mbosso Khan

Address

ELIZARACHELREBEKA INVESTIMENT
Moshi

Telephone

0718364882

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Kimath Marketing Investiment posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Kimath Marketing Investiment:

Share