26/05/2026
1.Professor Jay alizaliwa mwaka 1975, kwasasa ana umri wa miaka 50
2.Alianza muziki mwanzoni mwa miaka ya 1990s. Mwaka 1994 alijiunga katika kundi la Hard Blasters Crew, waliachia kazi mbalimbali ukiwemo Chemsha Bongo uliofanya vizuri
3.Mwaka 2001 alianza kazi k**a msanii anayejitegemea(solo artist), aliachia albamu yake ya kwanza ambayo humo ndani kulikuwa na nyimbo maarufu zikiwemo Bongo Dar es salaam, Piga Makofi na Ndio Mzee ambao ulifanya ashinde tuzo
4.Producer Master J aliweka wazi kwamba moja ya nyimbo bora alizowahi kutengeneza ni wimbo wa Bongo Dar es salaam wa mwanamuziki huyo wa hip hop
5. Mapinduzi Halisi ilikuwa albamu yake ya pili ambayo ilitoka 2003, ilishinda Kili Music Awards k**a albamu bora ya hip hop. Miongoni mwa nyimbo zilizopendwa zaidi ni Promota Anabeep, Msinitenge na Zali La Mentali ambao alioshirikiana na Juma Nature, Nargis Mohamed alianza kufahamika kupitia wimbo huu akiwa video queen kabla ya kufanya vizuri Miss Tanzania
6. Albamu nyingine alizotoa ambazo zilifanya vizuri ni pamoja na J.O.S.E.P.H ambayo moja ya nyimbo maarufu humo ni ule wa Nikusaidieje ulioshinda tuzo kadhaa. Albamu zake nyinginezo ni Aluta Continua, Izack Mangesho na Kazi Kazi ambazo pia zilikuwa na nyimbo zilizopokelewa vizuri
7.Professor Jay upitia nyimbo zake anatajwa kuwa msanii wa hip hop Tanzania aliyeweza kushawishi hata watu wenye umri mkubwa kufuatilia muziki huo kwani alikuwa na uandishi wa kipekee na wenye kubeba ujumbe unaogusa nyanja mbalimbali katika jamii
8.Ni miongoni mwa wanamuziki wachache nchini ambao wameweza kukubalika katika generations tofauti tofauti kutokana na kipaji na uwezo wake kisanaa
9.Kwa uwezo wake kimuziki, huwa anapewa heshima kubwa na wasanii wenzake sio tu Tanzania, hata nchi nyingine za Afrika mashariki ambako kazi zake zilifanya vizuri, kutumbuiza na kushirikiana na wanamuziki wa huko akiwemo Jose Chameleon wa Uganda
10. Sugu Joseph Mbilinyi na Lady Jay Dee(Jidee) ni miongoni mwa marafiki zake wa karibu katika tasnia pia walishirikiana kikazi nyakati tofauti
11. Katika maisha binafsi, Profesa Jay alifunga ndoa na Grace Mgonjo ambaye ni mshereheshaji(MC) anayefahamika, wana mtoto wa k**e mkubwa anayeitwa Lisa ambaye amefika elimu ya chuo kikuu. Jay ni mtu ambaye amekuwa akionekana kuwa karibu na familia yake ikiwemo kumpongeza binti yao kufanya vizuri kitaaluma
12. Mwaka 2015 professor Jay alishinda ubunge wa Mikumi akawa mmoja wa wanamuziki wachache walioshinda nafasi hiyo kupitia majimboni