23/01/2026
Rais wa Jamhuri ya Senegal, Bassirou Diomaye Faye, akiwa pamoja na wake zake wawili, Marie Khone Faye na Absa Faye. \n\nHii ni k**a YAKOBO alivyowaoa wake zake wawili, RAHEL (RECHO) na LEAH.., Hadithi ya YAKOBO na RAHELI kidogo ni ngumu. Je, unaweza kufanya kazi miaka 7 ukweni bila malipo kwa ahadi ya kupewa mke? Halafu miaka 7 inakatika, baba mkwe anasema akupe bintie wa kwanza umuoe kwanza siyo yule wa pili umpendae. Baba mkwe (LABAN) alimueleza YAKOBO kwa taratibu zao, mtoto wa kwanza (LEA) ndiyo anatakiwa kuolewa kwanza. YAKOBO akasema sawa, nipeni huyo, halafu akachukua miaka mingine 7 ya kufanya kazi bila malipo ili kumpata RAHEL. Jumla alifanya kazi ukweni miaka 14 kusubiri akabidhiwe kipenzi chake. Kwa kila mke mmoja, alipewa suria (msaidizi) mmoja. Masuria pia aliwafanya wake zake. Hivyo alikuwa na wake wanne (4) waliomzalia watoto 12 ambayo ndiyo mgawanyo wa makabila 12 ya ISRAELI leo. YAKOBO ni role model wangu. Anyways, hiyo hadithi utaipata katika kitabu cha Mwanzo. Tusome BIBLIA ndugu zangu.