Teacher Jacob makweta

Teacher Jacob makweta Teacher Jb

30/10/2024
06/07/2024

Katika hali isiyo ya kawaida mtoto mmoja aliyefahamika kwa jina Frola Samson (12), mkazi wa wilaya ya Ilemela amepatikana baada ya msako wa Jeshi la polisi Mkoani Mwanza akiwa eneo la Buhongwa ambako alijificha yeye na mdogo wake aitwaye France Samson (8) huku akidanganya kuwa wametekwa na kutaka wazazi watume fedha ili waachiwe.

Inadaiwa kuwa watoto hao walitoweka nyumbani mnamo tarehe 4.7.2024, ambapo Frola aliiba pesa za Mama yake kiasi cha shilingi 150,000/= na kisha kutoweka na mdogo wake wakielekea Buhongwa ambako alianza kupiga simu kwa Mama yake mzazi akidai atumiwe pesa kwa ajili ya waliowateka ili wawaachie huru.

Hata hivyo Jeshi la Polisi mkoani humo baada ya kupokea taarifa na kufanya ufuatiliaji, limefanikiwa kuwapata watoto hao wakiwa salama huku wakiwa na simu, godoro na vyombo vingine vya matumizi ya ndani walivyonunua kwa kutumia pesa aliyoiba mtoto huyo.

22/05/2024

Mchezaji wa soka wa Tanzania Mmbwana Ally Samatta ambae anakupiga kwenye klabu ya PAOK ya nchini Ugiriki, amefanikiwa kutwaa taji la ligi Kuu ya Ugiriki akiwa na klabu hiyo (PAOK).

PAOK wametwaa Ubingwa wa ligi ya Ugiriki wakiwa na alama 80 kwenye jumla ya michezo 36 waliyocheza kwenye ligi wakiwaqcha nyuma kwa alama mbili AEK Athens ambao wameshika nafasi ya pili wakiwa na alama 78.

17/05/2024

Taarifa ya hali ya dawa za kulevya Duniani ya mwaka 2023 imeonesha kuwa takribani Watu milioni 219 walitumia bangi mwaka 2021, sawa na 4% ya idadi ya Watu duniani ambapo idadi hiyo imeongezeka kwa 21% katika kipindi cha muongo mmoja uliopita.

Taarifa hiyo ambayo imeandaliwa na Mamlaka ya kudhibiti na kupambana na dawa za kulevya Nchini (DCEA) na kuwasilishwa Bungeni Jijini Dodoma leo May 16,2024 na Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge na Uratibu Jenista J. Mhagama inaonesha kuwa matumizi ya bangi yanaendelea kuongezeka kwa kasi duniani kote na kwamba matumizi ya bangi yameendelea kuwa ya juu zaidi Amerika Kaskazini ambapo 17.4% ya Watu wenye umri kati ya miaka 15 hadi 64 walitumia bangi mwaka 2021.

Barani Afrika taarifa imeonesha kuwa Afrika Kaskazini ni kitovu cha biashara haramu ya bangi iliyosindikwa (cannabis resin) kuelekea Ulaya Magharibi na matumizi ya bangi ni ya juu katika Afrika Magharibi na Kati na kufikia mwaka 2021, karibu 10% ya Watu (milioni 30) waliripotiwa kutumia bangi katika kipindi cha mwaka 2020, hususan katika Nchi ya Nigeria.

Nchi nyingi Afrika zina uzalishaji wa bangi na imeendelea kuwa moja ya dawa inayosababisha athari kubwa miongoni mwa Watu wanaopatiwa matibabu ya uraibu.

