Mtwara Press Club

Mtwara Press Club Mtwara Press Club is officially licensed by TCRA to provide online content. Informing, educating, and entertaining through content providing is our

We, MTPC are proud and ready to serve the community of Mtwara and outside the boundaries of Mtwara as well.

Rais Samia Suluhu Hassan wa Tanzania ametoa tangazo la kusisimua kuhusu uhusiano wa karibu na Guinea-Bissau, akisisitiza...
22/06/2024

Rais Samia Suluhu Hassan wa Tanzania ametoa tangazo la kusisimua kuhusu uhusiano wa karibu na Guinea-Bissau, akisisitiza nia ya nchi hizi mbili katika kukuza biashara na uwekezaji. Katika mkutano na viongozi kutoka Guinea-Bissau, Rais Samia alielezea azma ya pande zote kuchukua hatua za makusudi kuboresha ushirikiano wao, hususan katika sekta ya kilimo na biashara ya zao la korosho.

Tanzania na Guinea-Bissau ni wazalishaji wakubwa wa korosho barani Afrika, na kwa pamoja zinaweza kuchangia sana katika kuboresha thamani ya zao hili muhimu. Kupitia utafiti na uvumbuzi wa pamoja, nchi hizi zinatafuta njia za kuongeza uzalishaji na ubora wa korosho, na hivyo kuongeza mapato kwa wakulima na kukuza uchumi kwa ujumla.

Rais Samia pia aliongezea kuwa ushirikiano huu utasaidia kuvutia zaidi uwekezaji kutoka sekta binafsi katika miundombinu na teknolojia za kisasa zinazohitajika kwa maendeleo ya kilimo cha korosho. Kwa kufanya hivyo, Tanzania na Guinea-Bissau zinaimarisha msingi wao wa kiuchumi na kuweka misingi imara ya maendeleo endelevu na ustawi kwa wananchi wao.

Chama cha waandishi wa Habari Mkoani Mtwara (MTPC) wamemuaga Mkuu wa Mkoa anayemaliza muda wake Mh. Meja Jenerali Marko ...
05/08/2022

Chama cha waandishi wa Habari Mkoani Mtwara (MTPC) wamemuaga Mkuu wa Mkoa anayemaliza muda wake Mh. Meja Jenerali Marko Gaguti kwa namna ya kipekee kutokana na kufanya kazi iliyotukuka kwa kipindi chote alichokuwepo Mkoani hapa.

Katika hafla iliyofanyikia katika ukumbi wa Boma Mkoa August 4, 2022, Mwenyekiti wa chama hicho Bi Grace Kasembe amempa zawadi ya saa yenye picha yake Ili ikawe kumbukumbu ya kufanya kazi na waandishi kwa mafanikio makubwa.

Rais Samia Suluhu Hassan alimteua Brigedia Jen Marco Gaguti kuwa Mkuu wa Mkoa wa Mtwara mnamo Mei 15, 2021 akitokea Mkoa wa Kagera na sasa anarejea jeshini baada ya kupandishwa cheo na kuwa Meja Jenerali ili kuendelea na majukumu ya kijeshi.

Chama cha waandishi wa Habari Mkoa wa Mtwara kinamtakia kila la kheri katika majukumu yake

13/05/2022

Chama cha waandishi wa habari Mkoa wa Mtwara kimemtangaza mratibu wake mpya ndugu Abdallaah Nasoro kwa wanachama wake katika kilele cha maadhimisho ya siku ya Uhuru wa vyombo vya habari mkoani Mtwara mei 13, 2022.

Akizungumza mara baada ya kutambulishwa, Bwana Nassoro anayechukua nafasi ya Mwajuma Kitwana aliyemaliza muda wake, ameushukuru uongozi na wanachama wa MTPC huku akiomba ushirikiano ili kuendeleza na kuikuza taasisi.

Nae mratibu anaemaliza mkataba wake, Mwajuma kitwana ameshukuru kwa ushirikiano alioupata na kuahidi kuwa yeye bado ataendelea kuwa na waandishi wa Habari bega kwa bega.

Angalia katika video

https://www.facebook.com/UTPCTANZANIA

Umoja wa waandishi wa Habari Mkoani Mtwara (MTPC), leo mei 13, 2022 tunaadhimisha siku ya Uhuru wa vyombo vya habari Dun...
13/05/2022

Umoja wa waandishi wa Habari Mkoani Mtwara (MTPC), leo mei 13, 2022 tunaadhimisha siku ya Uhuru wa vyombo vya habari Duniani kwa kujifunza masuala mbalimbali juu ya Usalama kwa waandishi wa Habari.

Maadhimisho haya pia yanahudhuriwa na rais wa Umoja wa vilabu vya waandishi wa Habari Tanzania (UTPC) Deogratius Nsokolo.

Maadhimisho haya yanafanyika baada ya maadhimisho kitaifa na afrika kufayika mei 3,2022 jijini Arusha na kauli mbiu ya mwaka huu ni "waandishi wa Habari na changamoto za kidigiti"

Ahsante UTPC kwa kuwezesha maadhimisho haya kwa Mkoa wa Mtwara.
https://www.facebook.com/UTPCTANZANIA

Juma Mohamed mwandishi wa habari wa Clouds TV na Mwanachama wa Mtwara Press Club leo April 6, 2022 amepokea  tuzo pamoja...
06/04/2022

Juma Mohamed mwandishi wa habari wa Clouds TV na Mwanachama wa Mtwara Press Club leo April 6, 2022 amepokea tuzo pamoja na fedha taslimu ya shilingi Laki 5 kutoka kwa Mkuu wa Mkoa wa Mtwara Brigedia Jenerali Marco Elisha Gaguti baada ya kuibuka mshindi na kuwa mwandishi wa Habari Bora wa mkoa kwa kuandika habari za Elimu.

Gaguti ametoa tuzo hiyo wilayani Newala kwenye maadhimisho ya Juma la Elimulimu ambazo kimkoa zimefanyika katika wilaya hiyo.

21/02/2022

Official page for Mtwara Press Club

Address

Mtwara

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Mtwara Press Club posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share

Category