17/05/2024

ENGLAND: Klabu zinazoshiriki Premier League zimeombwa kuunga mkono hoja iliyowasilishwa na Klabu ya Wolverhampton Wanderers inayopendekeza azimio la kupiga Kura ya kufuta Matumizi ya 'VAR' kuanzia Msimu ujao

Pendekezo hilo ambalo linadaiwa kupingwa na Bodi ya Ligi Kuu linatarajiwa kusikilizwa Juni 6, 2024 ambapo imeelezwa Bodi inatambua haki ya Wolves kutoa pendekezo hilo, lakini inadhani kufutwa kwa kunaweza kusababisha maamuzi mengi yasiyo sahihi

Aidha, baadhi ya Maafisa wa EPL wanadai pendekezo hilo litaathiri Ubora wa Ligi, pia kwa mujibu wa takwimu za Msimu huu zinaonesha kiwango cha maamuzi sahihi ya Uwanjani kimeongezeka kutoka 82% hadi 96 kupitia VAR

Soma https://jamii.app/VARAbolition

17/05/2024

Kutoka Huko tumekuletea hii. Achana na "Burj khalifa" Ambalo ni jengo Refu zaidi Duniani Kwa sasa likiwa na Mita zaidi ya 800+ kutoka Chini ya Ardhi kwenda juu

"Jeddah tower" hili ni limjengo likubwa sana linajengwa huko Saudi Arabia likikamilika litakuwa na Urefu wa kilometer (1) kutoka Ardhini kwenda juu Angani , hii ni hatari sana Litakuwa ni jengo Refu zaidi kujengwa duniani

Hebu subiri kwanza - ujue kilometer Moja ni parefu sana ?🤔
hili dude litakuwaje unadhani ? Hebu toa maoni yako kwenye comment je unaweza Kuishi juu kwenye jengo hili ?

Imeandikwa na 🖋️ " Mnyilinga - Max "

17/05/2024

DODOMA; KATIKA kipindi cha Julai, 2023 hadi Aprili, 2024 Watanzania 63 walipatiwa uraia wa nchi nyingine baada ya kuukana Uraia wa Tanzania ikilinganishwa na Watanzania 58 walioukana uraia wa Tanzania 66 mwaka 2022/23.
-
Nchi hizo ni: Botswana (1), Canada (15), India (2), Kenya (3), Marekani (5), Mauritius (1), Oman (25), Pakistan (1), Uganda (1) na Ujerumani (9). Kwa msingi huo, watu hao wanakosa sifa ya kuendelea kuwa raia wa Tanzania kwa mujibu wa Sheria ya Uraia, Sura ya 357 Rejeo la 2002.
-
Kauli hiyo imetolewa na Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Mhandisi Hamad Masauni leo bungeni mjini Dodoma, takati akiwasilisha makadirio ya mapato na matumizi kwa mwaka wa Fedha 2024/2025.
-
Imeandaliwa na Waandishi Wetu, Dodoma
-
Una maoni, tuandikie
-

17/05/2024

Unatoa asilimia ngapi kwa Robot Eunice?

17/05/2024
17/05/2024

DODOMA: SERIKALI imewataka Watanzania wasiwe na hofu kutokana na ujio wa roboti za teknolojia ya Akili Bandia au Akili Mnemba (AI) kwa kudhani watanyang'anywa ajira zao.
-
Kauli hiyo imetolewa leo mjini Dodoma na Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Nape Nnauye alipokuwa akizungumza na Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC).
-
"Mashine hizi ni kwa ajili ya kurahisisha kazi ambazo zingemfanya mtu kuamka na kufuata kitu, lakini anaweza kuendelea kufanya kazi, huku akiliagiza roboti mafaili na mzigo mwingine ili kuongeza uzalishaji na kuchochea maendeleo ya taifa letu," amesema Waziri Nape.
-
Leo Waziri Nape amewasilisha bungeni makadirio ya mapato na matumizi ya fedha kwa mwaka wa fedha 2024/2025 kwa Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari.
-
Imeandaliwa na Genevieve Kisaka
-
/25

Address

Mwanza

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Teacher Jacob makweta posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Teacher Jacob makweta:

Share